Buriani Mohamed Mrisho

Buriani Mohamed Mrisho

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
BURIANI MOHAMED MRISHO
Kifo hakizoeleki.

Taarifa ya kifo cha Mohamed Mrisho nimekisoma kutoka ukurasa wa Vuli Yeni akiandika kutoka Johannesburg.

Sijui hata nianzie wapi.

Mohamed Mrisho alikuwa katika bendi ya The Revolutions ya vijana kutoka Tanga wengi wao kama Hemedi Chuki, Mabruki na Waziri Ali wote wametangulia mbele ya haki.

Hawa wote nimejuananao toka miaka ya 1970 na nilikuwa nikipenda sana muziki wao.

Nakumbuka wakati nasoma Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM) chumbani kwangu nilikuwa na stereo system na collection kubwa ya muziki wa jazz.

Mara moja moja wakinipitia kunisalimia na tusikiliza pamoja jazz kutoka wapigaji maarufu wa nyakati zile kama Bob James, Earle Klugh, George Benson na Groover Washington.

Hivi ndivyo nilivyomfahamu Mohamed Mrisho na kwa miaka mingi tukawa marafiki tukikutana sote tunafurahi na kuzungumza mengi.

Nakikumbuka kisa kimoja.

Katika miaka ya 1980s nilikuwa nakaa Hotel 77 Arusha na The Revolutions walikuwa Resident Band wakitumbuiza pale wakati wa ''diner'' yaani chakula cha jioni.

Ikawa kila jioni wakati wa chakula cha usiku nakwenda kuwasikiliza.

Miaka ile Earle Klugh na Bob James walikuwa wametoa album yenye nyimbo zilizowapendeza wapenda jazz wengi.

Mohamed Mrisho kwenye guitar na Waziri Ali kwenye keyboard ukiwasikiliza wakipiga hizi nyimbo utasema wenyewe Earle Klugh na Bob James wako Arusha pale wanatumbuiza.

Hawa rafiki zangu walikuwa na vipaji vya ajabu sana katika upigaji wa ala zao.

Wakati wa jioni walikuwa wanafanya mazoezi.

Siku moja nikaenda kuwasikiliza.

Walipomaliza wanataka kufunga vyombo mimi nikalinyanyua guitar lake Mohamed Mrisho.

Nikaanza kupiga ''introduction'' utangulizi wa nyimbo moja maarufu na The Revolutions wakiipiga - ''Summer Time,'' tofauti mimi nilipiga ''version'' ya Sam Cooke.

Ile kupiga ''chord'' za mwanzo tu.

Wote walishtuka wakageuka kuniangalia wengine midomo wazi.

''Mohamed unajua guitar.''
Mimi nilicheka sikuwa na la kusema.

Miaka ikapita nilirudi na keyboard kutoka Uingereza nikakutana na Waziri Ali Mtaa wa Mosque.

Muda mrefu tulikuwa hatujaonana.

Katika mazungumzo nikamwambia kuwa nimenunua keybord iko nyumbani.

Haraka akaniuliza aina gani?
''Casio,'' nilimjibu.

Waziri alicheka akaniambia, ''Mohamed Casio hiyo wanapiga watoto wadogo ungenunua Roland au Yamaha.''

Ikawa zamu yangu kucheka.

Mara ya mwisho kuwasikia hawa rafiki zangu wawili wakipiga pamoja ilikuwa miaka 14 iliyopita kwenye harusi ya bint yake Yanga Bwanga, Tanga Resort.

Siku ile niliwapiga hiyo picha hapo chini.

Tunamuomba Allah awasamehe ndugu zangu hawa dhambi zao na awatie peponi:

1725287137432.jpeg

1725287181243.jpeg
 
BURIANI MOHAMED MRISHO
Kifo hakizoeleki.

Taarifa ya kifo cha Mohamed Mrisho nimekisoma kutoka ukurasa wa Vuli Yeni akiandika kutoka Johannesburg.

Sijui hata nianzie wapi.

Mohamed Mrisho alikuwa katika bendi ya The Revolutions ya vijana kutoka Tanga wengi wao kama Hemedi Chuki, Mabruki na Waziri Ali wote wametangulia mbele ya haki.

Hawa wote nimejuananao toka miaka ya 1970 na nilikuwa nikipenda sana muziki wao.

Nakumbuka wakati nasoma Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM) chumbani kwangu nilikuwa na stereo system na collection kubwa ya muziki wa jazz.

Mara moja moja wakinipitia kunisalimia na tusikiliza pamoja jazz kutoka wapigaji maarufu wa nyakati zile kama Bob James, Earle Klugh, George Benson na Groover Washington.

Hivi ndivyo nilivyomfahamu Mohamed Mrisho na kwa miaka mingi tukawa marafiki tukikutana sote tunafurahi na kuzungumza mengi.

