Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Chama cha Mapinduzi (CCM), kimetoa onyo kwa watu wote wanaojipitisha katika majimbo kutaka ubunge kabla ya muda sahihi, hivyo kitawashughulikia.
Akizungumza katika uzinduzi wa ofisi ya CCM Wilaya ya Newala mkoani Mtwara Machi 1, 2025, Katibu wa Organizesheni wa chama hicho, Issa Ussi Gavu amesema atakayebainika kusumbua ufanyaji kazi wa wabunge na madiwani waliopo madarakani kabla ya muda atashughulikiwa.
"Hatukatazi kuwa na nia ya kugombea ubunge na udiwani, kwa sasa kaa nayo moyoni mpaka muda sahihi utakapofika utachukua fomu na kuomba ridhaa, ila kwa sasa tukikubaini tutakushughulikia," amesema Gavu.
Gavu ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM, amesema nafasi ambazo zimeshajazwa ni ya mgombea urais Tanzania bara na Zanzibar, nyingine zote zipo wazi.
Soma, Pia: CCM Iringa: Watiania wanaojipitisha majimboni kabla ya muda waambieni tutawafyeka
Akizungumza katika uzinduzi wa ofisi ya CCM Wilaya ya Newala mkoani Mtwara Machi 1, 2025, Katibu wa Organizesheni wa chama hicho, Issa Ussi Gavu amesema atakayebainika kusumbua ufanyaji kazi wa wabunge na madiwani waliopo madarakani kabla ya muda atashughulikiwa.
"Hatukatazi kuwa na nia ya kugombea ubunge na udiwani, kwa sasa kaa nayo moyoni mpaka muda sahihi utakapofika utachukua fomu na kuomba ridhaa, ila kwa sasa tukikubaini tutakushughulikia," amesema Gavu.
Gavu ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM, amesema nafasi ambazo zimeshajazwa ni ya mgombea urais Tanzania bara na Zanzibar, nyingine zote zipo wazi.
Soma, Pia: CCM Iringa: Watiania wanaojipitisha majimboni kabla ya muda waambieni tutawafyeka