CCM waibuka kidedea Bungeni

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kwa takribani siku sita,kulikuwa na mjadala juu ya Vifungu vya 37 na 38 vya Kanuni za Kudumu za Bunge la Katiba.Vifungu husika vinahusu namna ya kufikia uamuzi Bungeni kwa njia ya kupiga kura pale ambapo kutakuwa na haja ya kufanya hivyo. Kura zitapigwa hata wakati wa kupitishwa kwa kifungu kwa kifungu cha Rasimu ya Pili ya Katiba itakayojadiliwa na kupitishwa na Bunge.

Mvutano wa wazi na mkali ulikuwa juu ya Kura ya Wazi au Kura ya Siri. CCM katika mjadala mzima ilishindwa kuwashawishi Wajumbe waiunge mkono katika kuipigia upatu kura ya wazi. Mjadala ukawa mgumu na kuahirisha Bunge mara kwa mara. Ndipo ilipoundwa Kamati ya Maridhiano kushughulikia suala hilo.Hata Kamati nayo ikagonga mwamba katika kuamua.

Leo asubuhi,Bunge la Katiba limepitisha Kanuni husika likiviacha vifungu vya 37 na 38 kama vilivyo.Ikatolewa taarifa kuwa Kamati ya Maridhiano itashughulikia suala hilo. Hapo ndipo CCM iliponyakua ushindi. Baada ya kesho kuchaguliwa kwa Mwenyekiti wa kudumu wa Bunge la Katiba na Bunge kuanza kazi yake ipasavyo,maamuzi mengi na mamlaka yatakuwa katika kiti cha Mwenyekiti.

Kamati ya Maridhiano italazimika kumwachia Mwenyekiti aamue kuhusu suala hilo kwa kutumia busara zake. Iko wazi kuwa Mwenyekiti wa Kudumu atatokea CCM.Hii ni kwa kuangalia idadi wa Wajumbe wenye mafungamano na CCM. Hivyobasi,kuna uwezekano mkubwa Mwenyekiti huyo kutoka CCM akasimamia msimamo wa chama chetu wa kura ya wazi wakati wa kupitisha Rasimu ya Katiba. Na hapo ndipo mchezo utakapoishia.....

Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
 
Sijui ulikuwa wapi umeamshwa?alafu ukujua uanzie wapi
 
Yule mzee hakika atawageuka, na hiyo itakumbukwa katika historia ya Tanzania Daima.
 
CHADEMA na cuf wanataka siri ili ikifikia Yale mambo museveni ameyakataa wawezepiga kura bila kuffahamika hovyo kweli kura iwe ya wazii
 
mimi bado naona ngoma iko palepale,kama nilivyosema tukipita hiki kipengele cha kura ya wazi au ya siri basi tutapata katiba hata kabla ya siku 70
 
Mzee Vuta,
Siamini macho yangu ulichoandika leo. Swali la msingi, "Je katiba ni kwa manufaa ya nani?" Umesema kwa uhakika m/kiti atatokea ccm, je huo unategemea uamuzi tofauti na matakwa ya ccm katika namna ya upigaji kura?

It is a shame and pathetic the way ccm thinks that they own this country.
 
Wapinzani wa nchi hii ni "legelege" na kwangu sitoshangaa hilo likitokea.

Lakin tambua nguvu za upinzani hutoka kwe2 wananchi,kama hatujajitoa kwa dhati kuunga mkono upinzani ni wazi utakuwa legelege.Pia upinzani haujateremshwa toka mbinguni/angani bali unaundwa na sisi wananchi.Tukubali tukatae,sisi Watanzania ni "legelege" mno,hivyo usishangae na upinzani uka hvyo!
 
Ni wazi kwamba kama katiba mpya itapatikana kwa shinikizo la uwepo wa abunge wengi wa ccm, ni kuwa katiba hiyo haitakuwa na manufaa kwa Watanzania na itaacha kero nyingi katika jamii bila kushughulikiwa.

Kero hizo zitasababisha kuyumba kwa nchi na kulazimu kufanya marekebisho makubwa (amendments) kwenye katiba hiyo. Cha kusikitisha katika muonekano huo ni kwamba pesa za wananchi zitazidi kupotea, lakini hatimaye tutapata katiba ambayo wananchi wameiridhia.

Vile vile upo uwezekano wa ccm kupoteza uelekeo wake kutokana na shinikizo lao hili.
 
ni katiba ya ccm inaandikwa au?wameshinda kwa lipi?busara za mwenyekiti aijalishi aliyepita au atakayekuja haziwezi kuamua juu ya hilo isipokuwa tu kura ya siri ipigwe kuamua juu ya hilo alafu tutajua ccm wameshinda au ni watanzaniawameshinda
 
si kazi ya wapinzani tu kupinga mambo yasiyo haki bali wananchi wote, na pia wananchi ndo wenye maamuzi ya kuwatengeneza wapinzani wawe wakakamavu au legelege
 
CCM ni msaliti nambari moja wa Mtanzania...
 
Mh. Sitta haburuzwi na wao CCM wanalijua hilo, hawezi kuamua kuharibu record yake ili kuwafurahisha watu wa kundi lake. Pia umma wa watanzania wamejenga imani kuu juu yake!!

Ni wakati wake sasa upandisha turufu yake zaidi kuelekea 2015 - Taifa kwanza ukeleketwa wa ki-vyama baadaye
 

Hapo umesema kweli mkuu! Huyu mburura naye anamlaumu nani? Hapo sisi wote ni legelege ukimhusisha na huyo mburukenge! Si ajabu jamaa yuko kwa magamba! Tumb.ff kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…