Burkina Faso kununua mabasi 500 kwa ajili ya kurahisisha usafiri kwa wanafunzi

Burkina Faso kununua mabasi 500 kwa ajili ya kurahisisha usafiri kwa wanafunzi

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Serikali ya Burkina Faso inayoongozwa na Kapteni Ibrahim Traore inatarajia kununua mabasi 500 kwa ajili ya kurahisisha usafiri na kuondoa adha wapatayo wanafunzi hasa waishio maeneo ya mijini.

Hayo yamesemwa wakati wa utoaji wa ripoti ya kikao cha kawaida cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika tarehe 5 Disemba 2024 na kuongozwa na Kapteni Ibrahim Traore.

Mabasi hayo yatanunuliwa kwa awamu mbili ambapo katika kila awamu takribani mabasi 250 yatanunuliwa.

Mwezi uliopita baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyopo mji mkuu wa Ouagadougou nchini Burkina Faso waligoma kulalamikia adha ya usafiri wanayoipata kutokana na kutokuwepo kwa mabasi ya kutosha yaliyotengwa maalum kwa ajili yao.

Chanzo/ Source: Shirika la habari la Burkina Faso ( RTB)
 
Serikali ya Burkina Faso inayoongozwa na Kapteni Ibrahim Traore inatarajia kununua mabasi 500 kwa ajili ya kurahisisha usafiri na kuondoa adha wapatayo wanafunzi hasa waishio maeneo ya mijini.

Hayo yamesemwa wakati wa utoaji wa ripoti ya kikao cha kawaida cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika tarehe 5 Disemba 2024 na kuongozwa na Kapteni Ibrahim Traore.

Mabasi hayo yatanunuliwa kwa awamu mbili ambapo katika kila awamu takribani mabasi 250 yatanunuliwa.

Mwezi uliopita baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyopo mji mkuu wa Ouagadougou nchini Burkina Faso waligoma kulalamikia adha ya usafiri wanayoipata kutokana na kutokuwepo kwa mabasi ya kutosha yaliyotengwa maalum kwa ajili yao.

Chanzo/ Source: Shirika la habari la Burkina Faso ( RTB)
Wakwetu kazi yake ni kula na 💩 tu
 
Kununua mabasi ya wanafunzi nayo ni habari? Tena anatajwa Rais kabisa! Hizo si kazi za kila siku za mamlaka za miji na wilaya? Mbona hata private schools wananunua kila mwaka? Bara giza kweli hili.
Kwani hapo ulipo mamlaka za miji na wilaya washanunua mabasi yao kwa ajili ya wanafunzi..?
 
Kununua mabasi ya wanafunzi nayo ni habari? Tena anatajwa Rais kabisa! Hizo si kazi za kila siku za mamlaka za miji na wilaya? Mbona hata private schools wananunua kila mwaka? Bara giza kweli hili.
Mwenzetu uko wilaya gani ambapo wananunua mabasi kwa ajili ya wanafunzi wa shule za serikali? Nataka nihamie
 
Kununua mabasi ya wanafunzi nayo ni habari? Tena anatajwa Rais kabisa! Hizo si kazi za kila siku za mamlaka za miji na wilaya? Mbona hata private schools wananunua kila mwaka? Bara giza kweli hili.
Ukitaka kujua umuhimubwa matako, jaribu kukalia kichwa.

Hapa TZ lini serikali ilinunua walau Mabasi 50 tu ya wanafunzi?
 
Tatizo sio kuanzisha mradi, tatizo linaanza kwenye kuuendesha (maintenance). Yasije kutokea kama ya Dart.
 
Kununua mabasi ya wanafunzi nayo ni habari? Tena anatajwa Rais kabisa! Hizo si kazi za kila siku za mamlaka za miji na wilaya? Mbona hata private schools wananunua kila mwaka? Bara giza kweli hili.
Kufuatia adha waipatayo wakazi wa Kigamboni hasa baada ya MV Kigamboni kwenda matengenezo, waziri alipita pale Kigamboni na kuongea na wakazi wa Kigamboni, nae alimtaja mama. Hata mimi nilijiuliza swali hilo hilo, sasa hapa rais wa nchi anatajwa ili afanye nini? Kivuko sio jambo jipya, vivuko hivo vimekuwepo hapo over 50 years, waziri anamtaja rais ili iweje? Sikuelewa hadi leo yaani
 
Back
Top Bottom