CAF yaruhusu mashabiki 35,000 mechi ya Simba Vs RS Berkane, Uwanja wa Mkapa

CAF yaruhusu mashabiki 35,000 mechi ya Simba Vs RS Berkane, Uwanja wa Mkapa

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Uongozi wa Klabu ya Simba umethibitisha kupokea taarifa kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuwa inayotoa nafasi ya kuingiza mashabiki 35,000 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mchezo wa Kundi D, Kombe la Shirikisho dhidi ya RS Berkane ya Morocco.

Simba itakuwa mwenyeji wa mchezo huo, Jumapili Machi 13, 2022 ikiwa na deni la kulipa kisasi cha kufungwa mabao 2-0 katika mchezo uliochezwa mjini Berkane-Morocco, Februari 27.

Meneja wa Habari na Mawasilino wa Simba, Ahmed Ally amethibitisha taarifa za kuruhusiwa kwa mashabiki 35,000, idadi ambayo ni sawa na ile ya mchezo wa mzunguko wa kwanza dhidi ya ASEC Mimosas uliomalizika kwa mnyama kuchomoza na ushindi wa mabao 3-1.

“Tulitamani kupata ruhusa ya kuwa na mashabiki wengi zaidi uwanjani wakati wa mchezo wetu dhidi ya RS Berkane, lakini taarifa ya CAF imesisitiza lazima tuwe na mashabiki 35,000.

“Tuliwaombwa CAF kuwa na mashabiki 60,000, lakini wameturuhusu kuwa na idadi hiyo 35,000 ya mashabiki, hivyo tunawahimiza mashabiki wetu kufiwa Uwanjani ili kuzitendea haki nafasi hizo tulizozipata,” amesema Ahmed Ally.
 
Uongozi wa Klabu ya Simba umethibitisha kupokea taarifa kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuwa inayotoa nafasi ya kuingiza mashabiki 35,000 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mchezo wa Kundi D, Kombe la Shirikisho dhidi ya RS Berkane ya Morocco...
Simba Nguvu Moja
 
hawa ni wakusigina goli zaidi ya tatu wakija Lupaso,huyu Ibenge sio wakutukung'uta 2 bila Moroco,amenikera sana huyu papaa.
 
Hawa Kwakweli Tucheze nao Kufa Kupona Wasitokekwa Mkapa
Wachezaji Kama Mnatembelea JF
Juma pili Nitakuwepo kwa Mkapa Naomba Mjitoe Wengine Rohozetu Mtihani
 
Nchi za waarabu mashabiki wanajaza uwanja(katazame mechi ya Berkane,al ahly na raja kwao) afu za huku kanda nyingine wanaweka limit, CAF wanatuchukuliaje???
 
Simba yenyewe sasa
274806316_3120380921564310_8510181759731295280_n.jpg
 
Nchi za waarabu mashabiki wanajaza uwanja(katazame mechi ya Berkane,al ahly na raja kwao) afu za huku kanda nyingine wanaweka limit, CAF wanatuchukuliaje???
Na raisi wa kafu giza mwenzetu sasa sijui tuite ubaguzi wa aina gani
 
Na raisi wa kafu giza mwenzetu sasa sijui tuite ubaguzi wa aina gani
Rais wa caf hana nguvu ya kutosha kufanya maamuzi kama haya ni kama kivuli tu pale, inakera sana asee
 
Rais wa caf hana nguvu ya kutosha kufanya maamuzi kama haya ni kama kivuli tu pale, inakera sana asee
Tuacheni lawama bwana Caf kwenye suala la mashabiki wala sio kwamba wanapendelea tinu za waarabu kama utakuwa na kumbukumbu msimu uliopita tu timu ya Al ahly ilicheza mechi zake zote za group stage bila mashabiki sisi tukiruhusiwa washabiki 35,000 kwa kila mechi kitu ambacho Al Ahly walilalamikia sana hasa baada ya kukutana na shughuli ya mnyama uwanja wa taifa
 
Uongozi wa Klabu ya Simba umethibitisha kupokea taarifa kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuwa inayotoa nafasi ya kuingiza mashabiki 35,000 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mchezo wa Kundi D, Kombe la Shirikisho dhidi ya RS Berkane ya Morocco.

Simba itakuwa mwenyeji wa mchezo huo, Jumapili Machi 13, 2022 ikiwa na deni la kulipa kisasi cha kufungwa mabao 2-0 katika mchezo uliochezwa mjini Berkane-Morocco, Februari 27.

Meneja wa Habari na Mawasilino wa Simba, Ahmed Ally amethibitisha taarifa za kuruhusiwa kwa mashabiki 35,000, idadi ambayo ni sawa na ile ya mchezo wa mzunguko wa kwanza dhidi ya ASEC Mimosas uliomalizika kwa mnyama kuchomoza na ushindi wa mabao 3-1.

“Tulitamani kupata ruhusa ya kuwa na mashabiki wengi zaidi uwanjani wakati wa mchezo wetu dhidi ya RS Berkane, lakini taarifa ya CAF imesisitiza lazima tuwe na mashabiki 35,000.

“Tuliwaombwa CAF kuwa na mashabiki 60,000, lakini wameturuhusu kuwa na idadi hiyo 35,000 ya mashabiki, hivyo tunawahimiza mashabiki wetu kufiwa Uwanjani ili kuzitendea haki nafasi hizo tulizozipata,” amesema Ahmed Ally.
Sijui itakuwaje bila hamasa ya Haji Manara kuvuta watu kwenda uwanjani kwa do or die zake. Na Asec Mimosas ni shabiki 20,0000 waliingia na 15000 wakanyuti
 
Back
Top Bottom