Uchaguzi 2020 CCM tuwe makini upinzani (CHADEMA) wanaenda kutushangaza Oktoba

Uchaguzi 2020 CCM tuwe makini upinzani (CHADEMA) wanaenda kutushangaza Oktoba

Mshangai

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2008
Posts
468
Reaction score
1,086
Mimi ni mwanaccm asili, sijajiunga Jana au juzi kwa mihemko bali niko hapa kabla hata ya muundo wa vyama vingi.

Ni vizuri kusema ukweli tukielekea uchaguzi mkuu 2020, ile habari ya kutegemea chama chetu kitatumia ujanja na ubabe wa dola tuweke pembeni maana kwa sasa ni hatari kwani tumesha jijengea uadui na jumuia ya kimataifa hivyo madhara yaweza kuwa makubwa.

Nimepita maeneo mengi kuanzia watumishi wa umma wakiwemo polisi na wanajeshi, ukweli wametuchoka sana hata kama wanaimba mapambio kutusifu. Tukumbuke kura ni siri ya mtu.

Wanafunzi na makundi mengine wakiwapo baadhi ya wakulima wa maeneo kadhaa wameshtuka sio wale wa zamani.

Tutaponea wapi? Kukaa na kujidanganya ushirikiano na kina Mbatia au wabunge waliokimbia CHADEMA ambao hawana mvuto ni kujidanganya na kupoteza matumaini.

Ni wakati wa kuacha propaganda za uongo na visa kwa wapinzani, tujikite kurudisha imani kwa wananchi la sivyo uchaguzi wa Oktoba Upinzani hususani Chadema wanaenda kutugaragaza kwa aibu kubwa.

Na kama tutatumia mabavu au wizi wa kura tutegemee viongozi wetu kuishia The Hague kisha jela na chama chetu kusambaratika.

Kwa vijana mihemko wa sasa ndani ya chama chetu wataona hizi ni njozi lakini ndio ukweli maana kifo cha mzee kina mshindo.

Kama viongozi wa sasa wapo ili kukipoteza chama tuwakatae kabisa.
 
Ahsante kwa commedy nzuri.
Ccm ìs there to stay 4ver kama watanzania hawataacha kuendeshwa na matumbo yao badala ya akil.

2020 kwa kishindo mnoo wnapita ccm.
 
Ahsante kwa commedy nzuri.
Ccm ìs there to stay 4ver kama watanzania hawataacha kuendeshwa na matumbo yao badala ya akil.

2020 kwa kishindo mnoo wnapita ccm.
Ndio matamanio yetu wote. Lakini nimeweka angalizo LA kuwa na makini na washindani wetu maana nafasi ya kutumia dola au Tume ni hatari sana kwa chama nyakati hizi.
Tuko kwenye darubini Kali kwenye USO wa kimataifa kuliko wakati mwingine wowote.
 
Namshauri kuepuka mashambulizi, awa-BLOCK, vinginevyo atajuta kuzaliwa na kuja JF!
Hao vijana tumewatumia kuleta amsha amsha kwa chama. Sidhani kama wanaweza kukosa adabu na kuingilia ushauri toka kwetu tulio tumia umri na akili zetu kujenga chama hadi awamu ya tano kukikuta kiko hivi.
Tunapaswa kuwa makini sana, Chadema hawa sio wa kuwachezea kama inavyofikiriwa. Wamekwisha jikita huko waitako msingi.
 
Ahsante kwa commedy nzuri.
Ccm ìs there to stay 4ver kama watanzania hawataacha kuendeshwa na matumbo yao badala ya akil.

2020 kwa kishindo mnoo wnapita ccm.
KiKwete alishawahi kuzikataa kura hizo na akapita kwa kishindo, so hamna jipya hapo.CCM mbele kwa mbele, chadema fanyeni mchakato wa kupata wagombea siyo kuja kutishia nyau JF kwa kura usizo na uhakika
 
2414618_24gvpqh.jpg

Hawa hapa huwa wanatushangaza kila siku wala sio Oktoba!
 
Wew unaota ndoto Chadema hakiwezi kupata hata Mbunge mmoja nipo hapa Same mashariki tumeichoka chadema Kaboyoka hakuna alichokifanya ndani ya miaka mitano Lazima CCM ishinde kwa kishondo kwasababu Raisi MaKUFULI amefanya maendeleo mengi sana kwahiyo kusema chadema itashinda unaota
 
Kama uchaguzi utakuwa Huru na Haki sioni kama Ccm itapata nguvu kubwa kama 2015 japokuwa kwenye siasa kila kitu kinawezekana.
 
Ni kama tu hadi tunafanya uchaguzi hicho chama kitakuwepo ila pia we jamaa umewezaje kufanya tathmini ya nchi nzima juu ya nani anapenda au hakipendi chama fulani? Eti hadi wanajeshi wamekichoka chama, serious! Umeongea nao kabisa wakakuhakikishia hicho kitu? Chadema hamuishiwi sarakasi
 
Back
Top Bottom