BUTIKU: Ndani ya Nchi yetu wapo watu wanapenda siasa ya kihuni

BUTIKU: Ndani ya Nchi yetu wapo watu wanapenda siasa ya kihuni

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku amesema siku hizi siasa zitaka kugeuzwa kama mchezo wa kihuni huku akidai kuwa nchini kuna Watu wanaopenda siasa za kihuni.

IMG-20240910-WA0007.jpg

Akizungumza September 10, 2024 amesema kuwa jamii haitakiwi kuunga mkono wanaohitaji uongozi kwa kutumia njia za 'kihuni' ikiwemo kutekeleza mauaji au kutoa rushwa.

"Taifa letu halijafundishwa siasa za kihuni hata siku moja, tulipata kiongozi Baba wa Taifa (Mwl. Nyerere) alitulea vizuri hakuwa muhuni na kama tunamuita Baba wa Taifa basi sisi Watoto wake hatutarajii kuwa wahuni wa kuua Watu."anasema Butiku

Ameongeza"Kwahiyo siasa siku hizi inaanza kugeuzwa kana kwamba ni mchezo wa wahuni, SIVYO . Napenda Watanzania wasikubali kwamba wana siasa ya kihuni HAPANA"

Aidha anadai "Ndani ya Nchi yetu wapo watu wanaopenda siasa ya kihuni, lakini mfumo wetu ni wa siasa ya kiungwana."

"Hutafuti cheo kwa kuua wenzako ukifanya hivyo wewe ni muhuni, lakini zaidi hutafuti cheo kwa kuhonga, kununua haki ya wapiga kura na vilevile wewe raia husitake hela za wanaotafuta vyeo, raia wetu nao wanapokea hela pamoja na baadhi ya maaskari."

Amesisitiza kwamba unahitajika uwajibikaji kwa kuheshimu Watu ikiwemo kulinda maisha yao na mali zao, lakini amesema kuwa kwa sasa Watu wameanza kuingiwa na uoga, amedai kuwa wapo wanaojua ukweli wa mambo mbalimbali lakini hawasemi kwa kuhofia kutendewa visivyo.

"Katika kuwajibika inahitaji ujasiri wa moyo unaotoka na imani , kwamba watu ni watu wanastahili kuheshimiwa na maisha yao yanastahili kulindwa na mali zao, katika hilo hakuna uoga Taifa hili limeanza kuwa na Watu waoga.

Anaongeza" Mjue Demokrasia hupewi kwenye sahani inatakiwa huipiganie. Tanzania tumejengewa msingi mzuri sana tukibabaika na uoga na unafiki hatuwezi kufika." Amesema Butiku

Pia, soma: Joseph Butiku: Vyombo vya ulinzi na usalama visijifanye havijui mambo yanayoendelea nchini
 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku amesema siku hizi siasa zitaka kugeuzwa kama mchezo wa kihuni huku akidai kuwa nchini kuna Watu wanaopenda siasa za kihuni...
"Utafuti cheo kwa kuua wenzako ukifanya hivyo wewe ni muhuni, lakini zaidi hutafuti cheo kwa kuhonga, kununua haki ya wapiga kura na vilevile wewe raia husitake hela za wanaotafuta vyeo'... asante sana mzee butiku

wenye uchaguzi wao chamani, wamalize sehemu muhimu ya uchaguzi iliyobaki kwa salama na amani jamani dah... :pulpTRAVOLTA:
 
Sasa kila uchaguzi ukifanyika kwa kuua Watu,watawaongoza kina nani? Maana utakuwa umemaliza watu!
 
"Utafuti cheo kwa kuua wenzako ukifanya hivyo wewe ni muhuni, lakini zaidi hutafuti cheo kwa kuhonga, kununua haki ya wapiga kura na vilevile wewe raia husitake hela za wanaotafuta vyeo'... asante sana mzee butiku

wenye uchaguzi wao chamani, wamalize sehemu muhimu ya uchaguzi iliyobaki kwa salama na amani jamani dah... :pulpTRAVOLTA:
Acha kujifanya unahamisha magoli.Mambo yamewashinda sasa mnaleta unafiki wenu kwenye maisha ya watu.
 
"Utafuti cheo kwa kuua wenzako ukifanya hivyo wewe ni muhuni, lakini zaidi hutafuti cheo kwa kuhonga, kununua haki ya wapiga kura na vilevile wewe raia husitake hela za wanaotafuta vyeo'... asante sana mzee butiku

wenye uchaguzi wao chamani, wamalize sehemu muhimu ya uchaguzi iliyobaki kwa salama na amani jamani dah... :pulpTRAVOLTA:
CCM ya zamani ilikuwa ya wakulima na wafanyakazi, ilitegemea nguvu ya ushawishi. Hii CCM ya sasa ambayo watu wanatafuta madaraka kwa kuua wapinzani wao na kwa njia ya kuhonga, ni CCM ya kishetani. Wote wenye Roho wa Mungu wanatakiwa kujiweka mbali na hii CCM ya sasa, CCM ya kishetani.

"CCM hawaachiani glass ya maji mezani" - Jakaya Kikwete.

"Ndani ya CCM kuna majizi" - Magufuli

"WanaCCM wenzangu, tukilitegemea Jeshi la Polisi, tutapotea" - Jakaya Kikwete.

"CCM ya sasa, inayoamini kwenye uchaguzi wa hela, CCM inayoongelea udini na ukabila, siyo CCM tuliyoianzisha. CCM si baba yangu wala mama yangu" - Mwalimu Nyerere.

