Bye bye DSTV!

Bye bye DSTV!

Ibrah

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2007
Posts
2,730
Reaction score
530
Mlitutesa sana
Mlituumiza sana
Mlitutenga sana
Bye-bye DStv!

Mliringa sana
Mkaongeza matabaka
Ya walala hai
Na walala hoi
Bye-bye DStv

Bei yenu ilikuwa ghali
Kwa watu wa ghali
Mara dola sabini
Mara dola sitini
Bye-bye DStv


Leo nimekutana na tangazo la DStv katika kituo cha daladala hapa Arusha, sikuamini macho yangu. Ilibidi nisogee karibu na kuanza kulisoma kwa makini. NAdhani baadhi ya watu walinishangaa. Tangazo hilo lilinifanya nije na utenzi huo Byebye DStv!

Ati DStv sasa wamekuja na punguzo kwa wateja wao! Unapata channeli zisizopungua 25 kwa malipo ya shilingi 13,500/- kwa mwezi (vi9gezo na masharti yao kuzingatiwa!) Chaneli nyingi kati ya hizo 25 zinapatikana katika king'amuzi cha TBC; kuna TBN, TBC, Citizen, Trace, BeT nk. Chaneli za nyongeza ni ESPN, KBC, Gospel na Muslim.

Ilinikumbusha miaka ya ukiritimba na wizi waliotufanyia DStv kabla ya TBC kuja na ving'amuzi vya kichina-china. Walijipangia bei za ajabu-USD 60-70! Leo DStv wenyewe wamekubali yaishe. NAdhani watabaki wakiringia Super sports pekee ambayo ndo itawafanya wale wa madaraja ya juu kutupiga bao hapo lakini ikiwa TBC watalipia mechi zaidi za Premier League mwezi August ni wazi ngoma itakuwa droo.

Kwetu sisi wengineo ambao tuliwachukia DStv kwa ukiritimba na ubaguzi wao wa bei zao za kuruka, lau tumepata mahali pa nafuu kidogo.

NAkumbuka miaka ile ya kati ya 1990, DTV walikwa wakituonyesha mechi nyingi tu za Premier League kabla ya kuja hao DStv na kudai wao ndo wenye haki pekee ya kurusha mechi hizo Tanzania.

Hongera TBC,angalau kukomesha urasimu na majivuno ya DStv.
 
TBC2 bado hawajaeneza huduma nchini kote, kwa hiyo bado maumivu yapo kwa ambao hawaishi Dar, Dodoma, Mwanza na Arusha!
 
Still bado ntaendelea na DSTV,kama mdau wa michezo sijaona chanel ya maana kwenye hivyo vingamuzi vya Wachina
 
TBC kaza buti(hata kama Business partner wako ni mchina)... endeleza ushindani..Mwanzo daima mgumu!!! Binafsi naona ni bora nilipe huduma ya king'amuzi kwa huduma za TBC (nichangie maendeleo ya habari TZ) kuliko kwa hawa wageni ...DSTV watasalimu amri kwani nao wananunua haki za kutangaza vipindi vyao kama wengine..!!
 
TBC2 bado hawajaeneza huduma nchini kote, kwa hiyo bado maumivu yapo kwa ambao hawaishi Dar, Dodoma, Mwanza na Arusha!

Ni kweli itachukua muda lakini ikiwa kama TBC wataendelea na kasi hii, naamini ifikapo mwakani nchi nzima yaweza kuwa imefikiwa.
Still bado ntaendelea na DSTV,kama mdau wa michezo sijaona chanel ya maana kwenye hivyo vingamuzi vya Wachina


Hata wao DStv mamejua hilo ndo maana katika hizo channels 25 Supersports hazimo, lakini ikiwa TBC watang'amua hizo channels za michezo, DStv watasalimu amri. Ni suala la wakati tu hata ninyi loyal customers mtawakimbia.
 
Ingawa DSTV wana bei za juu, ukweli upo pale pale events kubwa za michezo duniani, narudia events kubwa za michezo duniani unazipata sehemu moja kutoka kwao.

Wale wapenzi wa Formula One, Athletics (IAAF Diamond League), Tour de France, Golf Majors, SBK, MotoGP, NBA, Tennis Majors + Ligi zote kubwa za soka duniani wataelewa nini nasema. Hii ni bila kusahau CNN, BBC, Sky, Euro News kwa upande wa habari.

Ni vigumu kupata-(kwa Afrika) Cable subscriber wa kukupa Sports events kama hizi kwa pamoja.

Kitu bora siku zote ni ghali.
 
dstv ni mwisho wa matatizo!
HAILINGANISHWI KABISA
 
Daah, Ibrah aliingia kwa kishindo kuiponda DSTV, naona wengi wamemkata maini kwa kuwa against na mtazamo wake. Hapa bila channel inayofanya coverage ya sports kwa wingi, sidhani kama watu watakuelewa, ukizingatia maisha yenyewe magumu na mahali pa kujifariji ni kwenye sports !
 
TBC2 bado hawajaeneza huduma nchini kote, kwa hiyo bado maumivu yapo kwa ambao hawaishi Dar, Dodoma, Mwanza na Arusha!

