Elections 2010 CCM ni CHAMA cha KIMATAIFA ==SMS

WAPENDWA WAPAMBANAJI,
DOKEZO: Hakuna lolote, SMS za wafu na wanaokimbiana wenyewe hao. Zile walizosema zilitoka nje ya nchi ni feki, zimetokea hapo Upanga (nahisi Mtaa wa Undali), wamewachukua vijana kadhaa wa Magabachori-wasanii wenzao kutumia utaalam mdogo tu kupitia Skype Free services (Hii inaruhusu kutumia route ya nchi yoyote kupiga simu au SMS na unaonekana kama upo ktk ile nchi kumbe sio). Usanii mtupu wa kifisadi na wizi. Wametumia Synovate, REDET na hatimaye wanaweza kuingilia mahakama kufanya wao hukumu kwa niaba ya yule jamaa Mume ***** waliyempangishia hoteli na mkoko kapewa kwa ajili ya kufanikisha ile kesi feki ya 'kuibiwa mke' kumbe ndi CCM wanaiendesha. Hawatasita kutoa hukumu musa si mrefu kupitia mahakama zetu hizi zilikataa hata mgombea binafsi kuinusuru CCM...
Na Bado SAA YA KUFA NYANI MITI YOTE HUTELEZA...! OKTOBA 31 ndio SMS zitawapa majibu sahihi kuwa ndiyo Laana yao. Na hakuna kuibiwa hata Kura 1, Dr Slaa anaiongoza Tanzania, huru na iliyojaa Amani tele, hakuna hata tone la damu kumwagika. PEOPLE'S POWER! YES WE CAN CHANGE ALL THESE AWKWARD LIFE created by CCM culprits.
 
Admin, naona kama umeiondoa comment nilitopost few minutes ago. May I know what was wrong with it au someone is blackmailing through your route!!
 
Sorry, it is back now! I meant comment No 21 above, was missing in the list, but it is back again! JF team thanks..!
 
Kwa kweli Kwa sisi wana CCM safi na ambao tunapinga rushwa na mafisadi walioko ndani ya chama chetu eg EL & RA.

Tunapatwa na wakati mgumu huko mitaaaani kusema jamani CCM tuchagueni na inakupasa uwe na Roho ngumu kama ya mwenda wazimu hivi ili kukitetea chama changu kwani wengi wa vijana wenzangu wanasupport upinzani na hii yote ni kuwa na viongozi wabovu ndani ya CCM wasio fuata maadili ya uongozi na miiko ya uongozi na wasiokuwa wazalendo. Na nitasimama kidete kuwaondoa mafisadi tuu(i mean wachafu wote) ndani ya (UVCCM/UWT maana huku kuna sumu mbaya imeisha mwagwa na vijana wamegeuka kuwasupport mafisadi siju ni njaa) then CCM in general.

Kwani pia kuna viongozi walio bora na safi wanaweza kukiongoza chama na serikali ila siju hili kundi la wana mtandao lilikotoka na rahana za wapi huko kuja kuchafua hali ya hewa ndani ya CCM
 
CCM ya enzi za uhuru ni completely different na CCM ya sasa..hawana hata chembe ya haya kutumia sifa hizi??!!
 
.....kila jambo na wakati wake!!! wakati ule movement kubwa ilikuwa ukombozi wa nchi za afrika na kwa vile nyerere (RIP) alikuwa mwana afrika halisi alikuwa mbele katika harakati zile. nasema mbele kwa maana alikuwa mwenyekiti na nchi zingine zilishiriki pia. kama Tanzania (not CCM) ili-participate kwenye ukombozi wa nchi fulani fulani, then what the issue now? kwa kazi ile tulipoteza rasilimali zetu, sasa tunataka recovery ambayo nyie manyang'au mmeshindwa!!! kufanya jambo fulani jema in the past sio justification ya kuboronga na kuendelea kuboronga sasa! na in reality, that was person view and efforts za Nyerere..thubutu CCM ya sasa (ya Makamba, Kikwete, Kinana) kama wataweza!!!
 
SMS haina namba simu inaandika CCM basi (no number!!!!!) Inawezekana ni kwa msaada wa TCRA na hii ni baada ya kutumia namba ya nje wakapigiwa kelele.

Na mimi NIMEPATA LEO ASUBUHI the same msg "CCM"
 
Kumbe nilidhani nimekosea kusoma hiyo taito, mi niliisoma hivi.."CCM ni Chama cha kimafia" nadhani sijui lakini kwamba ndio sahihi
huja kosea, mbaya zaidi wana tumia mali za watanzania kutufanyia umafia wao mfano jana niliona gari inayo tumika tuliza ghasia hilo hapo chini likizungukazungu mjini Arusha, watu wakawa wanajiuliza ndiyo tuna tishwa au walikuwa na malengo gani hasani..
 
Wasilo lijua CCM ni kuwa vitisho vingi ndivyo vitakavyo wapa watu ujasiri baadae.
 

Kuna taarifa kwamba, ujumbe huo unatumwa na chadema ili kupunguza nguvu za CCM.
 

ZENJ BARY: Haya ndio maisha yetu? je unasemaje utanipa kura yako?
 
Hatudanganyikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
Kama ni cha kimataifa kwa UFISADI ndiyo, ni cha kimataifa. na Mkuu wao ni JK na vinara wake anaowakumbatia na kuwapigia debe waendelee kuwadhulumu wananchi.
 
yaani sasa hivi wanaweweseka tu .walitegemea vijijini ndokwenye kura nako hawataki hata kuwasikia

Umefanya utafiti wa kina? kama umefanya basi ukweli ni kwamba CCM imejiimarisha sana katika maeneo ya vijijini na inauhakika wa kupata kura nyingi kutoka katika maeneo hayo.Vyama vya upinzani vilijisahau kujiimarisha ktk maeneo ya vijijini na kwa sababu hiyo haviwezi kushinda katika uchaguzi huu wa 2010
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…