Uchaguzi 2020 CCM si tulisema Magu hahitaji kampeni 2020? Chopa ya nini?

Uchaguzi 2020 CCM si tulisema Magu hahitaji kampeni 2020? Chopa ya nini?

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
CCM tulimpamba mzee sana kuanzia bungeni na nje ya bunge, tukaenda mbali na kusema kuwa hahitaji kampeni 2020 bora hata uchaguzi usifanyike ili apite bila kupingwa, hizi kauli za kinafki ni za kumhujumu mgombea wetu kuanzia leo iwe mwisho. Kama kweli hatukuhitaji kampeni wala uchaguzi huo CHOPA ni ya nini? Gharama zote za Chopa za nini?


Natoa wito kwa wanaccm wote, tuache unafki wa kumpamba mzee wetu wakati tunajua kuwa hali ni ngumu na uwezekano wa kuzidiwa ni mkubwa sana. Tunamdanganya mzee wetu kuwa mambo ni shwari kwa manufaa ya nani? Tukishindwa wa kwanza kupata hasara ni nani kama siyo mimi na wewe?

Kwa bahati mbaya sana chama chetu makao makuu kwenye uongozi timu nzima ya kampeni ni wageni wa siasa za nchi hii, Dr Bashiru na Polepole wameingia kwenye siasa juzi juzi. Hapa ukimtoa mzee Mangula wengine wote waliobaki ni wa kuja watupu na ndio wanaokigharimu chama hawa. Sitaki kuwa mnafki huu ndio ukweli acha niseme tu.

Nipo kwenye timu ya kampeni ndiyo na tunatazamana hapa wacha niseme ukweli mwenye kununa anune, mkiambiwa ukweli mnakua wakali.

1-2.jpeg
1-2.jpeg
3-1.jpeg
 
CCM wanapeleka mrejesho kwa wananchi juu ya kile wachotumwa mwaka 2015. Wanasherehekea mafanikio ndiyo maana sherehe zao zinaambatana na wasanii washereheshaji. Another 5yrs kwa JPM.
 
Makamu wa rais na waziri mkuu hawasikiki kabisa.
Macho na masikio ni kwa JEMBE kwanza. Makamu wa Rais na PM wabomoa kambi za upinzani mikoani kimya kimya, kule Tarime, Bunda na Rolya upinzani hali mbaya, PM anamaliza kazi kimya kimya
 
Yule mkuu wa mkoa wa Dar aliyepita alikuwa anasema katika mkoa wake hataruhusu mheshimiwa rais apige kampeni ni kumchosha,,,,,,,,
🤣 🤣 🤣 alimpeleka chaka sana. Unajua bhana, angekuwa kawaacha wananchi wapige mikutano ya hadhara, wajumuike, wajimwage kwenye magazeti nk, leo tunsingekuwa na la kukosoa kwa sababu kila kitu tungekuwa tushaongea. Kwa sasa ni free ride, kila mtu anaongea analojisikia
 
🤣 🤣 🤣 alimpeleka chaka sana. Unajua bhana, angekuwa kawaacha wananchi wapige mikutano ya hadhara, wajumuike, wajimwage kwenye magazeti nk, leo tunsingekuwa na la kukosoa kwa sababu kila kitu tungekuwa tushaongea. Kwa sasa ni free ride, kila mtu anaongea analojisikia
Alifanya kosa kubwa sana la kiufundi kuzuia mikutano ya kisiasa
 
Duh! Punguzeni hasira wana-CCM wenzangu MAHANJU na GENTAMYCINE . Tukisapoti chama hata Kama mna maoni tofauti. Tujenge chama ili tushinde. Tusiwape faida wapinzani kwa kuanika mambo hadharani. Chama kinatuhitaji kuliko wakati mwingine wowote Sasa.
 
Back
Top Bottom