CAF Confederation Cup: Namungo kumenyana na Primeiro de Agosto

CAF Confederation Cup: Namungo kumenyana na Primeiro de Agosto

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
IMG_20210108_191623_592.jpg

Namungo FC watakutana uso kwa uso na Primeiro de Agosto ya Angola katika hatua ya mtoano ya mashindano ya Kombe la shirikisho barani Afrika.

Timu hiyo ya Ligi Kuu ya Tanzania ambayo inacheza mara ya kwanza katika hatua hii, itacheza ugenini kabla ya mechi ya nyumbani ambapo mchezo wa kwanza utachezwa Februari 12 na wa pili Februari 21.

Mshindi wa matokeo ya ujumla kwa Nyumbani na Ugenini atafuzu hatua ya Makundi ya mashindano hayo.

Namungo, chini ya kocha mpya Hemed Morocco ilipata nafasi katika hatua ya mchujo baada ya ushindi wa jumla ya 5-3 dhidi ya El-Hilal Obayed ya Sudan.

Stephen Kwame Sey, alifunga katika mchezo wa kwanza ambao walishinda 2-0, Blaise Bigirimana na Edward Charles Manyama walifunga mabao matatu muhimu kwa Namungo katika mchezo wa mkondo wa pili uliomalizika kwa sare ya 3-3.

Kwa upande mwingine, Primeiro de Agosto, aliangukia Kombe la Shirikisho baada ya kufungwa na Kaizer Chiefs 1-0 katika mchezo wa mkondo wa pili.
 
Namungo wakitulia wanaweza fanya maajabu, na bahati nzuri wanaanzia ugenini halafu waje kumalizia kazi nyumbani.
 
Petro de angola ni bora kabisa katika misimu hii minne ya caf Sasa ni namna gani watachanga karata zao Ndio itaamua. Ila naona wazi namungo akifungasha vilago
 
Watanzania kwa ujumla wetu tunaitakia Namungo Fc kila la heri.
 
Petro de angola ni bora kabisa katika misimu hii minne ya caf Sasa ni namna gani watachanga karata zao Ndio itaamua. Ila naona wazi namungo akifungasha vilago
Timu iliyotajwa ni Primeiro de Agosto yaani timu inaitwa "Tarehe 1 mwezi wa Nane" na siyo Petro wa Angola.
 

Namungo FC watakutana uso kwa uso na Primeiro de Agosto ya Angola katika hatua ya mtoano ya mashindano ya Kombe la shirikisho barani Afrika.

Timu hiyo ya Ligi Kuu ya Tanzania ambayo inacheza mara ya kwanza katika hatua hii, itacheza ugenini kabla ya mechi ya nyumbani ambapo mchezo wa kwanza utachezwa Februari 12 na wa pili Februari 21.

Mshindi wa matokeo ya ujumla kwa Nyumbani na Ugenini atafuzu hatua ya Makundi ya mashindano hayo.

Namungo, chini ya kocha mpya Hemed Morocco ilipata nafasi katika hatua ya mchujo baada ya ushindi wa jumla ya 5-3 dhidi ya El-Hilal Obayed ya Sudan.

Stephen Kwame Sey, alifunga katika mchezo wa kwanza ambao walishinda 2-0, Blaise Bigirimana na Edward Charles Manyama walifunga mabao matatu muhimu kwa Namungo katika mchezo wa mkondo wa pili uliomalizika kwa sare ya 3-3.

Kwa upande mwingine, Primeiro de Agosto, aliangukia Kombe la Shirikisho baada ya kufungwa na Kaizer Chiefs 1-0 katika mchezo wa mkondo wa pili.
Namungo anaingia makundi kwa mara ya kwanza kabisa.De Agosto ni timu nzuri sana ila Namungo wamebebwa na Caf kuanzia ugenini na hapa nyumbani Namungo atashinda kwa kishindo kabisa.
 
Write your reply...namungo yuleeeee anafanya kitu ambacho yanga hawawezi fanya na hii timu yao ya sasa ivi....
 
Kama like lijamaa ambalo likifunga linacomekea jezi na kuwakera mashabiki litacheza basi namungo watafika mbali
 
Back
Top Bottom