koncho77
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 7,789
- 10,388
RAFIKI: Vipi mbona leo huna
uchangamfu.
JAMAA: Wanawake bwana,
mwanamke hata umpendeje
atakugeuka tu.
RAFIKI: Nini tena ndugu yangu? Mbona shemeji mtu
fresh sana.
JAMAA: Hata mimi nilikuwa
najua hivyo, leo nimegundua
kumbe ana siri kubwa sana
ananificha, mimi naita huu ni usaliti wa ndoa.
RAFIKI: Nini tena?
JAMAA:Nimegundua mke
wangu kumbe anafanya
biashara ya kitimoto na
hajawahi hata kuniambia.
RAFIKI: Kitimoto? We
umejuaje?
JAMAA: Leo asubuhi
nilichelewa kuamka niliamua
nijipumzishe kidogo kabla ya
kwenda kazini, simu ya mke
wangu ikalia, nikaamua
kuipokea, kabla hata sijafungua mdomo, nikasikia sauti ya
mwanaume mmoja akauliza,
“Huyo nguruwe
umeshamuondoa?’ Hebu wewe
fikiria nilivyoshtuka, yaani
mpaka sasa nashindwa kuamini kuwa mke wangu ananizunguka
anafanya biashara ya nguruwe
hajaniambia hata siku moja.
uchangamfu.
JAMAA: Wanawake bwana,
mwanamke hata umpendeje
atakugeuka tu.
RAFIKI: Nini tena ndugu yangu? Mbona shemeji mtu
fresh sana.
JAMAA: Hata mimi nilikuwa
najua hivyo, leo nimegundua
kumbe ana siri kubwa sana
ananificha, mimi naita huu ni usaliti wa ndoa.
RAFIKI: Nini tena?
JAMAA:Nimegundua mke
wangu kumbe anafanya
biashara ya kitimoto na
hajawahi hata kuniambia.
RAFIKI: Kitimoto? We
umejuaje?
JAMAA: Leo asubuhi
nilichelewa kuamka niliamua
nijipumzishe kidogo kabla ya
kwenda kazini, simu ya mke
wangu ikalia, nikaamua
kuipokea, kabla hata sijafungua mdomo, nikasikia sauti ya
mwanaume mmoja akauliza,
“Huyo nguruwe
umeshamuondoa?’ Hebu wewe
fikiria nilivyoshtuka, yaani
mpaka sasa nashindwa kuamini kuwa mke wangu ananizunguka
anafanya biashara ya nguruwe
hajaniambia hata siku moja.