CCM kwa muda mrefu sana mmelitia aibu taifa letu, kiasi cha nchi nzima kuonekana tuna changamoto ya afya ya akili

CCM kwa muda mrefu sana mmelitia aibu taifa letu, kiasi cha nchi nzima kuonekana tuna changamoto ya afya ya akili

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
IMG_20250204_092741.jpg

Kwa KWELI CCM imekuwa ikitutia aibu kila uchao mbele ya wageni kutoka nje ya taifa letu na wahisani wetu.

NI aibu sana kwa nchi fukara kama hii, chama tawala kwenda kununua mabasi ya kifahari kwa ajili ya kampeni, wakati wananchi wenu wanafukuzwa Hospitali kwa kukosa gloves za kujifungulia.
FB_IMG_17375278620527460.jpg

NI ukosefu wa uzalendo na matumizi mabaya ya rasilimali FEDHA za walipa kodi kuona utitiri wa misafara ya magari ya Viongozi, wakati hata kwa hao wanaotuhisani Hawana utitiri huo.

IGP wa Polisi ana msafara wa zaidi ya Gari tatu.

Mkuu wa majeshi CDF ana msururu mrefu mno.

Spika wa bunge naye ana msafara wake mrefu.

Nabii waziri mkuu naye ana msafara mrefu.

Haya ni matumizi mabaya ya rasilimali.

Uingereza tumeona mara nyingi msafara wa waziri mkuu ni Gari tatu mpaka nne tu.

Leo Tanzania chini ya CCM msafara wa rais una Gari zaidi ya hamsini.

Hivi hawa wanaotuhisani wanatuonaje? Wanatufikiriaje lakini? Je wanatuona tuna fikra sahihi?

CCM ya leo haitaki tena kusikia sera za kujitegemea. Mama anaamini kwamba nchi itaendeshwa kwa yeye kusafiri sana nje.

Sasa wahisani wameanza kukata misaada, je tumejipangaje kama taifa chini ya utawala wa CCM?

Viongozi wa serikali hii ya CCM wapunguze matumizi yasiyo ya lazima, ni aibu sana kwa wabunge kufanya mashindano ya kula.

Nini faida ya shindano kama hili? Huku ni kutukanisha Watanzania.
 
Nyerere alisema, ili nchi iendelee, inahitaji Watu, Ardhi, Uongozi Bora na Siasa Safi.

CCM wamekosa watu wenye sifa za kuliletea taifa maendeleo, ndio maana hamna uongozi Bora wala siasa safi, tunapora ardhi za wazawa na kuwagawia wageni. Hii ni laana
Hivi ukikaa kwa kutulia unaona upo mwaka mtapokea kijiti? Mnajidanganya
 
Ukweli uliowazi kabisa, FISIEM wametufikisha hapa tulipo, hayo wanayoita maendeleo, ukilinganisha na muda ambao toka tupate uhuru utaona ni jambo la kijinga kujisifia tumeendelea.
 
Nyerere alisema, ili nchi iendelee, inahitaji Watu, Ardhi, Uongozi Bora na Siasa Safi.

CCM wamekosa watu wenye sifa za kuliletea taifa maendeleo, ndio maana hamna uongozi Bora wala siasa safi, tunapora ardhi za wazawa na kuwagawia wageni. Hii ni laana
Hapo kwenye uongozi bora naona alianza kufeli yeye mapeema tu, ishu ya kukipa chama nguvu kubwa haya ndiyo madhara yake sasa chama kinamiliki kila kitu kuanzia vyombo vya sheria mpaka akili za wafuasi wao.
 
Hapo kwenye uongozi bora naona alianza kufeli yeye mapeema tu, ishu ya kukipa chama nguvu kubwa haya ndiyo madhara yake sasa chama kinamiliki kila kitu kuanzia vyombo vya sheria mpaka akili za wafuasi wao.
Alifeli big time. Hata muungano na Zanzibar, ni kufeli, Mwenge wa uhuru ni kufeli, harakati za ukombozi kusini mwa Afrika ni kufeli zaidi.
 
Back
Top Bottom