Elections 2010 Can REDET poll claims be trusted?

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
302
Kweli REDET wamebobea kwa uongo, kwa akili ndogo tu hivi kweli Daily News linaongoza kwa kusomwa sana na watu,vijijini au mijini? hapa tu inadhihirisha kuwa utafiti umefanyika maofisini hasa ofisi za serikali na hii inanifanya nitilie mashaka utafiti wao kama ni wa kweli au wa kubuni na kufurahisha watu wao.

Utafiti unatakiwa uendane na hali halisi iliyopo huwezi kusema utendaji wa serikali unaendelea vizuri wakati huohuo unasema 2/3 ya wabunge wao ambao ndio wanaunda serikali wameonekana hawatarudi maana yake hawafai, I believe in research but I dont trust every research.
 

Mkuu nakuunga mkona kwa hii hoja, February nilikuwa bongo basi kila ukikutana na mtu anauza magazeti ukimwita anaanza kukupa kiu, ijumaa, uwazi and the likes, ukimwambia huwa husomi hayo magazeti anaanza kukpa Dimba, Spoti,Simba and the likes. Unamuuliza o.k nitajie magazeti uliyonayo Utatjiwa mwananchi, daima, majira ,nipashe etc.

Unamuuliza vipi haya mengine (Citizen, Daily News, East African, The Express etc.) huuzi?????????? Hapo ndio anashtuka na kuanza kuyanadi pia hayo. This was in one of the porsche areas in Dar. I experienced this about four times. Well inawezekana kabisa hiki si kipimo cha, ni gazeti gani linasomwa sana lakini inareflect jamii yetu iko vp na inapendelea nn ifikapo wakat wa kununua na kusoma magazeti............. Sasa kuniambia eti Daily news inasomwa sana ni topic ambayo siielewi nahitaji kujuzwa!!!!!
 
ndugu jamaa na marafiki tafiti hazipigwi na maneno. zinapigwa na tafiti . najua wengi hamkutaka kusikia majibu ya tafiti yakiwa hivyo bt too bad ndo utafiti huo.70% wengine wote watapata 30% as in CHADEMA , CUF, TLP ,UDP,DP na wengine wote..........

Sasa ebu tumbie wewe mwenzetu kwa huu utafiti uliofanywa na hao hao REDET miaka ya nyuma unauelewewaje

asilimia zaidi ya 70% ya wananchi hawaridhiswi una utendaji wa mawaziri na maafisa waandamizi wa serikali ya JK

Hoja yangu hawa maafisa waandamizi waliteuliwa na JK au JK alikuwa ana uwezo wa kutengua uteuzi wao kama alifanya kwa liyumba.

Kwa hiyo ukitafakari na ukifaya detail anylysis kwenye research za REDET utagundua kuna ambiguity kama sio contradiction kwenye tafiti zao.

utata unakuja nakuja kama watu 70% wanampenda JK na watu zaidi ya 70% hawaridhishiwi na utendaji wa viongozi JK anaowateua .????? Tuelewe nini

Kwamba JK anapendwa sababu yuko presentable zaidi.?????

Na ingekuwa vizuri hizi tafiti zingeeleza hao waliohojiwa ni kwa nini wanampenda JK ni sababu z a sera za kiuchumi, kijamii, au sababu za kiamani na utulivu(CCM way)
 
Mkuu usiumize kichwa, hawa REDET wanaeleweka malengo yao ni nini

 
Wadau nimedokezwa na Mdau mmoja hapa kwamba REDET ni ya Prof. Mukandala wa UD na kabla ya JK kuwa Presidaa, Mukandala aliahidiwa ukuu wa Chuo na JK. So Prof. Mukandala analipa fadhila kwa kampeni za chini chini na takwimu mbofu mbofu.
 
hIVI HUWA WANAPITA KWA KINA NANI NA KUFANYA TAKWIMU ZAO ZA UONGO ??
 
hIVI HUWA WANAPITA KWA KINA NANI NA KUFANYA TAKWIMU ZAO ZA UONGO ??

Sina uhakika kama walifika na kufanya interviews zako Kigoma, Tarime, Musoma, Buzwagi, Busanda, Moshi, Karatu, Dar na Pemba. Research inayofanyika bila uwazi inakuwa na utata sana - anyway wacha wakipe moyo chama chao.
 
Si shehe yahaya alisema hakuna uchaguzi mwaka 2010, sasa inakuwaje REDET wanatuambia Kikwete atashinda kwa kishindo.
 
Sina uhakika kama walifika na kufanya interviews zako Kigoma, Tarime, Musoma, Buzwagi, Busanda, Moshi, Karatu, Dar na Pemba. Research inayofanyika bila uwazi inakuwa na utata sana - anyway wacha wakipe moyo chama chao.

hapo ndio kitendawili..nadhani takwimu zaidi zimefanywa katika jiji la Dar es salaam ngoja waendeleea kumpotosha prezident
 
Ni kweli Kikwete atashinda lakini sio kwa kishindo kama ilivyokuwa 2005..
 
