CCM Mnatupekeka Wapi Kiuchumi?

CCM Mnatupekeka Wapi Kiuchumi?

Bowie

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2016
Posts
4,373
Reaction score
6,084
Toka tupate Uhuru 1961 Tanzania imetawaliwa na Tanu na baadaye CCM lakini cha kusikitisha ni jinsi ya uchumi wa Tanzania unavyoendeshwa kwa njia tofauti katika utawala wote wa awamu sita.

Awamu ya kwanza njia zote za kiuchumi zilithibitiwa na serikali na utaifishaji mkubwa wa majumba/mashamba/biashara kubwa ulifanyika. Ilianzishwa mashirika ya serikali kama RTC, National Milling, Kabimita etc . Sera hiyo ya kiuchumi ilishindwa kabisa.

Awamu ya pili ilikuwa ni awamu ya ruksa ambapo serikali ilijitoa katika masuala ya kufanya biashara na biashara ikawa huria lakini ukusanyaji wa kodi ulikuwa mbovu sana.

Awamu ya tatu ilikuja na sera ya ubinafishaji ambapo tuliona mabenki na viwanda vikibinafishwa kwa bei chee na mfumo wa biashara huria uliendelea.

Awamu 4 Ulikuja na mikakati ya njia mbadala wa kutumia Gesi kama uzalishaji wa umeme na mabilioni ya fedha yalikopwa ili kujenga bomba la gesi kutoka kusini mpaka Dar. Mradi wa kujengwa bandari ya Bagamoyo ulianzishwa.

Awamu ya 5 Ulingia madarakani na kuacha mradi wa umeme wa gesi na kuamua kuingia kwenye mradi mkubwa wa umeme kwa kutumia maji.

Stiegler's Gorge project na mpaka sasa haujakamilika. Mradi wa treni wa standard gauge ulianzishwa pia. Sekta binafsi zilikuwa na wakati mgumu sana kipindi cha awamu hiki kwa kubandikiwa kodi na hii ilipelekea biashara nyingi kufungwa na wawekezaji kukimbia. Mradi wa kujenga Bandari ya Bagamoyo ulisitishwa.

Awamu ya sita Sekta binafsi imepata afueni na wawekezaji wameanza kurudi na mradi wa Ujenzi wa bandari ya Bagamoyo umeanza kuzungumzua upya.

Kwanini CCM isiweke Road Map kwenye masuala ya uchumi wa Tanzania ili kila awamu ifuate sera moja katika kujenga uchumi. Hii itasaidie wafanyabiashara na wawekezaji kuwa na imani serikali yeyote ya CCM katika kufanya biashara Tanzania
 
Kwanini CCM isiweke Road Map kwenye masuala ya uchumi wa Tanzania ili kila awamu ifuate sera moja katika kujenga uchumi. Hii itasaidie wafanyabiashara na wawekezaji kuwa na imani serikali yeyote ya CCM katika kufanya biashara Tanzania
Road Map yao ni namna ya kuiba chaguzi nzima nzima kwa kutumia Polisi na TISS...hapa SAA hizi wenzio wanawaza chaguzi tu. Nothing else
 
Swali fikirishi je tuna mfumo wetu wa kiuchumi wa Kitaifa ambao wanasiasa hawatakiwi kuuchezea? . Do we have, a National economic structure, that can not be tempered by any regime?

What we need is a National economy and social development strategy of an existing government and National Economic structure of the Nation
 
Swali fikirishi je tuna mfumo wetu wa kiuchumi wa Kitaifa ambao wanasiasa hawatakiwi kuuchezea? . Do we have, a National economic structure, that can not be tempered by any regime,? .What we need is a National economy and social development strategy of an existing government and National Economic structure of the Nation
Majirani zetu Kenya toka wapate uhuru zimepita awamu tatu lakini sera zao za kiuchumi hazijabadilika
 
Uchumi umeanguka ...Kipato Cha wananchi kimeshuka.. biashara zimedorora kwa Sababu purchasing power imepungua.

