CCM na tozo ni ile ya "tema tumpige" ya mama na mwana

CCM na tozo ni ile ya "tema tumpige" ya mama na mwana

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Watoto wadogo wanapolia kwa kuchokozwa na mtu mzima au hata kwa kuchomwa sindano, ili kumnyamazisha asilie mzazi atamuuliza mtoto swali la kizushi la "nani mchokozi?". Mtoto atasema yule pale, na mzazi atamwambie tema tumpige, na mzazi atampiga kizushi huyo mchokozi, na mtoto atanyamaza kwa kuamini yule mchokozi wake amekiona cha mtema kuni.

CCM inatuchezea shere kwenye mambo mengi sana na kutufanyia ileile ya tema tumpige kama watoto. Mwenyekiti wa CCM ndiye Mkuu wa nchi na mkuu wa serikali, mawaziri wote na 99% ya wabunge wote ni CCM. Hakuna mswada wala sheria itapitishwa bila CCM kufahamu na kushirikishwa kupitia Mwenyekiti wa CCM, mawaziri, na wabunge wa CCM.

Mfano, haiwezekani kusikia eti CCM haina habari na tozo kwa wananchi. CCM inataka kujitenga na malalamiko ya tozo kana kwamba haifahamu kilichofanyika na kinachofanyika kwa kuikemea seikali wakati mwenyekiti, mawaziri na wabunge wa CCM ndio waliopitisha tozo hizo, sheria na kanuni zote nchini tangu nchi ipate uhuru.

Binafsi ninajisikia kichefuchefu ninapowaona akina Kinana na Shaka wanazunguuka huku na huko wakifanya "tema tumpige" kwa wananchi mazuzu. Wanajifanya wanaishangaa serikali yao mbele ya wananchi kama vile walikuwa wamesafiri wakati serikali na bunge wakipitisha sheria na kanuni mbalimbali zinazowaumiza wananchi. Wanajifanya wanaikemea kizushi serikali yao ili kuwanyamazisha wananchi wanaolalamika dhidi ya sera za CCM zinazotekelezwa na serikali zao, yaani TEMA TUMPIGE.



 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ukweli mchungu ni kuwa sisi watanzania ni wajinga,waoga na legelege tusioweza hata kudai haki zetu za msingi.

Mfano watumishi wote ambao mishahara inapitia bank,umeshakatwa PAYE,hizo tozo za miamala ya bank za nini.

Hii double taxation ya nini kama si kukomoana na roho mbaya? Vyama vya wafanyakazi ni kama havipo, hakuna kauli wala juhudi za kupinga unyonyaji huu.

Na sie tunaenda kazini kama kawaida.

Trade unions, anzisheni basi hata harakati za mgomo!
 
Watoto wadogo wanapolia kwa kuchokozwa na mtu mzima au hata kwa kuchomwa sindano, ili kumnyamazisha asilie mzazi atamuuliza mtoto swali la kizushi la "nani mchokozi?"...
Tema mate tumpige. !!😅
 
Watoto wadogo wanapolia kwa kuchokozwa na mtu mzima au hata kwa kuchomwa sindano, ili kumnyamazisha asilie mzazi atamuuliza mtoto swali la kizushi la "nani mchokozi?". Mtoto atasema yule pale, na mzazi atamwambie tema tumpige, na mzazi atampiga kizushi huyo mchokozi, na mtoto atanyamaza kwa kuamini yule mchokozi wake amekiona cha mtema kuni.

CCM inatuchezea shere kwenye mambo mengi sana na kutufanyia ileile ya tema tumpige kama watoto. Mwenyekiti wa CCM ndiye Mkuu wa nchi na mkuu wa serikali, mawaziri wote na 99% ya wabunge wote ni CCM. Hakuna mswada wala sheria itapitishwa bila CCM kufahamu na kushirikishwa kupitia Mwenyekiti wa CCM, mawaziri, na wabunge wa CCM.

Mfano, haiwezekani kusikia eti CCM haina habari na tozo kwa wananchi. CCM inataka kujitenga na malalamiko ya tozo kana kwamba haifahamu kilichofanyika na kinachofanyika kwa kuikemea seikali wakati mwenyekiti, mawaziri na wabunge wa CCM ndio waliopitisha tozo hizo, sheria na kanuni zote nchini tangu nchi ipate uhuru.

