CCM inapata wapi uhalali wa kuwafundisha watu ustaarabu?

CCM inapata wapi uhalali wa kuwafundisha watu ustaarabu?

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Kiongozi Mkuu wa CCM aliwahi kuwaambia wananchi waliokuwa wakilalamikia ukubwa wa tozo ya huduma ya choo kuwa, kama hawataki kulipia hiyo tozo, wabakie na mavi yao.

Waziri wa Serikali ya CCM aliwahi kuwaambia wananchi waliokuwa wakilalamikia ukubwa wa tozo ya huduma za kivuko Kigamboni kuwa, kama hawataki kulipa, waogelee.

Kiongozi Mkuu wa UVCCM aliwahi kuwatamkia wananchi kuwa mara ya kwanza risasi zilishindwa kumwua (TL), akija safari hii tutamwua kwa kumdunga sindano. Ni huyo huyo aliwaambia wananchi wa Arusha kuwa ili kuwathibitishia UVCCM ni wanaume, itabidi wawatie mimba wake zao (yaani wake wa wananchi wa Arusha).

Ni waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Serikali ya CCM aliyethubutu kutoa kauli ya kufuru na kuwakera waumini wa kweli wa dini zote, akamtaja Magufuli kama Mheshimiwa Mungu.

Ni waziri wa mambo ya ndani wa serikali ya CCM, aliyewahi kukufuru na kuwakera wakristo kwa kutamka kuwa Magufuli ni kama Yesu.

Ni mkuu wa mkoa wa serikali ya CCM , aliyewahi kutamka hadharani na kuwakera watu wanaomwabudu Mungu, kuwa eti Mungu anatakiwa kumshukuru Magufuli.

Leo Mdude, aliyekuwa gerezani kwa zaidi ya mwaka mzima kwa kuonewa na utawala dhalimu, asiyejua kiundani Rais wa sasa yupoje, alipopewa nafasi ya kusalimia, akatamka kuwa ataendeleza mapambano, kwa wembe ule ule alioutumia kumnyolea Rais aliyetangulia. Kwangu mimi, hii ilikuwa ni kauli yenye ukakasi, na haikustahili kutamkwa dhidi ya Rais Samia, angalao kwa sasa. Lakini nina imani hata Rais Samia mwenyewe atakuwa amesamehe. Huyu mtu kwanza katekwa, kapigwa mpaka kukaribia kufa, kabambikiwa kesi na Serikali ya CCM, akitoka, kwake inakuwa vigumu kumtenganisha mtu binafsi na serikali dhulumati iliyokuwa imemtesa na kumwonea.

Lakini jambo la msingi la kujiuliza, hata kama Mdude katoa kauli mbaya, CCM ina uhalali wowote wa kukemea? Hivi jambazi ana uhalali wa kumlaani mdokozi? Chama kinachoteka wagombea wa upinzani wakati wa uchaguzi, chama kinachofuta wagombea wa uchaguzi wa vyama vingine, chama kinachoongoza Serikali inayoruhusu uwepo wa makundi ya watu wasiojulikana, makundi yanayofanya kazi ya kuua, kuteka, kupoteza watu na kubambikia watu kesi, kina uhalali wa kukemea kauli ya Mdude, kauli isiyo na athari yoyote kwa uhai wa mtu yeyote?

CCM hamna haki ya kumfundisha mtu yeyote ustaarabu. Ninyi ni sehemu ya uharamia mwingi unaofanyika kwenye nchi hii. Hivi Serikali iliyomwonea na kumbambikia Mdude kesi ya madawa ya kulevya, ilikuwa ya ACT au CCM? Hivi serikali iliyoua watu kule Zanzibar kwaajili ya uchaguzi kule Zanzibar ilikuwa ya DP au CCM? Hivi Serikali iliyokuwa inawapora wananchi pesa kwenye accounts zao, iliyokuwa inawabambikia kesi watu za uhujumu uchumi na itakatoshajo fedha haramu, ilikuwa Serikali ya UMD au ya CCM?

CCM muwe na aibu, ninyi ni wa kufundishwa ustaarabu, siyo wa kumfundisha mtu yeyote ustaarabu. Siasa zenu na uongozi wenu ni primitive.

Tunamwombea Mama Samia, hata kama yupo katikati ya uchafu mwingi wa CCM, hekima imtawale, ausafishe uchafu wote. Hilo linawezekana, akidhamiria, akivaa ujasiri, na Mungu akiwa naye daima.
 
Kuihusisha CCM na ustaarabu ni vitu viwili tofauti, kwasababu wao wamechafuka kwa ushenzi sasa wanalazimisha kuwachafua na wengine kwa kuwawekea maneno mdomoni ili wawafunge midomo wanaodai haki zao.
 
