Buzz ni bomba.. enzi hizo

SI unit

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
1,953
Reaction score
767
Enzi zile nilikua nafanya mchezo wa kubahatisha namba, nikikutana na sauti ya kiume napotezea, nikikutana na ya kike nachombeza. Sasa kuna huyo dada anaitwa ***, ana sauti laiiini kwenye simu. Daah! Tukaanza ku"flirt", tukakubaliana kuonana. Unajua nini kilinitokea?
...
Hata wewe au rafiki yako keshapitia huko.
...
Enzi hizo buzz ni bomba bana, mishale ya saa sita nait kali mpaka majogoo watu wanaongea "*****" kwenye vilongalonga vyao, mostly SIEMENS dole gumba, TWANGA pepeta na NOKIA jeneza n.k.!
...
This is chit chat
 
Dah nakumbuka enzi zileeeeee
Hivi Mobitel na Buzz ilianzaga ipi?
Hope Mobitel...huko ndo kwenyewe
 
sikua nayo kwakweli...simu alikua nayo baba tu!
 
Dah nakumbuka enzi zileeeeee
Hivi Mobitel na Buzz ilianzaga ipi?
Hope Mobitel...huko ndo kwenyewe
.
Kitu cho mobitel ndio kilianza, kuna kitu ingine ilikua inaitwa tritel..
 

Umenikumbusha Erickson yangu, kama mche wa sabuni. Kuna kipindi flan ilikuwa ikiita kwenye gari hata kupokea aibu, lakin enzi hizo unaonekana mtoto wa mjinii.
Yaani teknolojia inabadilika kwa kasi sana, leo hii watoto wadogowadogo wako na samsung tablet, smartphones, .... Mmmh
 
.
Enzi hizo sim card ilikua inauzwa up to Tsh 15,000. Vocha --> dola
 
Nakumbuka kipindi hicho nilikuwa naenda kulala kwa rafiki yangu kujisomea kwa ajili ya mtihani. Mama yake rafiki alikuwa anatumia Buzz, usiku anaicha kwenye chaji. Basi tunatuma meseji mpaka tunachoka,tatizo tulikuwa hatujui kufuta Sent message. Kuna siku yule mama alituuliza hivi nyinyi watoto huwa mnasoma kweli? Tukamuuliza kwanini mnasema hivyo mama? Akajibu mnatuma meseji zaidi ya mia wakati wa usiku,je mnasoma saa ngapi? Hapo ndio tukajua kumbe mama anajua, ukizingatia kuwa meseji nyingi zilikuwa za ushenzi tulipata aibu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…