Binafsi ninajisikia kichefuchefu ninapowaona akina Kinana na Shaka wanazunguuka huku na huko wakifanya "tema tumpige" kwa wananchi mazuzu. Wanajifanya wanaishangaa serikali yao mbele ya wananchi kama vile walikuwa wamesafiri wakati serikali na bunge wakipitisha sheria na kanuni mbalimbali zinazowaumiza wananchi. Wanajifanya wanaikemea kizushi serikali yao ili kuwanyamazisha wananchi wanaolalamika dhidi ya sera za CCM zinazotekelezwa na serikali zao, yaani TEMA TUMPIGE.



Mhhh, ccm buana yaani..au Basi.
 
Na unaweza kukuta kuna watu wanaamini huo utapeli wa CCM!
 
Na unaweza kukuta kuna watu wanaamini huo utapeli wa CCM!
Haiingii akilini Kinana aikosoe serikali ambayo mkuu wa serikali hiyo ni mwenyekiti wake wa CCM. Wanatufanya mataahila, Kinana anataka kuwaamina wajinga kuwa hivyo vitendo vya serikali vinavyowaudhi wapiga kura havikubaliki na sio mali wala sehemu ya CCM.
 
Upo sahihi kabisa mkuu! Hii ni janja janja tunachezeahewa..
 
Ukweli mchungu ni kuwa sisi watanzania ni wajinga,waoga na legelege tusioweza hata kudai haki zetu za msingi.

Wewe peke yako. Usituingize Watanzania wengine kwenye lege lege zako.
Mfano watumishi wote ambao mishahara inapitia bank,umeshakatwa PAYE,hizo tozo za miamala ya bank za nini.

Hii double taxation ya nini kama si kukomoana na roho mbaya? Vyama vya wafanyakazi ni kama havipo, hakuna kauli wala juhudi za kupinga unyonyaji huu.

Na sie tunaenda kazini kama kawaida.

Trade unions, anzisheni basi hata harakati za mgomo!
Kuna lugha nyingine hata kama huna akili, una davua Ujinga. Ukimbari. na Matusi kwa WATANZANIA.

Ingefaa wakupige tozo za uropokaji
 
Wewe peke yako. Usituingize Watanzania wengine kwenye lege lege zako.

Kuna lugha nyingine hata kama huna akili, una davua Ujinga. Ukimbari. na Matusi kwa WATANZANIA.

Ingefaa wakupige tozo za uropokaji
Pole aisee,siku yako leo ilikuwa mbaya
 
Wengi ni keyboard worriors, wanaongea wamejificha ukiwaambia nenda front wwtakuacha pekeako muulize Mange Kimambi.
 
Pole aisee,siku yako leo ilikuwa mbaya
Unalazimisha kweli!
Ni kweli, nasikitika Tozo, nasikitika kifo cha Malikia na nawasikitikia Wananchi wa Commonwealth.

Umepatia, langu.
Umekosa, la Watanzania.
 
Tema mate tumpige. !!😅
Binafsi ni muumini wa kulipa kodi, lakini napenda nikishalipa Kodi huduma kwangu zisiwe za kupapasa.
Kumba kuwa pamoja na Kodi na tozo hizi za serikali zipo Kodi nyingine ambazo zinamuandama mwananchi kama vile:
1. Serikali ya mtaa Kuna kodi tena ya kuzoa taka na ulinzi wa sungusungu
2. Serikali ya jamii, ziko Kodi za kuchangia misiba, harusi na kipaimara.
3. Serikali ya familia, ziko Kodi za ada za watoto, chakula, nauli na hela ya shule,
4. Serikali binafsi, ziko Kodi za chakula, malazi, mavazi, nauli, huduma za choo cha kulipia kila pahala kwenye mkusanyiko.

Serikali kuu inasahau kuwa mwananchi anazo Kodi nyingi nyingine. Kwanini mtu alipe Kodi na tozo halafu alipe tena ulinzi wa sungusungu? CCM hailifahamu hata hili linaloonhizwa na wajumbe wake wa nyumba 10?
 
Mshahara wangu nimeshalipa Kodi PAYE, kilichobaki nikaoekekewa benki, kufika huko benki nayo ikanikata fedha wakati ninauchukua kutoka kwenye akaunti yangu, baada ya hapo serikali tena kama vile haikutosheka ikaukata tena tozo wakati ninautoa Kwenye account yangu. Yaani serikali imeuandama mshahara wangu mara tatu; PAYE, makato ya Benki na tozo. Huu ni wizi Ndugu zangu. Eti msomi anatuambia namna tozo hizo hizo zinavyojenga madarasa na zahanati lakini hasemi fedha kutoka bandarini madini na utalii zinafanya nini na nini. Yaani anatuona sisi mazuzu hatujui kitu. Wamelewa madaraka kupitiliza.
 
Back
Top Bottom