CCM Kutawala Milele!

CCM Kutawala Milele!

Mtyama

Member
Joined
Feb 1, 2008
Posts
53
Reaction score
25
Ndugu wanabodi,

Salaam!

Nianze kwa kusema kwamba, nawapenda sana Wachina na naipenda sana China. Kwa historia, China si tu rafiki zetu; kwa Taifa letu la Tanzania na Bara zima la Afrika, China ni ndugu zetu. Tufikirie pia kama nchi, Tanzania tulivyoipambania China hiyo miaka ya 1970s huko UN hadi China kupata kura ya turufu (veto power) katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC).

Tofauti na nchi nyingi za Magharibi, China huwa haipendelei kushinikiza ushawishi wake kwa nchi rafiki au nchi ndugu kama Tanzania. Vyema tukailewa vyema China, na kama taifa, China ni taifa linalotupenda na kwa hatua kubwa za kimaendeleo China walizofikia, hawapendi kutuacha katika hatua zao hizi za kimaendeleo.

Vyama vingi vya Ukombozi wa Bara letu, vinavyoshindwa chaguzi kuu (karibu vyote), havijawahi kurejea madarakani. Chama chetu tawala, CCM vyema wakatambua kuwa chama cha CPC cha China na kama chama rafiki kwa CCM na kwa vyama vingine rafiki vya Ukombozi vinavyoendelea kuongoza dola, vinasaidiwa kujengewa uwezo wa hata kama vinaposhindwa kwenye chaguzi viweze kuwa na uwezo wa kurejea mamlakani.

Utawala wa Milele

Tanzania kama taifa inaongozwa kwa Katiba, Sheria na Taratibu. Utangulizi (Preamble) wa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatamka kuhusu Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na pia kuhusu Siasa za Vyama Vingi. Umilele una Mungu!

Nasema naipenda China kwa sababu China kama ndugu zetu, wanatufahamu fika. Vyema basi nasi tukawafahamu. Rais kutamka kuhusu CCM kutawala milele tena mbele ya delegation ya China inaonekana kuwa kauli ya kimkakati kama vile taifa kuondokana na siasa za kiushindani ila kama tumewaelewa vyema hawa ndugu zetu China, vyema mikakati hiyo kama kweli ndivyo hivyo, basi ikawa kwenye mchakato wa Kikatiba.

China si kwamba hawana Upinzani. Wana vyama 8 vya Upinzani selected kutoka sekta muhimu ambavyo hushiriki kwenye mikutano mikuu ya kitaifa, National People's Congress (NPC) na Chinese People's Political Consultative Conference (CPPCC). Mikakati hii na mingine ya kisekta ndiyo imewafanya China kuwa taifa shindani na lenye nguvu kubwa ya kiuchumi na kiushawishi, duniani.

Mikakati Yetu

Vyema kama taifa tukajitafakari kwa maono (vision), dira na dhima yetu ya wapi kama taifa tunaelekea maana hatujachelewa bado na ndugu zetu China wanatuonyesha njia. Kama China wamekuwa na Baraza Kuu la Kiushauri wa Kisiasa (People's Political Consultative Conference), vyema nasi tukaanza na hawa Viongozi wetu Wastaafu.

Kuwa na Baraza la Kiushauri kwa maoni yangu, kutasaidia kuwa na ushauri mwema na mzuri sana kimkakati hata kuelekea kurasimisha ushauri mzuri na maoni mengine mazuri ya kimaendeleo na kuyaweka katika Katiba yetu.

Hofu kubwa ya CCM ni kushindwa katika Uchaguzi Mkuu, na vyema ikaeleweka pia kuwa kushindwa kwa CCM katika Uchaguzi Mkuu ni elekeo la anguko lake hivyo si rahisi CCM kukubali kushindwa. Pengine ndiyo maana tunawasikia wakuu wa chama wakiyatamka haya, japo binafsi naweza pia kusema kuwa ni katika kupigana 'vijembe'.

Kama 'umilele' unaotamkwa ni katika mipango ya mikakati ya kitaifa, vyema basi CCM kama chama tawala wakaongoza mikakati hii katika sura ya kitaifa ili kupata mustakabali mwema wa kitaifa zaidi na hata baadae nchi kuwa na mikakati endelevu na ya kupiga hatua kubwa za kimaendeleo; kikanda na kimataifa (China Model).

