Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Mwili wa aliyekuwa Rais wa Burundi hayati Pierre Nkurunziza unazikwa leo kwenye makaburi ya mji wa Gitega ,mji mkuu wa kisiasa ulioko katikati mwa Burundi
Hafla ya mazishi zinatarajiwa kuongozwa na Rais mpya Jenerali Evariste Ndayishimiye na wakuu wengine wa serikali.
Hayati Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 mwezi huu ,miezi miwili kabla ya kukabidhi madaraka kwa mrithi wake kufwatia uchaguzi uliofanyika mwezi wa tano.
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na serikali ya Burundi, hafla itaanzia kwenye 'hospital du Cenquantenaire Twese Turashoboye' iliyoko kwenye mkoa wa Karusi ambako maiti yake imehifadhiwa.
Mlolongo wa magari yatakayosindikiza maiti yake utatoka kwenye hospitali hiyo utatoka Karusi na kuelekea katika mji wa Gitega ambao ni mji mkuu wa kisiasa katikati mwa Burundi.
Wananchi wameomba kusimama kwenye barabara kumuaga marehemu.
Kunatarajiwa hafla fupi ya jeshi kumtolea heshma za mwisho kwenye uwanja wa mpira wa Ingoma mjini Gitega,kabla ya mwili wake kupitishwa mbele ya wananchi watakaokuwa uwanjani humo kumwaga na baadae kufanyika maziko rasmi.
Tangazo la serikali ya Burundi linasema kwamba shughuli nyingine kama kuweka mashada ya maua kwenye kaburi lake au hotuba zitakazotolewa zitafahamishwa leo.
Rais Pierre Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 mwezi huu kutokana na mshtuko wa moyo kama ilivyotangazwa na serikali ya nchi hiyo.
Hafla ya mazishi zinatarajiwa kuongozwa na Rais mpya Jenerali Evariste Ndayishimiye na wakuu wengine wa serikali.
Hayati Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 mwezi huu ,miezi miwili kabla ya kukabidhi madaraka kwa mrithi wake kufwatia uchaguzi uliofanyika mwezi wa tano.
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na serikali ya Burundi, hafla itaanzia kwenye 'hospital du Cenquantenaire Twese Turashoboye' iliyoko kwenye mkoa wa Karusi ambako maiti yake imehifadhiwa.
Mlolongo wa magari yatakayosindikiza maiti yake utatoka kwenye hospitali hiyo utatoka Karusi na kuelekea katika mji wa Gitega ambao ni mji mkuu wa kisiasa katikati mwa Burundi.
Wananchi wameomba kusimama kwenye barabara kumuaga marehemu.
Kunatarajiwa hafla fupi ya jeshi kumtolea heshma za mwisho kwenye uwanja wa mpira wa Ingoma mjini Gitega,kabla ya mwili wake kupitishwa mbele ya wananchi watakaokuwa uwanjani humo kumwaga na baadae kufanyika maziko rasmi.
Tangazo la serikali ya Burundi linasema kwamba shughuli nyingine kama kuweka mashada ya maua kwenye kaburi lake au hotuba zitakazotolewa zitafahamishwa leo.
Rais Pierre Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 mwezi huu kutokana na mshtuko wa moyo kama ilivyotangazwa na serikali ya nchi hiyo.