Kuna picha kubwa sana imeonekana,
1: CCM ya sasa haijui Siasa na figisu za Siasa, watu walikuwa wanajua CCM wanaiba lakini sio kwa Kiwango na ubabe wa aina hii, huu sasa sio wizi bali ni ujambazi, wizi wa kutumia nguvu
2: pamoja na jitihada anazojaribu kutuonyesha mtukufu Rais, bado watu hawamwelewi na hakubaliki, kwa kweli ni ajabu kabisa, pamoja na CCM na mtukufu Rais kujinasibisha kuwa wapo kwenye vita kali ya kupambana na Rushwa, Ufisadi, nk lakini kisiasa yupo chini sana sana
3: CCM imechokwa kila kona, kinachotumika sasa ni Ni nguvu ya vyombo vya usalama pamoja na watendaji wa Kiserikali (Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Tume ya Uchaguzi nk) kuwaweka CCM Madarakani.
Lakini CCM na vyombo vyake wakae wakijua hili wanalolifanya lina mwisho, na mwisho unaweza kuwa mzuri ndicho tunachokiomba, lakini pia mwisho unaweza kuwa mmbaya na wenye maafa makubwa sana,
Hao wanaoumizwa sio kama hawana ndugu zao wanajeshi, Polisi, nk itafika siku watu wanaotumainiwa na CCM kama ngai yao watagoma kwenda kuwapiga na kuwaumiza baba zao, mama zao, kaka zao, jirani zao nk.
Kwenye jeshi la Polisi ni unit ndogo sana inayopaswa kuwa na Silaha, sehemu kubwa ya jeshi ni TII SHERIA BILA SHULUTI, lakini kwa sasa jeshi lote la Polisi limekuwa sio tena jeshi la Kiraia bali ni kama special unit ya JWTZ