Tuna Vivutio vya utalii vingi, vizuri sana...Tumekwama kuvutia watalii. South Africa wanayo million 10 tourists na zaidi, Morocco...wanayo beach peke yake.

TANAPA na Ngorongoro au Waziri wa utalii wanakiuka Mpango wa ILANI YA UCHAGUZI YA CCM.

Wanashindwa kutangaza utalii, na wanakwaza biashara ya utalii.

Waziri wa utalii akijipanga vizuri, Kila mkoa utoe Vivutio vyake, biashara ya utalii itaongeza ajira million 8 na zaidi ...ILANI YA UCHAGUZI YA CCM
 
CCM wamegota, fikra zimefika mwisho!
Wamebaki na bunduki na risasi tu, lakini hawana mission zozote tangible za kutuinua isipokuwa kuendelea kututia umasikini tu
CCM ina makundi 2 yanayopingana ..Janjaweed ya Sukuma Gang na Ccm masilahi ya akina Jk, etall
 
Bora hata Magufuli alikuwa anaeleweka na anatupeleka shimoni, huyu wa sasa na watu wake hata haijulikana mikakati yao ya muda mrefu ni ipi

Mara waseme wanaanzisha tozo za simu ili zitumike kuboresha huduma za kijamii wakati huo huo wanaenda kukopa fedha kwa wazungu kwa shughuli zilezile ambazo walisema tutatumia fedha zinazotokana na tozo

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Majirani zetu Kenya toka wapate uhuru zimepita awamu tatu lakini sera zao za kiuchumi hazijabadilika
CCM ,imeua biashara,asilimia 80% ya mafanikio kwenye bi ashara yoyote ile yanamtegemea mjasiriamali ,asilimia 20% ni yatakayo/yanayo mzunguka( the entrepreneur and his environments) kwenye hiyo asilimia 20 ,kuna utashi wa kisiasa,mfumo jumuishi wa maisha ya MTU mmoja mmoja na mengine ambayo yako nje la kusudio la binadamu( politics,social demographic variables and physical factors)
 
Uchumi umeanguka ...Kipato Cha wananchi kimeshuka.. biashara zimedorora kwa Sababu purchasing power imepungua.

Tuna Vivutio vya utalii vingi, vizuri sana...Tumekwama kuvutia watalii. South Africa wanayo million 10 tourists na zaidi, Morocco...wanayo beach peke yake...
Mimi ni mtaalamu wa elimu ya ujasiriamali ,kilichoua biashashara awamu ya 5 siyo mitaji wala ukosefu wa elimu ya ujasiriamali ,ni Sera ambazo hazina tija na Unyumbu (uncertainty policies and herding behaviour) .

Unyumbu nipale watu wachache tuliowapa dhamana wanapojitoa ufahamu (an occurrence of thoughtful people suspending their individual reasoning because of self-Absorbed group or fearing their leaders
 
20210809_145036_temp.jpg
 
Toka tupate Uhuru 1961 Tanzania imetawaliwa na Tanu na baadaye CCM lakini cha kusikitisha ni jinsi ya uchumi wa Tanzania unavyoendeshwa kwa njia tofauti katika utawala wote wa awamu sita...
Mengine yapo njee ya uwezo wao.Wasamehe TU Bure, ila tuitake katiba mpya na tuwatake wasiwe kikwazo Cha upatikanaji wake.
 
Mimi ni mtaalamu wa elimu ya ujasiriamali ,kilichoua biashashara awamu ya 5 siyo mitaji wala ukosefu wa elimu ya ujasiriamali ,ni Sera ambazo hazina tija na Unyumbu (uncertainty policies and herding behaviour) .

Unyumbu nipale watu wachache tuliowapa dhamana wanapojitoa ufahamu (an occurrence of thoughtful people suspending their individual reasoning because of self-Absorbed group or fearing their leaders
Example is Minister of Finance and another of Agriculture
 
Back
Top Bottom