"Nchi inahitaji vijana jeuri, vijana wanaoweza kuhoji vitendo vya watawala. Siyo vijana wa , NDIYO MZEE" - Mwalimu Nyerere.
 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku amesema siku hizi siasa zitaka kugeuzwa kama mchezo wa kihuni huku akidai kuwa nchini kuna Watu wanaopenda siasa za kihuni.


Akizungumza September 10, 2024 amesema kuwa jamii haitakiwi kuunga mkono wanaohitaji uongozi kwa kutumia njia za 'kihuni' ikiwemo kutekeleza mauaji au kutoa rushwa.

"Taifa letu halijafundishwa siasa za kihuni hata siku moja, tulipata kiongozi Baba wa Taifa (Mwl. Nyerere) alitulea vizuri hakuwa muhuni na kama tunamuita Baba wa Taifa basi sisi Watoto wake hatutarajii kuwa wahuni wa kuua Watu."anasema Butiku

Ameongeza"Kwahiyo siasa siku hizi inaanza kugeuzwa kana kwamba ni mchezo wa wahuni, SIVYO . Napenda Watanzania wasikubali kwamba wana siasa ya kihuni HAPANA"

Aidha anadai "Ndani ya Nchi yetu wapo watu wanaopenda siasa ya kihuni, lakini mfumo wetu ni wa siasa ya kiungwana."

"Hutafuti cheo kwa kuua wenzako ukifanya hivyo wewe ni muhuni, lakini zaidi hutafuti cheo kwa kuhonga, kununua haki ya wapiga kura na vilevile wewe raia husitake hela za wanaotafuta vyeo, raia wetu nao wanapokea hela pamoja na baadhi ya maaskari."

Amesisitiza kwamba unahitajika uwajibikaji kwa kuheshimu Watu ikiwemo kulinda maisha yao na mali zao, lakini amesema kuwa kwa sasa Watu wameanza kuingiwa na uoga, amedai kuwa wapo wanaojua ukweli wa mambo mbalimbali lakini hawasemi kwa kuhofia kutendewa visivyo.

"Katika kuwajibika inahitaji ujasiri wa moyo unaotoka na imani , kwamba watu ni watu wanastahili kuheshimiwa na maisha yao yanastahili kulindwa na mali zao, katika hilo hakuna uoga Taifa hili limeanza kuwa na Watu waoga.

Anaongeza" Mjue Demokrasia hupewi kwenye sahani inatakiwa huipiganie. Tanzania tumejengewa msingi mzuri sana tukibabaika na uoga na unafiki hatuwezi kufika." Amesema Butiku

Pia, soma: Joseph Butiku: Vyombo vya ulinzi na usalama visijifanye havijui mambo yanayoendelea nchini
Kwa hiyo anaogopa kuwataja CCM kuwa wanapenda siasa za kihuni? Hivi kuna wahuni wa siasa nchi hii zaidi ya CCM? Huyu mzee anatuchosha tu.
 
CCM ya zamani ilikuwa ya wakulima na wafanyakazi, ilitegemea nguvu ya ushawishi. Hii CCM ya sasa ambayo watu wanatafuta madaraka kwa kuua wapinzani wao na kwa njia ya kuhonga, ni CCM ya kishetani. Wote wenye Roho wa Mungu wanatakiwa kujiweka mbali na hii CCM ya sasa, CCM ya kishetani.

"CCM hawaachiani glass ya maji mezani" - Jakaya Kikwete.

"Ndani ya CCM kuna majizi" - Magufuli

"WanaCCM wenzangu, tukilitegemea Jeshi la Polisi, tutapotea" - Jakaya Kikwete.

"CCM ya sasa, inayoamini kwenye uchaguzi wa hela, CCM inayoongelea udini na ukabila, siyo CCM tuliyoianzisha. CCM si baba yangu wala mama yangu" - Mwalimu Nyerere.

"Nchi inahitaji vijana jeuri, vijana wanaoweza kuhoji vitendo vya watawala. Siyo vijana wa , NDIYO MZEE" - Mwalimu Nyerere.
infact,
CCM ni ya wakulima na wafanyakazi na kwakweli huko ndimo wamejazana watu hao wengi sana . By the way even me ni mkulima lakini pia ni mfugaji licha ya kua na majukumu mengine muhimu na mazito sana...

vyama vingine vya kisiasa, mathalani chadema misingi yake ni tofauti kidogo na ndio maana wengi hupata tabu kuelewa dhamira yake hasa ni nini kwa mfano ni taasisi ya kiraia au asasi binafsi ya kijamii? ni chama cha kisiasa na ni siasa gani? au ni kitega uchumi cha mtu au chamber of commerce flani hivi hapo mjini?
hili limewachanganya wengi sana....

na majuzi Makamu mwenyekiti wa Chadema Taifa alisikika akisema chadema si dini wala mamake anaweza kuondoka any time..

hiyo sio issue,
vyama vyote vya kisiasa nchini vimefanya chaguzi zao kwa salama na amani, why ilipoanza chadema tu matukio haya ya kishenz yakaanza?

na kwanini yanaongezeka na kua mabaya zaid chadema inapoelekea uchaguzi wa ngazi ya juu?

ni muhimu sana kujiridhisha,
Taarifa za utekaji zinatoka HQ chadema at the same time za mauaji ya mateka zinatoka HQ chadema...

ni kweli watoa taarifa hawa hawana taarifa za hapo katikati kwamba mateka alitendewa nini?

why mwanzo na mwisho tu?

we need special investigations ili tuelewe huu ni muujiza au mipango 🐒
 
Back
Top Bottom