the guardian 17
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 395
- 570
Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma kimewataka wanachama wake kuhakikisha wanazingatia taratibu, Sheria, na kanuni za Uchaguzi wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea wa Ubunge na Udiwani. Lengo ni kuwarudisha madarakani wagombea wanaopendwa na wananchi, lakini kwa kufuata miongozo ya chama na siyo kwa njia ya kupitisha wagombea bila ushindani.
Soma: Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Hayo yamebainishwa na Katibu wa CCM mkoa wa Ruvuma, Mohammed Ally Khalifan, akiwa katika ziara yake ya Siku Nne aliyoanza jana katika jimbo la Mbinga Mjini Katika ziara hiyo, amekutana na wanachama wa CCM katika kata za Kikolo, Kihungu, na Kitanda, ambapo ameweza kuzungumza nao sambamba na kuwapatia mafunzo ya Uchaguzi.
Source: KitengeUpdates
Soma: Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Hayo yamebainishwa na Katibu wa CCM mkoa wa Ruvuma, Mohammed Ally Khalifan, akiwa katika ziara yake ya Siku Nne aliyoanza jana katika jimbo la Mbinga Mjini Katika ziara hiyo, amekutana na wanachama wa CCM katika kata za Kikolo, Kihungu, na Kitanda, ambapo ameweza kuzungumza nao sambamba na kuwapatia mafunzo ya Uchaguzi.
Source: KitengeUpdates