Buriani Asayyid Sharif Hussein Ahmad Badawiy

Buriani Asayyid Sharif Hussein Ahmad Badawiy

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
BURIANI ASAYYID SHARIF HUSSEIN AHMAD BADAWIY​

Shariff Hussein Badawiy kaacha athari kubwa sana Dar es Salaam katika usomeshaji wa Qur'an Msikiti wa Badawiy (sasa Rawdha) hadi pale alipofukuzwa Tanganyika mwaka wa 1963 yeye na mdogo wake Mwinyibaba.

Masjid Badawiy ilisifika sana kwa kutoa wasomaji bingwa wa tajwid.

Nilibahatika siku moja kuzungumza na Shariff Hussein jirani ya msikiti wa Ibadh nilipomkuta kasimama nje na mtu mmoja.

Huyu bwana alikuwa rafiki yangu Sheikh Mtangala maarufu kwa jina la Kawawa.

Nilikwenda pale kumwamkia kisha nishike hamasini zangu lakini Sheikh Mtangala aliyekuwa anazungumzanae akanizuia nisiondoke ili nisikilize mazungumzo yao.

Nilibakia. Nilifaidika sana siku ile kwani nilimsikia mwenyewe akieleza mengi aliyoona wakati ule na pigo alilopata kwa kufukuzwa Tanganyika.

Msikiti wa Badawiy palikuwa na moja ya darsa kubwa mjini Dar es Salaam ambako Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alikokuwa akisomesha tafsir ya Qur'an.

Darsa hii ilikuwa inajaza msikiti na wanafunzi wake walikuwa masheikh wakubwa wa nyakati zile.

August Nimtz aliyeandika kitabu maarufu, ''Islam and Politics in East Africa The Sufi Order in Tanzania'' (1980) ameitaja hii madrasa katika kitabu chake.

Mwanafunzi wa mwisho naamini kufariki katika kundi hili la masheikh wa wakati ule ni Shariff Adnan ambae alibaki pale msikitini kama Imam Mkuu hadi kifo chake miaka michache iliyopita.

Nimepata kumpiga picha Shariff Hussein Lamu na Dar es Salaam baada ya yeye kurejea.
In Shaa Allah nitaziweka hapa baadhi kwani picha inasema maneno elfu moja.

Shariff Hussein baada ya kurejea Tanzania katika miaka ya 1980 alifungua madrasa Lushoto na akaanza kusomesha upya.

Allah amfanyie wepesi safari yake.

Angalia picha:

Screenshot_20210210-103743.jpg
Screenshot_20210210-104645.jpg
Screenshot_20210210-104534.jpg
 
Kaka Mohamed,

Nimefanikiwa kuingia JF leo nikakutana na habari za kusikitisha za kifo cha Seyyid Hussein Badawi(Mungu Amrahamu). Ni vigumu kumuelezea Aalim huyu kwa maneno machache. Itoshe kusema kua ni miongoni mwa Wanazuoni wachache wa kikwelikweli, Wacha Mungu, na waliofanya kazi kubwa sana kueneza Uislamu Afrika Mashariki

Seyyid Hussein Badawi alikuja Tanzania kama mchezaji winga wa timu ya Cosmo Politan miaka ya 1960s, na wazee wanaomjua wanasema ilikua ikifika wakati wa swala kama mpira unaendelea atatoka uwanjani aende kwenye ibada. Binafsi nilikutana na familia yake katika mji wa Bunia DRC ambapo aliwahi kuishi(na mji wa Beni pia) na kufanya kazi za kutangazaa kufundisha Uislamu kwa mafanikio makubwa sana

Familia yao yote kwa maana ya ndugu zake wakike na wa kiume ni watu wenye shime na elimu kubwa sana ya Kiislamu. Baadhi yao ni pamoja na Seyyid Ahmad Bin Ahamad Badawi(Mwenye Baba), Muhammad Badawi na pia mpwa wao Al Imaam Raahil, Seyyid Muhammad Bin Sharif Said Al Biidh ambaye alikua ni "Janazuoni Kuubwa sana"(kwa lahaja ya Ki Amu au Lamu)

Lushoto kwenye Madrasa kubwa saana iliyoasisiwa na Seyyid Hussein ambapo wanakaa wanafunzi zaidi ya 100 kutoka nchi mbalimbali hua kunafanyika miongoni mwa mambo mengine Maulid maarufu ikiitwa Maulid ya Padri. Huyu ni Padri Mzungu wa Kanisa Katoliki Vuga Lushoto na aliyekuwa swahiba wa Seyyid Hussein naye hufanya Maulid ya Kuadhimisha Mazazi ya Mtume Muhammad SAW. Ni tukio la kusisimua sana

Allah Amuwie Radhi Seyyid Hussein Badawi na Ajaalie kaburi lake liwe miongoni mwa mabustani ya peponi. Aamin
 
Back
Top Bottom