Tetesi: CCM kumtema Dr. Magufuli 2020 katika kinyang'anyiro cha urais?

Tetesi: CCM kumtema Dr. Magufuli 2020 katika kinyang'anyiro cha urais?

Rais2020

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2016
Posts
3,248
Reaction score
5,537
Amani itawale wana jf wote.
Imezoeleka kuwa kila baada ya miaka mitano ya awamu ya kwanza kwa kila rais anayeingia madarakani kupitia CCM huwa wanautaratibu wa kumwachia tena amalizie awamu ya Pili ya miaka mitano iliyobaki ili akamilishe miaka 10 ya awamu yake ya uongozi.

9ddf773dc36c4adb2f84bedb9036d13c.jpg


Katika kuendelea kukusanya mawazo kutoka kwa wanasiasa nguli wa CCM ili kutaka kujua wanauonaje uongozi wa mhemshimiwa sana.

Katika hali ya kushangaza kabisa mmoja wa kada nguli wa chama hicho akiongea na mimi bila kificho akiwa na wenzake alisema " tunashangaa awamu hii mambo yanaenda hovyo hovyo na hii itatufanya sisi kufanya maamuzi ya ajabu 2020 katika kumpata mgombe wa ndani kukiwakilisha chama".

Wanachama hao na wenye nafasi kubwa kabisa katika baraza la mawaziri walienda mbali zaidi na kusema " inaumiza sana nchi kuendeshwa bila kufuata misingi ya katiba".

Wanachama hao walinipa mawazo mengi na kunitia moyo ili mwaka 2020 niweze kugombea uraisi maana hata wao walisema watamweka mgombea ambaye ni kama akinishinda basi atawaongoza wananchi kwa kufuata katiba ya nchi,atasikikiza vilio vya watumishi Hewa,ataboresha afya na elimu.

Kiukweli wanachama na makada HAWA nguli wa chama pendwa walinitia moyo sana na sasa najipanga kwa ajili ya kuhakikisha nainyakua nchi hii maana yule mheshimiwa mwenye uwezo wa kupiga push ups hatagombea tena.

Aidha niwaombe wananchi na wapiga kura wangu wavumilie hii hali maana miaka minne iliyobaki sio mingi sana na 2020 Wananchi bila kujali kama ni tajiri au masikini wataishi kama malaika na sio kama mashetani.

ed4dab598097d19dea712a3deb4aadbc.jpg


Mwisho. Nawaomba mjifunge mkanda kuelekea 2020.

Rais2020
Rais wa mioyo ya watu
Nitarejesha matumaini yaliyopotea kwa watanzania.
 
Kama mlishindwa kusimamia katiba ya chama chenu pamoja na mbwembee zote katika kumtafuta mwenyekiti wenu mkaendelea na utamaduni wenu basi hata hili unalolisema hamwezi kulitekeleza
 
Yaani yeye ndiyo mwenyekiti wa chama yeye ndiyo boss wa kila kitu wanaanzaje kumtema hebu tupe taratibu za kumuengua mwenye nchi
 
Dah... Kama elfu mbili na kumiii...
Ukiwa na[emoji294] [emoji418] [emoji418] [emoji418] itakufuata popote[emoji13] [emoji13]
 
Mtoa mada anaota..Akiamka atakijukuta yupo wodi ya mirembe!Tumsamehe
 
hivi kama sio ndoto za Asubui! Yaani Mwenye Rungu Anaweza kuenguliwa?

Kama alitamka Adharani kwamba, ingekuwa ni yeye Pale Wanaccm walipoimba tuna Imani na Lowassa, Angewafurusha Wote Unategemea Nini na sasa yeye ndiye Kapteni?
 
tulia wewe.Magufuli Ndie Raisi Wako Mpaka 2025.Na Mwenyekiti Wako Mpaka 2026!
 
Mkuu nimecheka peke yangu maana naona unamtishia dereva na bastora wakati yeye anaweza kulipeleka gari korongoni mkapotea wote
 
Mzee wa Monduli kishajiunga kabisa na bundle ya kugombea Urais 2020 hakuna mchezo
 
Yaani yeye ndiyo mwenyekiti wa chama yeye ndiyo boss wa kila kitu wanaanzaje kumtema hebu tupe taratibu za kumuengua mwenye nchi
kuna watu wana pull strings wenye ushawishi zaidi yake nadhani, ishu ya Lowassa ndio inaniambia kila kitu ni possible ccm hata kama una nguvu kiasi gani ndani ya chama
possible but unlikely
 
Naona kuna vita kali sana kati ya Ukaskazini na Usukuma/kanda ya ziwa, naona hawa jamaa wa kaskazini wamekomaa kweli kumchafua Magufuli lakini nawaomba muwe wavumilivu uchumi utasimama na Magufuli atakumbukwa kuliko matarajio.
 
Kinachowapa jeuri Ccm ni tume ya chaguzi na katiba iliyopo....
Tukiweza ondoa hii na tukiziweka sawa Ccm ananguka kiulaini tu

Ova
 
Amani itawale wana jf wote.
Imezoeleka kuwa kila baada ya miaka mitano ya awamu ya kwanza kwa kila rais anayeingia madarakani kupitia CCM huwa wanautaratibu wa kumwachia tena amalizie awamu ya Pili ya miaka mitano iliyobaki ili akamilishe miaka 10 ya awamu yake ya uongozi.

9ddf773dc36c4adb2f84bedb9036d13c.jpg


Katika kuendelea kukusanya mawazo kutoka kwa wanasiasa nguli wa CCM ili kutaka kujua wanauonaje uongozi wa mhemshimiwa sana.

Katika hali ya kushangaza kabisa mmoja wa kada nguli wa chama hicho akiongea na mimi bila kificho akiwa na wenzake alisema " tunashangaa awamu hii mambo yanaenda hovyo hovyo na hii itatufanya sisi kufanya maamuzi ya ajabu 2020 katika kumpata mgombe wa ndani kukiwakilisha chama".

Wanachama hao na wenye nafasi kubwa kabisa katika baraza la mawaziri walienda mbali zaidi na kusema " inaumiza sana nchi kuendeshwa bila kufuata misingi ya katiba".

Wanachama hao walinipa mawazo mengi na kunitia moyo ili mwaka 2020 niweze kugombea uraisi maana hata wao walisema watamweka mgombea ambaye ni kama akinishinda basi atawaongoza wananchi kwa kufuata katiba ya nchi,atasikikiza vilio vya watumishi Hewa,ataboresha afya na elimu.

Kiukweli wanachama na makada HAWA nguli wa chama pendwa walinitia moyo sana na sasa najipanga kwa ajili ya kuhakikisha nainyakua nchi hii maana yule mheshimiwa mwenye uwezo wa kupiga push ups hatagombea tena.

Aidha niwaombe wananchi na wapiga kura wangu wavumilie hii hali maana miaka minne iliyobaki sio mingi sana na 2020 Wananchi bila kujali kama ni tajiri au masikini wataishi kama malaika na sio kama mashetani.

ed4dab598097d19dea712a3deb4aadbc.jpg


Mwisho. Nawaomba mjifunge mkanda kuelekea 2020.

Rais2020
Rais wa mioyo ya watu
Nitarejesha matumaini yaliyopotea kwa watanzania.
Hii ni taarifa ya kutunga, au ulimuhoji yule ambaye mirija ya ulaji ilizibwa.
 
Back
Top Bottom