Elections 2010 CCM Bukoba mjini watimuana

Elections 2010 CCM Bukoba mjini watimuana

Zak Malang

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2008
Posts
5,404
Reaction score
239
Lilian Lugakingira, Bukoba

HALMASHAURI ya CCM, Wilaya ya Bukoba mjini, imewasimamisha kushiriki katika kampeni za chama hicho, viongozi watano, akiwemo mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) wa wilaya hiyo mjini, Murungi Kichwabuta.

Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Robert Bahati alitaja viongozi wengine wa chama hicho waliosimamishwa wasishiriki katika kampeni za chama hicho kwa madai ya kukihujumu chama kuwa ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa, Abdalah Kichwabuta na Pius Kaijage ambaye ni katibu wa CCM , Kata Kahororo.


Bahati aliwataja wengine waliosimamishwa kuwa ni Sylivanus Muhyoza aliyekuwa diwani wa Kata Kahororo kipindi kilichopita na Udi Miruko katibu mwenezi CCM Kata Bilele.


Alisema wanachama hao wamezuiliwa kujihushisha na kampeni za chama hicho juzi na halmashauri ya CCM wilaya ya Bukoba mjini baada ya kubainika kukihujumu chama katika kampeni zinazoendelea kwa kupinga wagombea wa CCM.


Mwenyekiti huyo wa CCM Bukoba mjini alisema kuwa pamoja na kusimamishwa wasihusike katika kampeni, wanachama hao wataendelea kuwa chini ya uangalizi wa chama hicho.


Alisema pia baadhi ya wanachama hao wamejihusisha na vitendo vya kufanya kampeni ya umeya wa Manispaa ya Bukoba kabla hata ya uchaguzi wakati meya huchaguliwa na madiwani.


Imedaiwa kuwa wanachama hao wanapita kwa wagombea udiwani ambao wanaonyesha uelekeo wa kushinda na kuwaomba wakichaguliwa wamchague tena Samwel Ruangisa ambaye alikuwa meya katika kipindi ilichopita, ili aendelee na wadhifa huo.


Hivi karibuni uongozi wa CCM Bukoba mjini, mbele ya mke wa mgombea urais wa CCM mama Salma Kikwete, uliwatuhumu Samwel Ruangisa ambaye pia anagombea udiwani katika kata Kitendaguro na Murungi Kichwabuta mwenyekiti wa UWT Bukoba mjini kuwa wanakihujumu chama na watakikosesha kura.


Chanzo: Mwananchi
 
Lilian Lugakingira, Bukoba

HALMASHAURI ya CCM, Wilaya ya Bukoba mjini, imewasimamisha kushiriki katika kampeni za chama hicho, viongozi watano, akiwemo mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) wa wilaya hiyo mjini, Murungi Kichwabuta.

Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Robert Bahati alitaja viongozi wengine wa chama hicho waliosimamishwa wasishiriki katika kampeni za chama hicho kwa madai ya kukihujumu chama kuwa ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa, Abdalah Kichwabuta na Pius Kaijage ambaye ni katibu wa CCM , Kata Kahororo.

Bahati aliwataja wengine waliosimamishwa kuwa ni Sylivanus Muhyoza aliyekuwa diwani wa Kata Kahororo kipindi kilichopita na Udi Miruko katibu mwenezi CCM Kata Bilele.

Alisema wanachama hao wamezuiliwa kujihushisha na kampeni za chama hicho juzi na halmashauri ya CCM wilaya ya Bukoba mjini baada ya kubainika kukihujumu chama katika kampeni zinazoendelea kwa kupinga wagombea wa CCM.

Mwenyekiti huyo wa CCM Bukoba mjini alisema kuwa pamoja na kusimamishwa wasihusike katika kampeni, wanachama hao wataendelea kuwa chini ya uangalizi wa chama hicho.

Alisema pia baadhi ya wanachama hao wamejihusisha na vitendo vya kufanya kampeni ya umeya wa Manispaa ya Bukoba kabla hata ya uchaguzi wakati meya huchaguliwa na madiwani.

Imedaiwa kuwa wanachama hao wanapita kwa wagombea udiwani ambao wanaonyesha uelekeo wa kushinda na kuwaomba wakichaguliwa wamchague tena Samwel Ruangisa ambaye alikuwa meya katika kipindi ilichopita, ili aendelee na wadhifa huo.

Hivi karibuni uongozi wa CCM Bukoba mjini, mbele ya mke wa mgombea urais wa CCM mama Salma Kikwete, uliwatuhumu Samwel Ruangisa ambaye pia anagombea udiwani katika kata Kitendaguro na Murungi Kichwabuta mwenyekiti wa UWT Bukoba mjini kuwa wanakihujumu chama na watakikosesha kura.

Chanzo: Mwananchi


(Utasikia) Mwananchi wachochezi.
 
hapo lwakatare tu; kwani hata wakati wa ule 'mwenge wa vijana' alisifiwa sana.
 
Huu ni ugomvi unaomuhusisha Mzee Ruangisa na kampeni za umeya na wala haijabadili upepo wa kampeni za ubunge, Lwakatare asijipe matumaini yasiyokuwepo.
 
ccm wamekwisha elekea Kibra, wamekaa mkao wakuliwa, hatuna wasiwasi nao, tunajielekeza kuwamaliza 31 October
 
Huu ni ugomvi unaomuhusisha Mzee Ruangisa na kampeni za umeya na wala haijabadili upepo wa kampeni za ubunge, Lwakatare asijipe matumaini yasiyokuwepo.
Huo ugomvi wa umeya unaweza ukawasaisia wapinzani.
 
Kuna mengi nyuma ya issue hii ambayo hatuyajui.
Hata hivyo kushindwa kwa sisi m Bukoba mjini ndiko kunawapa homa viongozi wa jimbo hilo. Na sasa wanatafuta mchawi kabla mgonjwa hajafa.

Kama mwenyekiti Robert Bahati ambaye binafsi amegombea udiwani mara nyingi na kushindwa na upinzani akiweza kutuambia mbona ushirikiano wa Kagasheki na watendaji wa chama chake ni wa kutia shaka katika kipindi hiki chote cha uchaguzi, nitakuwa wa kwanza kumpiga mawe mwizi wa ushindi wa wao sisi m.

Imefikia mahali Kagasheki anasema wazi bila yeye sisi m Bukoba ilikuwa haipo. Na alikuja kama mwokozi wao.
 
Back
Top Bottom