kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Wapo watu wanaona wao ndio walizaliwa kuzungumza,kutafakari sahihi na kuamua kwa ajili ya wengine. Wapo watu wameaminishwa kwamba wanaishi hapa Duniani kupumbuza wengine ili wao na familia zao warithishane madara. Zipo familia Leo baba,mama,watoto wanatumia usafiri wa serikali,wanalipiwa nyumba na serikali, wanalipwa posho kwa kifupi zipo familia kwa mwezi zinagharamiwa zaidi ya milioni 50 Hadi 100 na serikali. Si kwamba wana akili au Wana miujiza ila wameamua kututawala na wanatamani familia zao wazidi kututawala.
Familia hizi zilianza miaka 30 nyuma kukabidhiwa nafasi wakaweka ndugu zao. Wamejiwekea utaratibu kwamba wao wataamua hatma yetu Kama Taifa huku wakiamini kuelimika kwetu ndio ukombozi wetu.
Leo hii wamekuwa na kiburi kufikia kutuamulia Ni Nani tumsikilize na Nani tusimsikilize. CCM Leo hii wameamua kutokupambana kwa hoja Bali kupambana kwa kutumia dola. Kama hoja zinajibiwa kwa dola, Ni lini hoja kinzani zitapata majibu. Polisi hawajibu hoja wanazima hoja, CCM wote kwa ujumla nao wameamua kuishi si kuwapambana kwa hoja Bali kwa kuwatuma polisi wakawanyamazishe watoe hoja. Hi si Hali nzuri na tusipoangalia tunatengeneza kizazi Cha kudai haki ambacho kinaweza kuibukia popote na kuyumbisha amani.
Familia hizi zilianza miaka 30 nyuma kukabidhiwa nafasi wakaweka ndugu zao. Wamejiwekea utaratibu kwamba wao wataamua hatma yetu Kama Taifa huku wakiamini kuelimika kwetu ndio ukombozi wetu.
Leo hii wamekuwa na kiburi kufikia kutuamulia Ni Nani tumsikilize na Nani tusimsikilize. CCM Leo hii wameamua kutokupambana kwa hoja Bali kupambana kwa kutumia dola. Kama hoja zinajibiwa kwa dola, Ni lini hoja kinzani zitapata majibu. Polisi hawajibu hoja wanazima hoja, CCM wote kwa ujumla nao wameamua kuishi si kuwapambana kwa hoja Bali kwa kuwatuma polisi wakawanyamazishe watoe hoja. Hi si Hali nzuri na tusipoangalia tunatengeneza kizazi Cha kudai haki ambacho kinaweza kuibukia popote na kuyumbisha amani.