Nakikumbuka kisa kimoja.

Katika miaka ya 1980s nilikuwa nakaa Hotel 77 Arusha na The Revolutions walikuwa Resident Band wakitumbuiza pale wakati wa ''diner'' yaani chakula cha jioni.

Ikawa kila jioni wakati wa chakula cha usiku nakwenda kuwasikiliza.

Miaka ile Earle Klugh na Bob James walikuwa wametoa album yenye nyimbo zilizowapendeza wapenda jazz wengi.

Mohamed Mrisho kwenye guitar na Waziri Ali kwenye keyboard ukiwasikiliza wakipiga hizi nyimbo utasema wenyewe Earle Klugh na Bob James wako Arusha pale wanatumbuiza.

Hawa rafiki zangu walikuwa na vipaji vya ajabu sana katika upigaji wa ala zao.

Wakati wa jioni walikuwa wanafanya mazoezi.

Siku moja nikaenda kuwasikiliza.

Walipomaliza wanataka kufunga vyombo mimi nikalinyanyua guitar lake Mohamed Mrisho.

Nikaanza kupiga ''introduction'' utangulizi wa nyimbo moja maarufu na The Revolutions wakiipiga - ''Summer Time,'' tofauti mimi nilipiga ''version'' ya Sam Cooke.

Ile kupiga ''chord'' za mwanzo tu.

Wote walishtuka wakageuka kuniangalia wengine midomo wazi.

''Mohamed unajua guitar.''
Mimi nilicheka sikuwa na la kusema.

Miaka ikapita nilirudi na keyboard kutoka Uingereza nikakutana na Waziri Ali Mtaa wa Mosque.

Muda mrefu tulikuwa hatujaonana.

Katika mazungumzo nikamwambia kuwa nimenunua keybord iko nyumbani.

Haraka akaniuliza aina gani?
''Casio,'' nilimjibu.

Waziri alicheka akaniambia, ''Mohamed Casio hiyo wanapiga watoto wadogo ungenunua Roland au Yamaha.''

Ikawa zamu yangu kucheka.

Mara ya mwisho kuwasikia hawa rafiki zangu wawili wakipiga pamoja ilikuwa miaka 14 iliyopita kwenye harusi ya bint yake Yanga Bwanga, Tanga Resort.

Siku ile niliwapiga hiyo picha hapo chini.

Tunamuomba Allah awasamehe ndugu zangu hawa dhambi zao na awatie peponi:

Nashukuru kusikia kuwa ulikuwa na kipaji cha muziki hususan kupiga guitar
 
Pole sana Mzee Mohamed Said kwa kuondokewa na marafiki zako.

Toka maktaba :
VULI YENI'S MUSIC JOURNEY FROM DAR ES SALAAM TANZANIA TO THE WIDER WORLD

INTERVIEW AT MABOPANE COMMUNITY RADIO STATION


View: https://m.youtube.com/watch?v=ZXCg5wkiekw

Source : Vuli Yeni


1725297320601.png

The Revolutions, Kilimanjaro Hotel, Dar es Salaam, 1979. Left to right: Mohammed Mrisho (guitar), Hemedi Chuki (lead vocals), Vuli Yeni (organ), Ibrahim Mtumwa (drums) and Joe 'Ball' Ribeiro (bass guitar). Source: Photograph courtesy of Vuli Yeni​

 
Vuli Yeni akiandika kutoka Johannesburg.

Mwanamuziki wa kutoka Afrika ya Kusini bwana Vuli Yeni akiwa live na Lucky Dube mkali wa reggae duniani Vuli Yeni alikulia Tanzania.


LUCKY DUBE LIVE



Lead vocal : Lucky Dube
Keyboards: Thuthukani Cele
Keyboards: Eugene Mthethwa
Percussion : Chris Dlamini
Saxophone: Vulindela (Vuli) Yeni
Trombone: Robert Jabu Mdluli
Trumpet: Ndumiso Nyovane
Guitar Bass: Jabulani Sibumbe
Lead Guitar: Sandile Dhlamini
Drums: Isaac Mtshali
Backing Vocalsa: Nolusindiso Gaeza, Cynthia Malope, Kabanina Ntsele
Manager: Richard Siluma
 
Wapumzike kwa amani... ila uzuri wa hili andiko lako ni flow ya usimuliaji haichoshi... uandishi murua sana.
Ni mwandishi mzuri sana sana. Anajua kuumba wahusika, anafanya msomaji ajione kama anaangalia movie anayotamani isiishe hapo hapo anataka ajue mwisho wake. Vipaji kama hivi Tanzania hatuna vingi.
 
Mwanamuziki wa kutoka Afrika ya Kusini bwana Vuli Yeni akiwa live na Lucky Dube mkali wa reggae duniani Vuli Yeni alikulia Tanzania.


