Elections 2010 CCM Kupoteza Moshi Vijijini-Lyatonga Mrema Kuibuka Kidedea!

.
io
Asante kwa sahihisho, hii Moshi Vijijini na Vunjo bado inanichanganya sana. Namkumbuka Mbatia aliwahi kulitwaa, akaja Jesse Makundi ndipo akaingia Kimaro, hivi Mrema naq aliwahi, enzi zake akiwa CCM.
Ndio, Mrema alikuwa ni kati ya wabunge walioshinda kwa kura nyingi wakati huo. Kupewa uwaziri ni kutoka na umachachari wake jimboni Moshi Vijijini -kabla haijagawanywa kuwa Vunjo na Moshi Vijijini- ambao ulimfanya kuandikwa sana kwenye magazeti kipindi hicho.

Alianza ubunge kwa nguvu ya hali ya juu. Mapolisi kipindi hicho walikuwa wananuka rushwa na unyanyasaji kutoka kwa wafanya biashara wadogo wa boda,mpakani mwa Kenya na Tanzania na kuwaacha wafanya biashara wakubwa ambao walikuwa wadili na maboss zao.
Umaarufu wa Mrema ulikuja kwa kuwatetea awa wafanya biashara wadogo hasusani wakinamama. Kama sijakosea alimpiga Polisi mmoja vibao kwa kukimbizana na wakina mama wanaofanya biashara ndogo ndogo na hii kama sijakosea tena ndiyo iliyompa uwaziri.

Kwa hiyo sitashangaa wanavunjo kuchagua Mrema kwa mazuri aliyowatendendea. Mimi binafsi ninaamini Mrema wa sasa hivi sio yule wamiaka ishirini iliyopita.

 
 
Mimi ninaamini wamemchagua Salakana kutokana mentality kwamba alishashinda ubunge akiwa Chadema kwa hiyo anawaelewa Chadema- ambao wamelishikilia jimbo la Moshi mjini kwa miaka kumi-zaidi mgomea yoyote yule.
 
Jana nikiwa pale njia panda L A Mrema alikwenda kufunguwa tawi mbele ya stendi mpya ya njia panda aliondoka na msafara wa magari 3 suzuki yake ya matangazo na shangigi lake pamoja na kenta yenye muziki ilikuwa mida ya saa 3 asubui basi baada ya kufungua hilo tawi jipya alirudi kwa miguu huku akishangiliwa na kina mama wapatao 20 hivi akicheza taarabu iliyokuwa ikivurumishwa kwenye kenta yake, nikajaribu kwadodosa watu wapale njia panda wakasema mrema anakubalika sana vunjo hivyo nilazima atashinda ingawa watu wanamwona amechoka (kisisasa) kwao bado ananguvu sana tena wakasema bunge la mwakani litakuwa zuri sana kwani mrema atakuwapo, mbowe,zito,halima mdee, marando,lisu,ndesamburo nk.
 
mrema alienda nyumbani kwa kimaro asubui saa kumi na mbili na mazungumzo yalikuwa hivi
mrema; aloyece kimaro una nini na mimi mrema, weni mmeo omao?, yaani mini ni mme wa mamako? tazama kimaro , wewe ndo uliongoza wafanyibiashara wenzakko mkaninjengea nyumba pale kiraracha wakati huo miye waziri lakini nina nyumba ya udongo unakumbuka? nilipoamua kuasisi mageuzi ukajiunga na mimi, mpaka leo sijui zile t-shirt, fulana, vitenge , nk vya chagua mrema 1995, ulivitoa wapi na mpaka leo sijadaiwa hata sumni! leo napigania ubunge baada ya ccm kukutosa wewe nasikia unapita majukwaani kunitukana!, kama nampigia kampeni kikwete rais wako, na kwa kuwa ccm mkoa walikutosa je kwa nini unawababe?

ALOYCE KIMARO AKABLOO SASA YUKO NA MREMA
 
wakati akiwa waziri kahawa iliuzwa 2400/= kwa kilo, so wanahope itakuwa hivyo tena
 
Kiukweli jimbo la vunjo ni kubwa sana. Linatakiwa kugawanywa. La sivyo madiwani wawe wa kutosha kabisa. Nadhani ndugu Pasco umetembea vizuri huko na kuona hali ya kimaisha. Kimaro hakufanya lolote! Watu wanang'oa mikahawa na kubakiza migomba tu. Inamaanisha zao hilo la kiuchumi limesahauliwa. Leo hii ukipita pale Kyala KNCU ni kama mahame. Vijana mle wamekuwa wahuni mno! Sasa wakiona haya na mengine wanaona bora wamkumbuke Mrema ambaye aliwaonjesha neema wakati fulani. Huwezi kujua labda mambo yatabadilika kiasi. Ile barabara toka mtoni hadi kilema inahitaji lami na mambo yanaweza kubadilika kuanzia hapo
 
Kunatofauti gani kati ya Mrema na sisimu njoo kwetu tule rasilimali ya nchi MREMA NI MWASIASA UCHWARA MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Hata mimi ningelikuwa Vunjo kura yangu ningempa A Mrema kwasababu huko nyuma alionyesha kwa matendo kwamba ana ubunifu na aliweza kukabiliana na matatizo ya wananchi si kwa maneno ya majukwaani bali kwa vitendo mitaani.

Pamoja na uzee bado Mrema ni bora kuliko hawa wanasiasa wa majukwaani.

Kila la heri Mrema!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…