Burundi yakanusha kuhusika na tukio la Bukavu

Burundi yakanusha kuhusika na tukio la Bukavu

MBOKA NA NGAI

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2025
Posts
350
Reaction score
576
Jeshi la Burundi limekanusha ripoti kwamba lilihusika na mashambulizi ya Mabomu huko Bukavu, Kivu Kusini, ambako mkutano wa AFC/M23 ulikuwa unafanyika.

Brigedia Jenerali Gaspard Baratuza, Msemaji wa Jeshi, amethibitisha kuwa hakuna Mwanajeshi wa Burundi ambaye yupo katika mji wa Bukavu.

Hilo linakuja baada ya Kiongozi wa M23, Bertrand Bisimwa, kupitia akaunti yake ya X, akisema kuwa baada ya uchunguzi, ilibainika kuwa vilipuzi vilitumiwa na jeshi la Burundi Mashariki mwa Congo.

Soma Pia: Waasi wa M23 Wateka Bukavu, Jiji la Pili kwa ukubwa Mashariki mwa DRC

Kiongozi wa M23, katika nyaraka zake, anathibitisha kwamba waandalizi wa kitendo hichi cha kigaidi, walinuia kumuua Kiongozi Corneille Naanga ambaye tayari alikuwa katika sehemu hiyo.

Watu 11 waliuawa na wengine 65 kujeruhiwa. Corneille Nangaa, anayeongoza AFC/M23, alikuwa tayari amewaambia washiriki kwamba ndani ya saa 48 wangewatambulisha Magavana wapya wa jimbo la Kivu Kusini kwenye maeneo wanayodhibiti na jiji la Bukavu.
 
Kwa jinsi yale mabomu yalivyoua watu kwenye ule mkutano sidhani kama huko Bukavu kutakuja kuwa na mkutano wa wazi tena hao M 23 wanaitamani na Burundi tena..
 
Wao MATAKO23 walijua itakuwa rahisi rahisi tu kuitawala KONGO.
 
K
Jeshi la Burundi limekanusha ripoti kwamba lilihusika na mashambulizi ya Mabomu huko Bukavu, Kivu Kusini, ambako mkutano wa AFC/M23 ulikuwa unafanyika.

Brigedia Jenerali Gaspard Baratuza, Msemaji wa Jeshi, amethibitisha kuwa hakuna Mwanajeshi wa Burundi ambaye yupo katika mji wa Bukavu.

Hilo linakuja baada ya Kiongozi wa M23, Bertrand Bisimwa, kupitia akaunti yake ya X, akisema kuwa baada ya uchunguzi, ilibainika kuwa vilipuzi vilitumiwa na jeshi la Burundi Mashariki mwa Congo.

Soma Pia: Waasi wa M23 Wateka Bukavu, Jiji la Pili kwa ukubwa Mashariki mwa DRC

Kiongozi wa M23, katika nyaraka zake, anathibitisha kwamba waandalizi wa kitendo hichi cha kigaidi, walinuia kumuua Kiongozi Corneille Naanga ambaye tayari alikuwa katika sehemu hiyo.

Watu 11 waliuawa na wengine 65 kujeruhiwa. Corneille Nangaa, anayeongoza AFC/M23, alikuwa tayari amewaambia washiriki kwamba ndani ya saa 48 wangewatambulisha Magavana wapya wa jimbo la Kivu Kusini kwenye maeneo wanayodhibiti na jiji la Bukavu.
Kuna Taarifa hapa Nyamisati kwamba waasi wa M23 wameshavurugana wao kwa wao na kwamba huyo mkoloni Nangaa hataki kuendelea na mapigano baada ya kuona vifo vinaongezeka vya watu wa kabila lake...

Ndugu AFP naomba utuwekee sawa hili...
 
Kwa jinsi yale mabomu yalivyoua watu kwenye ule mkutano sidhani kama huko Bukavu kutakuja kuwa na mkutano wa wazi tena hao M 23 wanaitamani na Burundi tena..
Waivamie Sasa waiteke ...
 
Back
Top Bottom