LUCKY DUBE LIVE



Lead vocal : Lucky Dube
Keyboards: Thuthukani Cele
Keyboards: Eugene Mthethwa
Percussion : Chris Dlamini
Saxophone: Vulindela (Vuli) Yeni
Trombone: Robert Jabu Mdluli
Trumpet: Ndumiso Nyovane
Guitar Bass: Jabulani Sibumbe
Lead Guitar: Sandile Dhlamini
Drums: Isaac Mtshali
Backing Vocalsa: Nolusindiso Gaeza, Cynthia Malope, Kabanina Ntsele
Manager: Richard Siluma

1725335323591.jpeg

Kulia Vuli Yeni, Waziri Ali na Mohamed Said Chef Pride Restaurant 2021​
 
Ni mwandishi mzuri sana sana. Anajua kuumba wahusika, anafanya msomaji ajione kama anaangalia movie anayotamani isiishe hapo hapo anataka ajue mwisho wake. Vipaji kama hivi Tanzania hatuna vingi.
Hakika mkuu
Ni mwandishi mzuri sana sana. Anajua kuumba wahusika, anafanya msomaji ajione kama anaangalia movie anayotamani isiishe hapo hapo anataka ajue mwisho wake. Vipaji kama hivi Tanzania hatuna vingi.
Unatamani usome halafu mwishoni ukutane na neno itaendelea hahahaaa.
 
Je ulikuwa unacheza vyombo hivi kama relaxation tu? au ulikuwa na uwezo wa kupanda jukwaani kama akina Waziri Ally?
Huihui...
Nikipiga kujifurahisha na kuwafunza wengine.

Waziri Ali alipata kuniambia kuwa mimi mwenyewe sikutaka lakini nilikuwa na kipaji.

Nilikuwa na hamu kubwa ya kurekodi nyimbo mbili mimi nikiimba na Waziri akini-back na keyboard: "A Whiter Shade of Pale" ya Procol Harum na "Autumn Leaves" ya Nat King Cole.

Sikujaaliwa.
 
View attachment 3085420
Kulia Vuli Yeni, Waziri Ali na Mohamed Said Chef Pride Restaurant 2021​

Mzee Mohamed Said una mengi sana kutuambia kupitia kalamu, makala na video kuhusu jiji la Dar es Salaam enzi zenu za ujana, sisi tunasimuliwa kwa mdomo mitaani tukikaa na wazee wetu ila wewe unaitumia kalamu vizuri kwa makala kemkem za kila aina.

Kila la kheri endelea kutuletea makala na habari maana jamii isipoandika historia inakuwa jamii isiyo kamili

Rafiki yako Vuli Yeni analalamika katika interview kuwa pamoja ya kuwa Dar es Salaam ilikuwa kama Mecca kwa vyama vya ukombozi wa Kusini mwa Afrika mfano waafrika ya Kusini lakini hakuna maandiko ya kutosha hali ilikuwaje Dar es Salaam na miji mingine ilipojaa wakimbizi kutoka nchi za Afrika na hata wale wakimbizi weusi wa Black panther toka USA.
 
Pole sana Mzee Mohamed Said kwa kuondokewa na marafiki zako.

Toka maktaba :
VULI YENI'S MUSIC JOURNEY FROM DAR ES SALAAM TANZANIA TO THE WIDER WORLD

INTERVIEW AT MABOPANE COMMUNITY RADIO STATION


View: https://m.youtube.com/watch?v=ZXCg5wkiekw

Source : Vuli Yeni


View attachment 3085250

The Revolutions, Kilimanjaro Hotel, Dar es Salaam, 1979. Left to right: Mohammed Mrisho (guitar), Hemedi Chuki (lead vocals), Vuli Yeni (organ), Ibrahim Mtumwa (drums) and Joe 'Ball' Ribeiro (bass guitar). Source: Photograph courtesy of Vuli Yeni​


Astakafilulah
Waislamu waimba nyimbo za dunia badla ya kaswida au kuimba albadiri
 
Huihui...
Nikipiga kujifurahisha na kuwafunza wengine.

Waziri Ali alipata kuniambia kuwa mimi mwenyewe sikutaka lakini nilikuwa na kipaji.

Nilikuwa na hamu kubwa ya kurekodi nyimbo mbili mimi nikiimba na Waziri akini-back na keyboard: "A Whiter Shade of Pale" ya Procol Harum na "Autumn Leaves" ya Nat King Cole.

Sikujaaliwa.
Mambo yako yote safi, tunapishana tu unapotaka kubadili historia ya uhuru wa Tanganyika/ Tanzania. Unatetea sana wazee wako
 
Mambo yako yote safi, tunapishana tu unapotaka kubadili historia ya uhuru wa Tanganyika/ Tanzania. Unatetea sana wazee wako
Huihui,
Kwani huamini kuwa historia ya kweli ilifutwa?
 
Back
Top Bottom