Kama asilimia 61.7 ya wabunge wanaweza kupoteza ubunge ikizingatiwa idadi kubwa ya wabunge hivi sasa ni wa CCM iweje JK ashinde kwa kishindo ? samaki mmoja akioza wameoza wote REDET waache Ushekh Yahya hapa.
 
Wadau nimedokezwa na Mdau mmoja hapa kwamba REDET ni ya Prof. Mukandala wa UD na kabla ya JK kuwa Presidaa, Mukandala aliahidiwa ukuu wa Chuo na JK. So Prof. Mukandala analipa fadhila kwa kampeni za chini chini na takwimu mbofu mbofu.

waweza kuwa correct kabisa, siamini kama Redet ni independent researching tool, lazima kuna mkono wa mtu, yaani hizo asilimia zaidi ya 70 CCM na Kikwete watazitoa wapi
 
Jamani hebu nisaidieni kutoka asilimia 67.4 Oktoba 2009 hadi asilimia 49.3 March 2010 ni kupanda au kushuka kwa utendaji kazi wa Kikwete.
 
Ni kweli wala sio tetesi Prof. Mukandala ndio alikuwa mtafiti kiongozi wa REDET kabla ya kuwa mkuu wa chuo UD.

Mimi napata shida kidogo kuwaelewa kwanini wahoji 60% ya watanzania wa vijijini na only 40% ya waTZ wa mjini? hivi si ni wazi kuwa uelewa wa waTZ wa vijijini juu ya sisa za bongo ni mdogo kiasi kuliko wale wa mjini. Huu utafiti uko very biased kwa sababu kwa uwiano huu mbovu wa asiliamia ya watu waliohojiwa ni wazi haya ni matokeo ya kutegemea hata kabla ya utafiti wenyewe!

Lakini pia matokeo ya utafiti pia huathiriwa na jinsi unavyouliza swali, nina hakika swali hilo hilo moja unaweza pata majibu tofauti kulingana na unavyoliuliza, sasa REDET waliuliza maswali ya aina gani, na mbona hawasemi walibalance vipi jinsia maana uwiano wa jinsia pia ni muhimu sana katika tafiti kama hizi, maana ni wazi na ni kweli kabisa women perception on politics ni quite different from men perception?

Mimi nafikiri haya matokeo yanaleta maswali mengi zaidi kuliko majibu! Mukangala, JK na REDET yenu hebu jipangeni upya!
 
Opinion Poll ni opinion poll. Njia pekee ya kupinga opinion poll ni kufanya another poll. Kulalama humu hakusaidii. Redet wanafanya polls miaka yote na lawama ni hizi hizi. Utasikia watu wanalalamikia sampling wakata maisha yao hawajawahi kufanya polling. Marekani yenye watu 200m plus wana sample watu wasiozidi 2000. Uingereza hivi sasa wana uchaguzi pia sample hawazidi 2000. Mbadilike watanzania.

Mmefanya poll hapa JF ambayo sio ya kisayansi maana haina representative sample na tukajisifu kweli kweli (kujidanganya) maana ni poll ya members wanaojisikia na humu kuna members wana majina mpaka 10 na wamepiga kura. Tukubali hiyo yetu na hiyo ya redet.

Changamoto kwa vyama vya upinzani ni kwenda zaidi ya kelele za ufisadi na kuonyesha watanzania kuwa wanaweza kuongoza dola. Hilo halipo kwa sasa na imbedaki kelele tu. Mnadhani huyo Slaa na Zitto watafanya nini mbele ya machinery ya CCM?

Hivi kwa nini Watanzania hatubadiliki na kuanza kuangalia mambo kisasa na kuweka mikakati ya kuleta changes nchini?

Acheni kulalama lalama
 
Haya maoni nimeyaona kule Mwananchi:



http://www.mwananchi.co.tz/componen...-hawachaguliki-uchaguzi-2010.html#comment-499
 
Opinion poll za REDETni sawasawa na kupiga ramli sio kigezo halisi, ni copy and paste, jambo muhimu ni watu waliojiandikisha kupiga kura kwenda kupiga kura siku ya uchaguzi.

REDET anataka kutumia report yake kama swing votes kwa wale ambao hawana upande.

Kufanya Opinio poll zilitakiwa fedha nyingi za kuzunguka nchi nzima,pesa hizo alitoa nani,je kuna mkono wa wadau kwa maana wagombeaji katika uchaguzi mkuu?

Umahili,umakini wa waliofanya utafiti uko je? Quality Management System ya REDETyenyewe iko je?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…