CCM ni chama hatari sana,kinaweza kulitia doa baya sana taifa letu. Huu ndio ukweli wenyewe

CCM ni chama hatari sana,kinaweza kulitia doa baya sana taifa letu. Huu ndio ukweli wenyewe

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
Haiwezeki na haiingii akilini kwenye heka heka za Chaguzi karibia zote za marudio zinazoendelea nchini kila kata wagombea udiwani wa CCM wanapita bila kupingwa, kwani Upinzani wameanza kugombea leo? Mwanzo walikua wanafanyaje?
Watu wanaporwa form mchana kweupe na wasimamizi wa uchaguzi wanatazama, watu wanatishwa na wasimamizi wa uchaguzi wanatazama. Mbona miaka ya nyuma hali hii ya hovyo kabisa haikuwepo, kwanini ni sasa? Hivi hawa watu wanalitaka nini taifa?

Ifikapo kuanzia 2019 kwenye uchaguzi za serikali za mitaa hali inaweza kua tete kuliko ilivyowahi kutokea tangu nchi ipate Uhuru, CCM wanataka kulazimisha mambo kwanini?Hatima ya kutumia nguvu na kunyanyasa watu ni ipi? Tunataka kuelekea wapi?

Binafsi napenda tu niwashauri CCM kua hali ikiwa tete wao ndio watajibu na watakua chama cha kwanza kukimbiwa na watu na kufa kabisa, baadae watajibia haya. Wasione fahari watu kufanyiwa haya, wafurahie katiba iliyopo lakini watambue kua katiba hii hii ambayo hawataki mabadiliko yake ndiyo baadae itageuka kua shimo lao.

Najiuliza, je, upinzani nao wakiamua kusema na sisi hatutaki hali itakuwaje? Hivi CCM wanadhani upinzani wanamuogopa mtu au ni uvumilivu tu ambao unatumiwa na viongozi wao wa juu? Tunafikiri huu uvumilivu wa kina Mbowe,Zitto na wengine hautakua na mwisho? Ikifika mahali nao wakiwaambia wafuasi wao sasa inatosha itakuwaje?

Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama itafika mahali vitasimama katika haki, itafika mahali vitajali raia wao kwa misingi ya katiba ya nchi, watazingatia yale yatakayolinda utulivu wetu. CCM wasifikirie hivi vyombo ni vyao kwa Mtazamo wa Hussein Bashe,hivi vyombo ni vya umma kama ilivyo wao pia wana ndugu walioko upinzani.

Haiwezekani kusema eti Kiongozi flani anafanya mambo makubwa eti ipelekee wagombea wa CCM wapite bila kupingwa, kwani Upinzani wameanza kushiriki uchaguzi leo kiasi kwamba wawe ni watu wa kukosea tuu?Ipo shida kubwa sana tuu, trust me wallah muda utanena.
 
Nchi yoyote inayoongozwa na dikteta mifumo ya kisheria huwa haifanyi kazi kwa mujibu wa majukumu yake
 
Unapelekaje mtu asiejua kusoma nankuandika halaf awe duwani? Jiulizen mnakosea wap sio kulalamika,mlalamishi yyte ana laana,nakuhakikishia tu msipobadilika na kusimamia mnachokiamin mtanyooshwa sana na sisiem hii ya Magu.. Unapoambiwa kwamba tukimaliza uchaguz tunajipanga kwa uchaguz ujao hua hamwelewi ila nakuakbia tu sisiem inapomaliza uchaguz wwte inajipanga miaka mitano mbele,nyie mnabaki kulalamika wao wanapiga hatua,

Mliutangazia umma wa watanzania kwamba hamtashiriki uchaguz wwte mpk mmsikilizwe mnachokitaka,jumuia ya kimataifa haiwez kuwasikiliza kwa sana km mnashindwa kushikilia msimamo wenu,mnatangaza leo hatutashiriki kesho mnapeleka watu,ukiamua kugoma bas kazia hapo hapo,chaguz yyte uwe mkubwa au mdogo..na kukukumbusha sisiem ni ngumu sana kuishinda ktk uchaguz wa marudio,itatokea mia kwa wawil lakin itawagalagaza tu... Simamien mnachokiamin sio kuwa ndumilakuwili leo mnagoma kesho mnaingiza timu,kuwen kama Yanga walikataa kagame na wakashikilia msimamo wao mwanzo mwisho. Watanzania wanawadharau sbu labda hamjui mnachotaka na kwa wakat upi
 
Time will tell...

Jimbo, kata, tarafa, kitongoji kinachoongozwa na upinzani maendelea huchelewesha kwa kusudi na hila...


Cc: mahondaw
 
Duuu!! aisee jipangeni upya kuweni na msimamo sio ndimi mbilimbili...mkisusa suseni kweli watanzania sio wajinga kiasi hicho!!
 
Kuna vyama kama KANU siku ikipatikana dawa nahis na Kinga itatengenezwa hutosikia tena gonjwa hilo
 
Unapelekaje mtu asiejua kusoma nankuandika halaf awe duwani? Jiulizen mnakosea wap sio kulalamika,mlalamishi yyte ana laana,nakuhakikishia tu msipobadilika na kusimamia mnachokiamin mtanyooshwa sana na sisiem hii ya Magu.. Unapoambiwa kwamba tukimaliza uchaguz tunajipanga kwa uchaguz ujao hua hamwelewi ila nakuakbia tu sisiem inapomaliza uchaguz wwte inajipanga miaka mitano mbele,nyie mnabaki kulalamika wao wanapiga hatua,

Mliutangazia umma wa watanzania kwamba hamtashiriki uchaguz wwte mpk mmsikilizwe mnachokitaka,jumuia ya kimataifa haiwez kuwasikiliza kwa sana km mnashindwa kushikilia msimamo wenu,mnatangaza leo hatutashiriki kesho mnapeleka watu,ukiamua kugoma bas kazia hapo hapo,chaguz yyte uwe mkubwa au mdogo..na kukukumbusha sisiem ni ngumu sana kuishinda ktk uchaguz wa marudio,itatokea mia kwa wawil lakin itawagalagaza tu... Simamien mnachokiamin sio kuwa ndumilakuwili leo mnagoma kesho mnaingiza timu,kuwen kama Yanga walikataa kagame na wakashikilia msimamo wao mwanzo mwisho. Watanzania wanawadharau sbu labda hamjui mnachotaka na kwa wakat upi
Ngoja nikuulize kama una kumbukumbu, suala la vyeti, mbona jiwe alimwambia mama wa madini aseme uongozi hauhitaji shule ili tu panga isimpate bashite, mkadai siasa hazitaki lazma uende shule, leo hii mnakuja ati hawajui kusoma na kuandika, kweli inaingia akilini, bashite wako hata darasa la 7 hajui kamaliza shule ipi na mwaka gani, naungana na mtoa hoja, kwani wapinzani wameanza kuhombea jana huo udiwani, msilazimishwe kupenda mnaweka sheria wenyewe kisha mnakula matapishi yenu wenyewe, kama kukosea haingii akilini ati ccm wote wasikosee, wapinzani ndio wakosee, tunawachora tu, lakini ipo siku ya kwenye mabano tutaamka, suala la muda tu,
 
Back
Top Bottom