Business partinership in used car tires

Business partinership in used car tires

Yamwana

Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
36
Reaction score
6
Kheri ya mwaka mpya kwa wana biashara wote.

Nimepata deal la second hand car tires kutoka moja ya wadau wangu wa muda mrefu. Mdau huyu anasema ana uwezo wa ku-supply haya magurudumu kwa kiasi cha contena ya futi 20 au 40 kila baada ya muda mfupi kulingana na mahitaji ya soko. Magurudumu haya yatakuwa yanatoka katika nchi za Ulaya, zaidi Ujerumani, ubora wake nimeambiwa ni wa kuridhisha kwa kiwango cha second hand. Pia nimefahamishwa kuwa kuwa, magurudumu haya yako katika kiwango ambacho hata huko yatokako bado ni bora kwa matumizi.

Hivyo basi, ninachokitafuta hapa jukwaani ni wadau ambao wanahitaji supply ya kutosha na ya kuaminika ya used car tires. Supplier yuko tayari kufunga mzigo wa idadi ya contena na kuufikisha Tanzania/Dsm kwa gharama zake mwenyewe. Anachohitaji ni mteja au wateja wa jumla ambao watachukua mzigo wote at one go/mkupuo. Kutokana na umbali wa alipo supplier, uchuuzi/retailing haifai.

Kwa wale wote ambao wataguswa na hii kitu, tafadhari wasisite kuwasiliana nami hapa jamvini openly au kwa hata kwa PMs. Maswali na mapendekezo juu ya hii biashara yanakaribishwa kwa mikono miwili.

Pia kama kuna mtu ana uzoefu na hii biashara au ni mwepesi wa kuchangamkia fursa, basi asisite kuwasiliana nami. Nitabandika tangazo la uwakala kule kwene jukwaa la kazi. Kwa ufupi majukumu yatakuwa ni kutafuta wateja wa kuaminika wanaohitaji mzigo, pia kutafuta taarifa zaidi juu ya masoko mapya pamoja na bei. Uwezo wa ku-supply nje ya soko la Tanzania upo, endapo masoko hayo yatakuwa na tija. Hivyo basi mtu mwenywe uwezo wa aina hiyo kama yumo humu ndani anakaribishwa pia.

Ahsanteni nyote.
 
Niliwahi kusikia kuwa second hand tyres haziruhusiwi kuingizwa Tanzania. Ngoja wajuvi waje watujuze zaidi.
 
Kheri ya mwaka mpya kwa wana biashara wote.

Nimepata deal la second hand car tires kutoka moja ya wadau wangu wa muda mrefu. Mdau huyu anasema ana uwezo wa ku-supply haya magurudumu kwa kiasi cha contena ya futi 20 au 40 kila baada ya muda mfupi kulingana na mahitaji ya soko. Magurudumu haya yatakuwa yanatoka katika nchi za Ulaya, zaidi Ujerumani, ubora wake nimeambiwa ni wa kuridhisha kwa kiwango cha second hand. Pia nimefahamishwa kuwa kuwa, magurudumu haya yako katika kiwango ambacho hata huko yatokako bado ni bora kwa matumizi.

Hivyo basi, ninachokitafuta hapa jukwaani ni wadau ambao wanahitaji supply ya kutosha na ya kuaminika ya used car tires. Supplier yuko tayari kufunga mzigo wa idadi ya contena na kuufikisha Tanzania/Dsm kwa gharama zake mwenyewe. Anachohitaji ni mteja au wateja wa jumla ambao watachukua mzigo wote at one go/mkupuo. Kutokana na umbali wa alipo supplier, uchuuzi/retailing haifai.

Kwa wale wote ambao wataguswa na hii kitu, tafadhari wasisite kuwasiliana nami hapa jamvini openly au kwa hata kwa PMs. Maswali na mapendekezo juu ya hii biashara yanakaribishwa kwa mikono miwili.

Pia kama kuna mtu ana uzoefu na hii biashara au ni mwepesi wa kuchangamkia fursa, basi asisite kuwasiliana nami. Nitabandika tangazo la uwakala kule kwene jukwaa la kazi. Kwa ufupi majukumu yatakuwa ni kutafuta wateja wa kuaminika wanaohitaji mzigo, pia kutafuta taarifa zaidi juu ya masoko mapya pamoja na bei. Uwezo wa ku-supply nje ya soko la Tanzania upo, endapo masoko hayo yatakuwa na tija. Hivyo basi mtu mwenywe uwezo wa aina hiyo kama yumo humu ndani anakaribishwa pia.

Ahsanteni nyote.

used tyres haziruhusiwi tanzania bara....nu-pm nikwambie zinafikaje tz
 
Back
Top Bottom