Cc vs cylinder

Fmruma

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2013
Posts
498
Reaction score
783
Hv gari ikiwa na Cc ndogo ila piston(cylinder) nyingi mfano cc 1980 with 6 cylinder au gari ikiwa cc kubwa ila poston(cylinder)chache mfano cc 2300 with 4 cylinder je ipi itakua ina kula sana mafuta..?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hv gari ikiwa na Cc ndogo ila piston(cylinder) nyingi mfano cc 1980 with 6 cylinder au gari ikiwa cc kubwa ila poston(cylinder)chache mfano cc 2300 with 4 cylinder je ipi itakua ina kula sana mafuta..?


Sent from my iPhone using JamiiForums
mkuu ulikua unataka inayo kula supu?
 
Nnavyojua;

Cc(cubic centimetre)ni ujazo/ukubwa uliopo ndani ya cylinder kwenye nafasi inapotembea piston kutoka (TDC)top dead center kwenda (BDC) bottom dead center.

Kwahivyo basi;
Gari kula mafuta inategemea na ukubwa wa CC na sio uwingi wa cylinder.
 
Kwa teknolojia ya dunia ya sasa ni vigumu saana kutoa jibu la moja kwa moja kwenye swali lako. Maana watengenezaje wa engine wameweza kutengeneza engine za cc nyingi au cylinders nyingi zikawa very efficient kuliko za cc chache. Mfano kuna gari za cylinder 8 zina tumia mafuta karibu sawa au vizuri kuliko kina Crown wa cylinder 6 na cc chache.
 
teknolojia imekua sasa...unakuta gari mfano premio ya 2000cc d4 inakula mafuta Sawa na premio ingine ya cc 1500 ambayo sio d4 on highway..
 
Wingi wa cylinder sio tatizo kwenye ulaji wa mafuta, ila tatizo ni ujazo wa hizo cylinder.
Zamani sana kipindi nilipokuwa sielewi kuhusu mambo ya magari watu walipokuwa wakibishana kuhusu uwingi wa cylinder kuwa ni kula mafuta mengi hata mimi nilikuwa naamini hivyo. Lakini kwa sasa naelewa kuwa uwingiwa cylinder sio hoja bali hoja ni ukubwa wa hizo cylinder. Ukikuta magari mawili yenye cc sawa bali moja lina cylinder nyingi basi yote yako sawa na tena lenye cylinder nyingi linaweza kuwa na mwendo zaidi.

"ᵀʰᵉ ᶠⁱʳˢᵗ ʳᵘˡᵉ ᵒᶠ ʷᵃʳ ᵃⁿᵈ ᵇᵘˢⁱⁿᵉˢˢ ⁱˢ ᵗᵒ ᵏⁿᵒʷ ʸᵒᵘʳ ᵉⁿᵉᵐʸ"
 
V = π/4 x (D)² x H x N
Where, V = Volume, D = Bore Diameter, H = Stroke Length, N = No. of Cylinders.
Kwa hiyo ukisema cc tayari na idadi ya cylinders imekua consider kutafuta hiyo Engine capacity (cc).
 
To the best of my knowledge ni kuwa ukipewa Gari mbili zenye cc zinazolingana ie 1980 lakini zinaztofautiana idadi ya cylinder, labda Moja four cylinder nyingine six, uko salama zaidi kama utachukua yenye cylinder Sita! Kuanzia ulaji WA mafuta hadi kudumu kwa engine

Iko hivi!, stress kwenye parts za engine za four ie pistons, rods na bearing ni kubwa kuliko engine za six, means kwa kazi Aina Moja engine ya four ita struggle wakati engine ya six itafanya kwa kurelax

Cha pili ni cooling efficiency engine kubwa huwa (six) Zinachukua eneo kubwa na pia kuingia maji mengi, hii ni advantage Kwan kuchemsha ni ngumu sana

Tatu ni stability ya torque,! Firing order kwenye engine za four ipo mbali mbali, yaan Kuna interval kubwa Kati ya pogo Moja na jingine, hii hupelekea vibration flani katika engine inapo run, katika engine za six interval ni karibu karibu, na ndo sababu engine za six huweza ku idle katika Rev mdogo Sana na isitetemeke au kuzima

Stable torque ni Moja ya sababu ya engine zenye cylinder nyingi kudumu muda mrefu.

Ulaji wa mafuta naamini kwa engine zinazolingana cc, engine ya six itakula vizuri kushinda ya four, kama utafata kanuni za kuendesha engine kubwa.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
KUNA WATU WENGINE HUKU HAWATAKI KUJIFUNZA KAZI YAO NI KUHARIBU MADA ZA WATU, NA MBAYA ZAIDI UNAKUTA HANA HATA UTAALAM WOWOTE KUHUSU GARI, ANACHOJUA YEYE NI DHIHAKA TU..

WATU WENGINE ACHENI UTOTO 2019 HII, HIZI NYUZI ZA JF ZINATUSAIDIA TUNAOPENDA KUJIFUNZA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…