CCM kwa hili la mchakato wa katiba mmekosea na naamini mnalijua na mnakosa la kufanya

CCM kwa hili la mchakato wa katiba mmekosea na naamini mnalijua na mnakosa la kufanya

mayoscissors

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2009
Posts
975
Reaction score
478
Hainiingii akilini wanaccm bungeni kukataa ukweli usiopingika,huu mchakato hauna mashiko na wanachi wa kawaida tumeshalijua na sasa wajipange kwani hatuko tayari kwa hili na linaongeza nguvu kwa upinzani kwani siku zote wanatumia wanatuelimisha na ndo maana tunawaamini.
Kwa sasa majukwaa rasmi yazidishe kasi ya kutuelimisha ili tupambane na mwovu ccm
 
Wana jf habarini, kwa suala la ubaguzi wa wazi uliofanywa na Tume ya mabadiliko ya katiba kwenye muundo wa mabaraza ya katiba hasa kwa bara, kwa kuruhusu kikundi cha watu wachache kiitwacho WDC, KUMEFANYA mabaraza ya katiba kwa bara kuwa ya chama kimoja, ilihali ni ya vyama vyote, wabunge wa tanganyika(tanzania bara ) hawajatutendea haki katika hili kwa kutoungana na mh. Lissu ili kuwapa uwanja mpana zaidi wananchi wa bara kwa kutumia direct democracy katika kupata wajumbe wa mabaraza ya katiba ya wilaya! Je watanganyika tutaendelea kuburuzwa na wazanzibar mpaka lini??. Nalaani sana kwa kitendo cha wabunge wa Tanzania bara kutokuwa wazalendo kwa tanganyika yetu! Je wengine mnasema? Binafsi nampongeza lissu kwa kuipenda zaidi tanganyika yetu! Pia hongereni wananchi wa singida mashariki!
 
wabunge wenyewe walio wengi ni wa ccm unategemea wataacha kusapoti mambo yao!
 
Tuachieni Tume ya Warioba haiwahusu nyie si mmejitoa nendeni mkajipange kushawishi wapiga Kura waikatae kwenye Kura ya Maoni kelele za Nini, au mmerudi kimya kimya maana ndo style yenu maana hata Jakaya mlitangaza kutokumtambua na Bungeni mkakataa kusimama alipoingia lakin Mlipoenda ikulu mlisema Mnataka kumuona Rais Kikwete na alipoingia wote mkasimama kwa heshma na Taadhima. Mkirudi kwenye Mchakato waambieni wanachama wenu maana washajitoa wanasubiri kupiga kura za Maruhani!
 
Kwa jinsi hali inavyoendelea maslahi ya nchi hii yatazikwa rasmi kama CCM itaendelea kuishi. Maana kwa ubabe wa wazi wanaofanya ilimradi tu kujihakikishia wanaendelea kutawala iwe isiwe. Wangetutendea haki watanzania kama hiki chama kingevunjwa na mali zake zote zirudi serikalini. Vipande vya makundi yao vikajisajili vyama vipya vya siasa. Hapo hakika tutasonga mbele.
 
CCM tusipowaangalia watatunyang'anya haki zetu hawa
 
Kura Za kuitoa hazitoshi sasa mnatafuta Plan B, unaambiwa Jeuri ya CCM ni Wanachama na Misingi walioachiwa na waasisi wake. CCM nambari one!
 
Tuachieni Tume ya Warioba haiwahusu nyie si mmejitoa nendeni mkajipange kushawishi wapiga Kura waikatae kwenye Kura ya Maoni kelele za Nini, au mmerudi kimya kimya maana ndo style yenu maana hata Jakaya mlitangaza kutokumtambua na Bungeni mkakataa kusimama alipoingia lakin Mlipoenda ikulu mlisema Mnataka kumuona Rais Kikwete na alipoingia wote mkasimama kwa heshma na Taadhima. Mkirudi kwenye Mchakato waambieni wanachama wenu maana washajitoa wanasubiri kupiga kura za Maruhani!
Hatukujitoa ili tukae kimya. Kuanzia sasa kelele mtindo mmoja!
 
Wana jf habarini, kwa suala la ubaguzi wa wazi uliofanywa na Tume ya mabadiliko ya katiba kwenye muundo wa mabaraza ya katiba hasa kwa bara, kwa kuruhusu kikundi cha watu wachache kiitwacho WDC, KUMEFANYA mabaraza ya katiba kwa bara kuwa ya chama kimoja, ilihali ni ya vyama vyote, wabunge wa tanganyika(tanzania bara ) hawajatutendea haki katika hili kwa kutoungana na mh. Lissu ili kuwapa uwanja mpana zaidi wananchi wa bara kwa kutumia direct democracy katika kupata wajumbe wa mabaraza ya katiba ya wilaya! Je watanganyika tutaendelea kuburuzwa na wazanzibar mpaka lini??. Nalaani sana kwa kitendo cha wabunge wa Tanzania bara kutokuwa wazalendo kwa tanganyika yetu! Je wengine mnasema? Binafsi nampongeza lissu kwa kuipenda zaidi tanganyika yetu! Pia hongereni wananchi wa singida mashariki!
usichanganyi wabunge woteni wabunge wa ccm tu, na spika ndio hawakututendea haki. maana walijifanya hawajui linaloongelewa na Lisu kama walivyokuwa wanajifanya hawajui lililokuwa linatakiwa na wananchi wa Mtwara kuhusu gesi,na spika badala ya kuwapa nafasi wabunge kujadili kwa kina hakaleta ndiooo au hapanaa na ingawa tuliosikiliza sauti za kukubaliana na Lisu zilikuwa nyingi spika akasema anafikiri waliompinga Lisu ndio wengi
 
Back
Top Bottom