2183704_IMG_1183.jpg
 
Ccm wameona aibu kwa ile hukumu ya Mdude kwani imemuacha uchi yule kiongozi muovu. Sasa wanajaribu kucheza na maneno ya hisia kali za mdude baada ya kuumizwa sana. Lengo lao hasa ni kufunika ile aibu ya mwendazake, na kutaka kumjaza mama apige marufuku mikutano ya kudai katiba mpya. Hili la mikutano ya kudai katiba mpya ni kitisho kikubwa sana kwao, hivyo namna pekee ni kurejea kwenye mbeleko yao halisi ya madaraka ya urais, ili wabaki salama.
 
CCm hawafanyi KWA makosa lengo lao nikutoa kwenye mjadala wa KATIBA MPYA, kauli ya Mdude wanaivalia bango KWA makusudi, CCM watu wa ajabu Sana hoja hawana ila Sasa kudemka na Mambo madogo hawajambo ukiacha na WANACCM HURU, wengine tupa kule
 
Imagine hawa leo hii ndiyo wanataka wafundishe watu ustaarabu!👇WTF!!!
5tfvce11.png
 
CCm hawafanyi KWA makosa lengo lao nikutoa kwenye mjadala wa KATIBA MPYA, kauli ya Mdude wanaivalia bango KWA makusudi, CCM watu wa ajabu Sana hoja hawana ila Sasa kudemka na Mambo madogo hawajambo ukiacha na WANACCM HURU, wengine tupa kule
Ni punguani pekee ndiye atakayesema hakuna haja ya katiba mpya.

Tume ya katiba ya Warioba iliwahoji wanaCCM na wasio wana CCM.

Kufuatana na report ya Tume ya Jaji Warioba, wengi walisema wanataka katiba mpya, wachache walisema hawahitaji katiba mpya, walitaja mambo ambayo wanataka yabadilishwe kwenye katiba ya sasa, lakini mabadiliko waliyoyataja, kimsingi, kwa maoni ya Tume, ilikuwa inamaanisha kuibadilisha katiba ya sasa. Na kwa maoni ya Tume, ni kwamba watu hao nao walikuwa wanataka katiba mpya.

Tume ya katiba haikuundwa na Mbowe, iliundwa na Rais Kikwete. Waliohojiwa hawakuwa wanachama wa CHADEMA, bali wananchi wa Tanzania bila kujali itikadi zao. Report hiyo ya Tume ya Warioba, ndiyo uthibitisho wa pekee ambao tunao mpaka leo, kuwa Watanzania wanahitaji katiba mpya.
 
Imagine hawa leo hii ndiyo wanataka wafundishe watu ustaarabu![emoji116]WTF!!!
View attachment 1840787
Ndani ya CCM kuna wendawazimu wengi kuliko tunavyodhania. Halafu mtu punguani kama huyu leo amepewa nafasi ya kuwaongoza watu wenye akili timamu.

Ndiyo maana tunahitaji katiba mpya. Katiba itakayozuia watu punguani kama huyu Heri James, kuwa kiongozi wa watu wenye akili timamu, huku ni kuwadhihaki na kuwatukana Watanzania wote wenye akili sawia.
 
Ni punguani pekee ndiye atakayesema hakuna haja ya katiba mpya.

Tume ya katiba ya Warioba iliwahoji wanaCCM na wasio wana CCM.

Kufuatana na report ya Tume ya Jaji Warioba, wengi walisema wanataka katiba mpya, wachache walisema hawahitaji katiba mpya, walitaja mambo ambayo wanataka yabadilishwe kwenye katiba ya sasa, lakini mabadiliko waliyoyataja, kimsingi, kwa maoni ya Tume, ilikuwa inamaanisha kuibadilisha katiba ya sasa. Na kwa maoni ya Tume, ni kwamba watu hao nao walikuwa wanataka katiba mpya.

Tume ya katiba haikuundwa na Mbowe, iliundwa na Rais Kikwete. Waliohojiwa hawakuwa wanachama wa CHADEMA, bali wananchi wa Tanzania bila kujali itikadi zao. Report hiyo ya Tume ya Warioba, ndiyo uthibitisho wa pekee ambao tunao mpaka leo, kuwa Watanzania wanahitaji katiba mpya.
Wape dawa mkuu , ccm vichwa aina ya kwako ni wachache , madini Kama madini Yani thanks
 
Sasa hivi watamnyosha...
Subutu labda Kama mungu yupo likizo, SSH rais akiwasikiliza wapambe akaanza leta ya mwenda zake amini nawambieni Kama mungu haishivyo miaka yake 4 Kama kiongozi aliobakiza ataioyona Kama miaka 100, acheni mchezo nawambia
 
Back
Top Bottom