Business Location inasumbua watu wengi sana na wengi hufunga baada ya Kodi ya Awali kuisha

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
7,872
Reaction score
9,263
Swala la Location ya Biashara linahitaji hesabu kari sana. Watu wengi sana wanachemka mno hii sehemu.

Unakuta mtu ana wazo zuri sana ila location huja kuua lile wazo.

Wengi baada ya Kodi ya Miezi 6 au mwaka kuisha huwa wanakimbia make huja kugundua hakuna wanacho make.

Location inahitaji akili sana kwenye kuplani ni wapi hasa uweke biashara yako.

Lazima uwe na Justfication za kutosha kwenye hiyo location yako.

Biashara kama Migahawa, super Market hawa ndo wahanga wakubwa wa location.

Kuna mambo lazima uyajue kabla huja amua location.
- Aina ya watu unao watafuta.
- Vipato vyao.
- Ufikiwaji wa hiyo offisi yako, je inafikiwa kirahisi?
Hii pia huwa ni changamoto kubwa sana location labda hakuna Packing au iko sehemu yenye usalama hafifu au usalama mkari sana vyote vina madhara.

- Competitors walioko eneo hilo hapa kuna Direct na Indirect.
- Gharama ya kodi.
- Aina ya Product au Service na upatikanaji wake.Je service au product yako ni uniq sana?
- Muda/Wakati wa kuwa na wateja wengi
Kuna baadhi ya biashara hupata wateja jioni pekee, zingine Mchana pekee, zingine ni asubuhi pekee, zingine ni Weekend pekee na zingine ni Usiku pekee na zingine ni muda wote na wakati wote.
 
Wale wazee wa ki ingilishi wanasemaga hivi "Failure to plan, you're planning to fail" mwisho wa kunukuu.
 
hii ni changamoto kubwa hasa kwa wafanyabiashara wa chini kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…