Pre GE2025 CCM: Maneno ya M/Kiti wa Baraza la Wazee CHADEMA ni ya Viongozi wa CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Katibu wa Itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa Amos Makalla ameeleza hayo wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa CCM Wilaya ya Kinondoni amesema

Namnukuu

"Lakini mimi ninataka niseme upandacho ndicho uvunacho, Mzee Hashim Issa hajatamka kimakosa, ametamka yale maneno, ni kauli za viongozi wakuu wa CHADEMA wenyewe, wamekuwa wakipinga muungano, wamekuwa wakieneza udini, wamekuwa ni chama cha ukanda. Kwahiyo Mzee Hashim amesema yale ambayo Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Freeman Mbowe) aliwahi kuyatamka, Tundu Lissu (Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA bara) aliwahi kuyatamka, na yeye anatekeleza kauli ya viongozi wake Wakuu"
Pia soma
Your browser is not able to display this video.
 
Na maneno ya mkuu wa mkoa nayo ni ya CCM..!!
 
..Makala ataondolewa hapo muda si mrefu.

..kama Mwenezi wa Ccm Makala anafanya makosa kushambulia Waislamu, wakati Mwenyekiti wa Ccm Mama Samia ni Muislamu.
 
Mheshimiwa Mwenezi wetu CPA Amos Gabriel Makala kaongea UKWELI Mtupu.Ndio maana tunaendelea kusisitiza kuwa CHADEMA ni lazima iogopwe kama ukoma.na kupingwa na kila mtanzania mwenye akili Timamu na anayejitambua.
 
..Makala ataondolewa hapo muda si mrefu.

..kama Mwenezi wa Ccm Makala anafanya makosa kushambulia Waislamu, wakati Mwenyekiti wa Ccm Mama Samia ni Muislamu.
Si unaona unavyoonyesha ujinga wako wa Udini? Hivi kwanini wewe na chama chako mnapenda sana Udini? Ndio maana watanzania wanaendelea kuiamini na kuiunga mkono CCM tu.
 
Reactions: Tui
Hii nafasi inampwelepweta Makalla
 
Kwahiyo na anayeua ni yule anayejinasibu kuwa hajawahi kuua hata sisimizi!
 
Alishaomba msamaha kwamba aliteleza. Mengine ni umbea na unafiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…