Kusita kuwa na mikakati hii na kwa dalili zinazojitokeza miongoni mwa watu, kuna athari zake, tena kubwa. Binafsi ninaejiita Mpinzani, pia sitoweza sita kupambania haki zetu hizi za Kikatiba na haki zingine za msingi.

Uchumi bora, maisha bora, maendeleo bora; yote haya hayatakuwa na tija kama haki za Kikatiba na zile za msingi kukiukwa (utawala wa milele pasipo haki), sina shaka wengi tutaendelea kupambana katika kujenga Taifa la Haki.

Tusiende ndivyo sivyo hadi hao tunaowaita 'mabeberu' nao kuanza kama vile kutusaidia katika kutafuta hizi haki zinazokiukwa, na hasa wanavyoona tunavyokaribiana zaidi na ndugu zetu, China.

Mungu Ibariki Tanzania

Gerald Josephat Nyerere,
Musoma, Mara.

www.muhunda.com
 
Ndugu wanabodi,
Hofu kubwa ya CCM ni kushindwa katika Uchaguzi Mkuu, na vyema ikaeleweka pia kuwa kushindwa kwa CCM katika Uchaguzi Mkuu ni elekeo la anguko lake hivyo si rahisi CCM kukubali kushindwa. Pengine ndiyo maana tunawasikia wakuu wa chama wakiyatamka haya, japo binafsi naweza kusema kuwa ni katika kupigana 'vijembe'.
Mungu Ibariki Tanzania

Gerald Josephat Nyerere,
Musoma, Mara.

CCM kutumia Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi, Inajua Ikishindwa Ndio Itakufa Jumla, Itakubali?

P.
 
Shukurani kwa uchambuzi na kwa makala zako, Paschal.
 
Shukurani kwa uchambuzi na kwa makala zako, Paschal.
Tatizo CCM haiwezi Kujifananisha na CPC kule China hata ukiwa kiongozi wa chama ukiwa na matendo machafu haswa kula rushwa unakamatwa na kushtakiwa kitu ambacho CCM kimewashinda, CPC kule China inaangazia zaidi maendeleo ya nchi na watu wake katika nyanja zote tofauti na Tanzania ambapo viongozi wanatazama mifuko yao na ndugu zao tu.
 
Ahead of BRICS, China’s Xi Jinping begins Africa visits

By AT editor - 19 July 2018 at 5:14 am

Xi.jpg


President Xi Jinping of China begins Thursday a trip that will bring him to Senegal and Rwanda for state visits, before he heads to South Africa and the BRICS Summit in Johannesburg.

“The visits will promote the further deepening of political mutual trust, mutual development assistance, mutual learning on each other’s concepts between China and Africa and the building of a closer China-Africa community of common destiny,” said China’s Ministry of Foreign Affairs (MFA).

Xi begins his tour in the United Arab Emirates before heading for Senegal. There, the Chinese leader will meet with President Macky Sall to deepen cooperation between the two governments ahead of the Forum on China-Africa Cooperation (FOCAC) to be held in September in Beijing. It will be the first time he visits a West African nation, the MFA said.

It will also be Xi’s first visit to Rwanda, and the first by a Chinese president, as he meets with President Paul Kagame. “They will jointly witness the signing of a series of cooperation agreements to elevate China-Rwanda practical cooperation to new highs,” the Chinese MFA said in a statement.

In South Africa, Xi will hold talks with President Cyril Ramaphosa before attending a celebration marking the 20th anniversary of the establishment of China-South Africa diplomatic relations. He will stay in Johannesburg for the BRICS meetings, which begin on Wednesday.

“We look forward to strengthening cooperation among the five countries,” Beijing said, in what it describes as a “new industrial revolution among the BRICS countries.”

Xi also will meet with Prime Minister Pravind Kumar Jugnauth in Mauritius on his return trip from the summit.

Image: MFA China/Xinhua
 
Sidhani. Tumejaribu kujenga mazingira bora ya kisiasa tangu Uhuru na inaonekana tumeshindwa kujenga uwanja sawa wa kiushindani nchini tangu mapokeo ya mageuzi ya kisiasa duniani. Hatujachelewa bado, muhimu tuwe na dhamiri njema katika ujenzi wa taifa lenye kujali HAKI.
 
Back
Top Bottom