Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,180
- 7,346
Msimamo wa CCM wa kutaka srikali mbili unatarajiwa kuibua mtifuano mkali sana siku chache zijazo.
Msimamo wa CCM unatariajia kupata upinzani mkubwa sana ndani na nje ya bunge kutoka katika timu zifuatazo
1. Wazanzibari - Wanataka serikali tatu na wana 'nguvu' kubwa kama mshirika mwenza kwenye muungano
2. Wapinzani - Wanataka serikali tatu na wana nguvu kubwa sana kwa kuwa wanaungwa mkono na majority of middle class people ambao wanasauti kubwa kupitia vyombo vya habari
3. Wazee wa chama - Ingawa Mukama na Nape waliua nguvu yao kwenye chama, lakini tumeona ushawishi mkubwa sana kwa wazee hawa ambao wengi wapo kimya (isipokuwa Kingunge) lakini ni wazi kuwa watamuunga mkono mzee mwenzao Warioba
4. Wananchi - Wamenena kupitia maoni yao kwenye rasimu kuwa wanataka serikali 3. Watakuwa na influence kubwa sana nje ya bunge
5. Tume ya marekebisho ya katiba - Wanatetea rasimu yao. Watasaidiwa sana na ushawishi wa watu kama Palamagamba na Butiku.
Tusisahau kuwa kamisaa wa mchezo (JK) nae anataka katiba mpya ipatikane na katika hilo anajua kuwa wakipeleka rasimu inayosema serikali mbili, itakuwa rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko rasimu hiyo kukubaliwa kwenye kura ya maoni...
Msimamo wa CCM unatariajia kupata upinzani mkubwa sana ndani na nje ya bunge kutoka katika timu zifuatazo
1. Wazanzibari - Wanataka serikali tatu na wana 'nguvu' kubwa kama mshirika mwenza kwenye muungano
2. Wapinzani - Wanataka serikali tatu na wana nguvu kubwa sana kwa kuwa wanaungwa mkono na majority of middle class people ambao wanasauti kubwa kupitia vyombo vya habari
3. Wazee wa chama - Ingawa Mukama na Nape waliua nguvu yao kwenye chama, lakini tumeona ushawishi mkubwa sana kwa wazee hawa ambao wengi wapo kimya (isipokuwa Kingunge) lakini ni wazi kuwa watamuunga mkono mzee mwenzao Warioba
4. Wananchi - Wamenena kupitia maoni yao kwenye rasimu kuwa wanataka serikali 3. Watakuwa na influence kubwa sana nje ya bunge
5. Tume ya marekebisho ya katiba - Wanatetea rasimu yao. Watasaidiwa sana na ushawishi wa watu kama Palamagamba na Butiku.
Tusisahau kuwa kamisaa wa mchezo (JK) nae anataka katiba mpya ipatikane na katika hilo anajua kuwa wakipeleka rasimu inayosema serikali mbili, itakuwa rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko rasimu hiyo kukubaliwa kwenye kura ya maoni...