The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,968
- 2,957
Kuna kila dalili kwamba CCM itaendelea kututawala watanzania kwa namna yoyote kwa miaka mingi ijayo, na ukizingatia kwamba mtaani njaa ni kali sana.
Hata kama ingekua ni wewe ndugu yangu, katika mazingira kama ya Tanzania ambapo chama tawala kinahodhi kila kitu serikalini, ungeacha kutumia fursa hiyo kugandamiza wapinzani ili uendelee kula mema ya nchi?
Hata hivyo kuna mambo ya msingi ambayo sisi kama wananchi kwa umoja wetu tukiyapazia sauti angalau hawa watawala wanaweza kutusikia na kurekebisha mambo kuliko kukaa kimya au kulalamika tu na kusubiri CCM iondoke madarakani jambo ambalo sioni dalili likitokea hivi karibuni.
Hivyo nikuombe mdau uorodheshe mambo ambayo unadhani CCM inapaswa kujibadilisha/kubadilika ili yatufae sisi wananchi wote ikiwemo na wa vyama vingine na si CCM peke yao.
Maana hii nchi ni yetu sote si ya CCM peke yao.
Hata kama ingekua ni wewe ndugu yangu, katika mazingira kama ya Tanzania ambapo chama tawala kinahodhi kila kitu serikalini, ungeacha kutumia fursa hiyo kugandamiza wapinzani ili uendelee kula mema ya nchi?
Hata hivyo kuna mambo ya msingi ambayo sisi kama wananchi kwa umoja wetu tukiyapazia sauti angalau hawa watawala wanaweza kutusikia na kurekebisha mambo kuliko kukaa kimya au kulalamika tu na kusubiri CCM iondoke madarakani jambo ambalo sioni dalili likitokea hivi karibuni.
Hivyo nikuombe mdau uorodheshe mambo ambayo unadhani CCM inapaswa kujibadilisha/kubadilika ili yatufae sisi wananchi wote ikiwemo na wa vyama vingine na si CCM peke yao.
Maana hii nchi ni yetu sote si ya CCM peke yao.