Uchaguzi 2020 CCM wagawana kata Arusha, Gambo ushindi saa nne

nyamadoke75

Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
93
Reaction score
288
Wakati Joto la Uchaguzi likizidi kushika kasi hapa nchini, Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Arusha tayari kinadaiwa kupanga safu ya siri ya wagombea udiwani katika kata sita huku Mrisho Gambo akizidi kucheza rafu kuhakikisha nafasi ya Ubunge anashinda mapema asubuhi.

Licha ya kutoanza kinyang'anyiro cha kura za maoni baadhi ya makada wa CCM wanaowania kata hizo wameibua taharuki wakibainisha kwamba iwapo mpango huo utafanikiwa chama hicho kipo katika hatari ya kupoteza kata hizo.

Habari za kuaminika zimedai kwamba mpango huo unaratibiwa na mtaalamu wa fitina, Mrisho Gambo kwa kushirikiana na Mwenyekiti Wa CCM Wilaya, Joseph Massawe, lengo ni kuhakikisha wale wanaowahitaji wanapita ili kumsaidia Gambo katika kinyang'anyiro cha Ubunge baada ya kuahidiwa nafasi ya Uwaziri.

Makada wanaodaiwa kugawiwa kata hizo ni pamoja na Ally Meku (kata ya Kati) Sakina Mpufu(Olorien) Issa (Ungalimited) Abraham Mollel (Kimandolu)pamoja na Mary kisaka ambaye amepewa nafasi ya ubunge wa viti Maalumu.

Hata hivyo Gambo amewaahidi kuwapatia Pikipiki Makatibu wote wa kata na Wenezi wa CCM katika kata zote jijini Arusha iwapo watampa ushirikiano katika nafasi ya Ubunge na tiyari pikipiki hizo zimeshaingia zikisubiri mpango ukamilike waweze kugawiwa.

Gambo mpaka sasa amefanikiwa kwa kiwango kikubwa kumweka mfukoni mwenyeviti wa ccm wilaya ,Joseph Masawe na Mwenyekiti Wa Ccm Mkoa Wa Arusha ,Zelothe Steven ambaye ushindi wake wa nafasi hiyo ulifanikishwa na Gambo pamoja na Catherine Magige kwa lengo la kuwasaidia katika mambo yao ya Ubunge.

 
Kikubwa ni kufutwa kwa Chadema Arusha
Kabisa, maendeleo arusha yamekua ya ovyo ovyo halafu ukiangalia wanaoshabikia chadema ni wahuni tu na vijana wa mtaani , ila mbunge wao ni tajiri ana pesa ila uliza maisha ya wananchi wake, sijajua hata alichoifanyia arusha
 
Hizo piki piki zitatolewa kama RUSHWA alafu kuna majinga yamekaa kimya huku yakimuwaza mbowe!
 
Arusha haitakaa ikaendeshwa na wachumia tumbo kamwe na ikitokea basi michumia tumbo itajiongoza yenyewe na sio wana ARUSHA !!
Unaisemea Arusha ipi wewe?,kwa sasa CCM imetamalaki kila kona we ndo umebaki
 
Nawaonea huruma Arusha. Yaani Gambo eti awe muwakilishi wenu Bungeni. Mtakuwa mmepotea sana, na mtakuwa mmepoteza nafasi.

Kwangu suala si CCM au CHADEMA, bali kupata mtu atayeweza kuwawakilisha kikamilifu kwa kipindi cha miaka 5. Jamani hata kama kutoka CCM tafuteni sura nyingine sio huyu anayeishi na na FITINA toka asubuhi mpaka usiku. Anajadili watu badala ya maendeleo.
 
Gambo hana nafasi kabisa pamoja na kusaidiwa na wafanyabiashara wakubwa kama mkurugenzi wa Kibo guide na wengine wa mawe bado atashindwa asubuhi na mapema.
 
Haya madaraka haya....yanatafutwa kwa udi na uvumba.
 
Kabisa, maendeleo arusha yamekua ya ovyo ovyo halafu ukiangalia wanaoshabikia chadema ni wahuni tu na vijana wa mtaani , ila mbunge wao ni tajiri ana pesa ila uliza maisha ya wananchi wake, sijajua hata alichoifanyia arusha
Vipi wananchi walio chini ya CCM wao hali zao zikoje?... Acheni ushabiki WA kipumbafu kama kuisoma namba tunaisoma sawa sawa bila kujali wewe ni Chadema NCCR au CCM,,,,,WE HAVE TO STOP THIS STUPID POLITICS FOR THE BETTER OF COUNTRY
 
Kwa hiyo ndo umekuja kumshitaki huku sawa.... ila kama mwenzako anagawa piki piki we gawa magari na kama mwenzako kamshika mwenyekiti wa wilaya na mkoa we mshike wa taifa... acha kulalamika pambana mkuu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…