BURKINAFASO: Takriban Wanakijiji 30 wauawa baada ya kushambuliwa na Wanamgambo

BURKINAFASO: Takriban Wanakijiji 30 wauawa baada ya kushambuliwa na Wanamgambo

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Wanamgambo wanaosadikika wa kundi la Jihad wamevamia kijiji mashariki mwa Burkinafaso na kuua wanakijiji wanaokadiriwa 30.

‘Kundi kubwa la watu wenye silaha lilivamia kijiji cha Kodyel jimbo la Komandjari jumatatu asubuhi na kufanya shambulio liligharimu maisha ya watu wanaokadiriwa kufikia 30. Kama idadi ya vifo ipo sahihi hili linakua shambulio la hatari zaidi kuwahi kutokea nchini’alisema afisa habari.

Mashambulio ya kiislamu yameongezeka nchini hasa mikoa inayopakana na nchi za Niger na Mali. Shambulio hili linakuja wiki moja baada ya waandishi wawili wa habari raia wa Ireland waliokua sehemu ya doria dhidi ya ujangili kuuawa nchini humo.
 
Jamaa wanazidi kushamiri, mdogomdogo mwisho wa siku wanamiliki west au east Africa.
 
Wanamgambo wanaosadikika wa kundi la Jihad wamevamia kijiji mashariki mwa Burkinafaso na kuua wanakijiji wanaokadiriwa 30.

‘Kundi kubwa la watu wenye silaha lilivamia kijiji cha Kodyel jimbo la Komandjari jumatatu asubuhi na kufanya shambulio liligharimu maisha ya watu wanaokadiriwa kufikia 30. Kama idadi ya vifo ipo sahihi hili linakua shambulio la hatari zaidi kuwahi kutokea nchini’alisema afisa habari.

Mashambulio ya kiislamu yameongezeka nchini hasa mikoa inayopakana na nchi za Niger na Mali. Shambulio hili linakuja wiki moja baada ya waandishi wawili wa habari raia wa Ireland waliokua sehemu ya doria dhidi ya ujangili kuuawa nchini humo.

Sawa
 
Jamaa wana pamba moto wanazidi kuishika Africa.Huku kwetu Tz kama ikiwezekana style ile ile ya Kibiti wamalizane nao huko huko maporini.
 
Burkina Faso ndo taifa pekee lenye wakristo wengi katika nchi za Sahel (Mali, Gueanea, Senegal, Chad na Mauritania) na ndio Target ya hawa magaidi.

Yesu awalinde na awatangulie.
 
Ni ajabu vijana wanarubuniwa kuwaua ndugu zao kwa jina la dini! Kwanini?
Hawajui kwamba ingetokea wamezaliwa katika India Basi wangekuwa wahindu na pengine wangezaliwa saudia wangekuwa waislam.
Kila nikijiuliza sipati jibu je Kuna anayewatuma? Kwamba Leo kaueni mtaa mzima mungu atawajaalia thawabu na ridhki?
 
East Africa hawawezi labda ipite miaka 300
Huko east Afrika mna Nini anawezekana Marekani.. anafuatwa nyumbani anapigika.?
Omba tu mungu mkuu isitoshe Hawa Mara nyingi wanatumika na wazungu kulinda maslahi y kiuchumi
 
Ni ajabu vijana wanarubuniwa kuwaua ndugu zao kwa jina la dini! Kwanini?
Hawajui kwamba ingetokea wamezaliwa katika India Basi wangekuwa wahindu na pengine wangezaliwa saudia wangekuwa waislam.
Kila nikijiuliza sipati jibu je Kuna anayewatuma? Kwamba Leo kaueni mtaa mzima mungu atawajaalia thawabu na ridhki?
Hakuna kitu kama hicho chief, ni ukosefu wao wa elimu ya dini hiyo wanayojidai wanaipambania..

Kuna mengi nyuma ya pazia, ila kubwa ni kukosa elimu sahihi.. Hapa nitumie neno sahihi.
 
Hakuna kitu kama hicho chief, ni ukosefu wao wa dini hiyo wanayojidai wanaipambania..

Kuna mengi nyuma ya pazia, ila kubwa ni kukosa elimu sahihi.. Hapa nitumie neno sahihi.
Bila shAka Ni elimu potofu waipatayo kutoka wapi?
 
Back
Top Bottom