Hata huko ambako TBC2 haiko, DSTV haiko pia au ni watu wachache sana wenye uwezo wa kulipia hayo ma-DSTV
 
Daah, Ibrah aliingia kwa kishindo kuiponda DSTV, naona wengi wamemkata maini kwa kuwa against na mtazamo wake. Hapa bila channel inayofanya coverage ya sports kwa wingi, sidhani kama watu watakuelewa, ukizingatia maisha yenyewe magumu na mahali pa kujifariji ni kwenye sports !

Mkuu, inategemea nini hasa unachokihitaji. SIku nyingi sana nimekuwa siwapendi hawa DStv kwa kuwa ghrama zao ni juu mno. Naamini kabisa TBC wataweza kutupatia Sports channels kwa bei nafuu kuliko DStv, si unakumbuka GTv? Mbona waliweza kutupatia channels nyingi tu za michezo kwa gharama nafuu kuliko DStv?

Mimi kwa sasa angalau natosheka na thamani ninayolipia king'amuzi cha TBC. Premier League inaanza mwezi ujao naamini tutaona mechi nyingi zaidi za Premier League kuliko mwaka jana maana uwezo wa kifedha wa TBC kununua haki za kupokea na kurusha mechi za Premier utakuwa umeongezeka.
 
Ibrah, channel pekee zilizokuwa zinauza GTV decoders ni zile za English Premier League, lakini zaidi ya hapo hawakuwa na michezo mingine kama ilivyo DSTV na ndiyo maana walionekana nafuu. Ni kwa sababu wao waliangalia tu EPL, with time kama wangetafuta rights za michezo mingine kama DSTV wasingecheza mbali katika subscription fee.

Ndiyo maana nasema Kitu Bora ni Ghali.
 
haaaaaaaaaaaaaa bravoooooooooooo chanel ten,itv na tv tumaini ni ivyo ndo ninavyoweza ku acces
ma dstv sjui manini sjui :fish2: ya kichna tbc ni kitendawili kwangu!!!!!!!!!!!

aya nyie maclassic jadilini mambo yenu mi simo kwenye class i
hongereni
 
Ukweli ni kuwa ni vigumu sana ku-access michezo yote na haiwezekani kushuhudia michezo yote at a time. Tukipata hiyo EPL inatutosha kabisa, so TBC wakipata haki ya EPL kwa mechi zote utashuhudia anguko kubwa sana la wateja kwa upande wa DStv na ndo maana wamefikia hatua ya kuchaji Tsh. 13,500/- , siku TBC wakipata haki ya EPL hao DStv watafika hata kuchaji kama TBC- ni suala la muda tu!
 
Lakini bado DSTV wanacoverage kubwa inapokuja suala la michezo! Kwa sisi wapenzi wa ligi ya Italia bado TBC haijatusaidia sana, labda kwenu mnaopendelea ligi ya kwa malkia!
 
Mkuu Ibrah:

Bila TBC(1 or 2) kuwa na "Sports Channels" bado DSTv wataendelea "kula vichwa": Kwa ujumla "audience" ipo interested na:

1. Sports
2. Drama/Movies
3. Others

DSTv bado wanaongoza kwa item(s) 1 and 2.
 
Mimi nalipia DsTV kwa sababu kubwa moja: EPL, kama TBC au mwingine atapata rights za kurusha angalau 90% ya michezo ya EPL nitahama DsTV. Tatizo ni kwamba hawadumu, walikuja GTV tukanunua ving'amuzi wakatutoroka bila hata kuaga lakini DsTV, mwe kila siku wapo ili mradi umelipia.
Kila kizuri kina gharama
 
Ukweli ni kuwa ni vigumu sana ku-access michezo yote na haiwezekani kushuhudia michezo yote at a time. Tukipata hiyo EPL inatutosha kabisa, so TBC wakipata haki ya EPL kwa mechi zote utashuhudia anguko kubwa sana la wateja kwa upande wa DStv na ndo maana wamefikia hatua ya kuchaji Tsh. 13,500/- , siku TBC wakipata haki ya EPL hao DStv watafika hata kuchaji kama TBC- ni suala la muda tu!
Ibrah ninachofahamu ni kuwa tangu siku nyingi DSTV walikuwa na package za aina 3,but premium ndio ina chanel nyingi na bei yake ni kubwa.TBC walianza kwa mbembwe wakasema wanaonesha La Liga at the end wakaonyesha mechi hata 20 hazifiki,wakaja tena wataonyesha Premier league wakaishia kuonyesha game za Sunderland VS Newcastle,Hull VS Blackburn.
GTV walitoza bei ndogo lakini wako wapi sasa
 
Mkuu Ibrah:

Bila TBC(1 or 2) kuwa na "Sports Channels" bado DSTv wataendelea "kula vichwa": Kwa ujumla "audience" ipo interested na:

1. Sports
2. Drama/Movies
3. Others

DSTv bado wanaongoza kwa item(s) 1 and 2.

Naungana na wewe baba enock,mbali na ughali wao,hawa jamaa is the best!!

 
Back
Top Bottom