Pre GE2025 CCM inajua kuwa kumshambulia Mbowe ni kuendelea kumwongezea umaarufu?

Pre GE2025 CCM inajua kuwa kumshambulia Mbowe ni kuendelea kumwongezea umaarufu?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Ni wazi kuwa mpinzani mkuu wa CCM ni CHADEMA! Ndiyo maana hata sisi tusio na vyama vya Kisiasa si shida kutambua kuwa kati ya wanasiasa wanaoipa tabu CCM ni Mbowe na Lissu!

Kwa miaka nenda Rudi, kwa mfano, CCM imekuwa ikimzodoa Mbowe kuwa kakaa muda mrefu madarakani. Lakini kama kukaa madarakani ni issue, kwa nini isiwanange na wanasiasa wengine kama akina John Cheyo na Profesa Lipumba?

Hiyo inatosha kutoa taswira kuwa Mbowe anawanyima usingizi. Vinginevyo, wangempuuzia kama ilivyowapuuzia na akina Lipumba na Cheyo.

Leo hii CCM wanalalamika kuwa Mbowe anatumia chopa na msafara wa magari mengi wakati Lissu akitumia gari moja tu, kwamba inasikitisha na hiyo hali mpaka wakiamua kumchangia. Unajua hiyo nayo inachekesha ee! CCM inamuonea Lissu huruma? Kweli? Ama kweli wanasiasa ni "wanafiki" mno!

Kama ni kweli Mbowe anatumia usafiri bora kuliko makamu wake ni sawa kama ndivyo walivyokubaliana, na hakuna cha ajabu. Hata katika nchi huwezi kulinganisha ukubwa wa msafara wa Rais na viongozi wengine. Mkubwa atabaki kuwa mkubwa tu.

Kama CCM haijui, ni bora kada mwelewe aieleweshe kuwa kumsema Mbowe ni kumwongezea mileage kisiasa.

Mwembe wenye matunda ndiyo hupigwa mawe!

 
1723735417503.jpg
 
Ni wazi kuwa mpinzani mkuu wa CCM ni CHADEMA! Ndiyo maana hata sisi tusio na vyama vya Kisiasa si shida kutambua kuwa kati ya wanasiasa wanaoipa tabu CCM ni Mbowe na Lissu...
Halafu kutwa kucha wanamsema lakini yeye hata siku moja hajawajibu yaani amewapuuza.
 
Viongozi Washamba wa ccm hawawezi kumpa Umaarufu Mbowe, Ambaye ndiye kiongozi pekee wa kisiasa Katika walio hai nchini Tanzania mwenye exposure kuliko yoyote.

Kwa mfano , Mkulima wa Mpunga mvomero kama Makalla anawezaje kumpa umaarufu Mbowe mwenye Mahoteli Dunia nzima?
 
Unakuaje mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo alafu unang'ang'ania madarakani miaka 20+ hiyo demokrasia iko wapi?
 
Unakuaje mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo alafu unang'ang'ania madarakani miaka 20+ hiyo demokrasia iko wapi?
Mbona CCM imedumu kwenye madaraka miaka 60 kwa nguvu afadhali ya mbowe.
 
Mbona CCM imedumu kwenye madaraka miaka 60 kwa nguvu afadhali ya mbowe.
Mbowe akikabidhiwa nchi akiwa Rais kwa tabia yake ya kung'ang'ania madaraka hawezi kutoka atakua kama nkurunzinza
 
Mbowe akikabidhiwa nchi akiwa Rais kwa tabia yake ya kung'ang'ania madaraka hawezi kutoka atakua kama nkurunzinza

..Mbowe hakuwa mgombea pekee ktk nafasi ya Mwenyekiti wa Chadema.

..kwa nafasi ambazo hazina ukomo wa kutumikia haina tatizo mhusika kugombea ilimradi wananchi wanamkubali.

..kuna wana-Ccm wako bungeni kwa kipindi kirefu kuliko Mbowe alivyokuwa Mwenyekiti Chadema.
 
Unakuaje mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo alafu unang'ang'ania madarakani miaka 20+ hiyo demokrasia iko wapi?
Unajua waliompa nafasi hiyo ni wanachama, tena kipindi cha dokta slaa ndio wakapiga kura hiyo, si kwamb alitaka ila wenyewe walimpa
 
Ni wazi kuwa mpinzani mkuu wa CCM ni CHADEMA! Ndiyo maana hata sisi tusio na vyama vya Kisiasa si shida kutambua kuwa kati ya wanasiasa wanaoipa tabu CCM ni Mbowe na Lissu!

Kwa miaka nenda Rudi, kwa mfano, CCM imekuwa ikimzodoa Mbowe kuwa kakaa muda mrefu madarakani. Lakini kama kukaa madarakani ni issue, kwa nini isiwanange na wanasiasa wengine kama akina John Cheyo na Profesa Lipumba?

Hiyo inatosha kutoa taswira kuwa Mbowe anawanyima usingizi. Vinginevyo, wangempuuzia kama ilivyowapuuzia na akina Lipumba na Cheyo.

Leo hii CCM wanalalamika kuwa Mbowe anatumia chopa na msafara wa magari mengi wakati Lissu akitumia gari moja tu, kwamba inasikitisha na hiyo hali mpaka wakiamua kumchangia. Unajua hiyo nayo inachekesha ee! CCM inamuonea Lissu huruma? Kweli? Ama kweli wanasiasa ni "wanafiki" mno!

Kama ni kweli Mbowe anatumia usafiri bora kuliko makamu wake ni sawa kama ndivyo walivyokubaliana, na hakuna cha ajabu. Hata katika nchi huwezi kulinganisha ukubwa wa msafara wa Rais na viongozi wengine. Mkubwa atabaki kuwa mkubwa tu.

Kama CCM haijui, ni bora kada mwelewe aieleweshe kuwa kumsema Mbowe ni kumwongezea mileage kisiasa.

Mwembe wenye matunda ndiyo hupigwa mawe!

View attachment 3071248
umaarufu wa kihalifu right?🐒
 
Back
Top Bottom