Uchaguzi 2020 CCM wamesaidia kumpandisha chati Tundu Antipas Lissu

Uchaguzi 2020 CCM wamesaidia kumpandisha chati Tundu Antipas Lissu

UTAKUJA UJE

Member
Joined
Aug 4, 2020
Posts
34
Reaction score
78
Kila nikimsikiliza Tundu Lissu, nashindwa kuamini kama kweli anayosema ni uwezo wake mwenyewe au kuna nguvu gani nyuma yake. Ukiachilia mbali uwezo na ukuu wa Mungu aliyemponya kifo,ukaachilia mbali ujasiri wake,jambo kubwa linalomfanya Lissu akubalike na azidi kupaa kisiasa ni serikali ya CCM chini ya utawala kandamizi wa John Magufuli,ntafafanua.

Magufuli na Serikali yake wamekuwa wakijipambanua kuwa Serikali ya wanyonge na mtetezi wao mkuu. Unajiitaje serikali ya wanyonge ilihali Rais pekee anatembea na maburungutu ya pesa kwenye gari na kuwagawia wananchi kila pahala apitapo kwa kisingizio cha kutatua kero.Pesa hizo ni mshahara wa Rais! Ni pesa iloyoidhinishwa na wabunge!Inakaguliwa na nani?Majibu yake hayajulikani-lissu anapeta

Serikali ya CCM chini ya Magufuli iliwatimua wanafunzi pale UDOM ambao wengi wao ni watoto wa maskini.Mbaya zaidi ni kauli chafu toka kinywani mwa magufuli,kwamba wale ni vilaza.Unajiitaje mtetezi wa wanyonge ilihali unafukuza watoto wa wanyonge na kuharibu kabisa ndoto zao-tundu lissu pasua anga

Magufuli na CCM yake wamedhulumu haki za wafanyakazi. Huongezi mishahara ya wafanyakazi miaka mitano,hupandishi madaraja,wewe ni mnyonga wanyonge-lissu tusua,fisiem wamefeli

Mtetezi wa wanyonge anatumia mabilioni ya pesa kujenga uwanja wa ndege chato na miundombinu mingine mingi bora.Huku ni kuwafanya wananchi mazezeta.Makao makuu ya mkoa wa geita ni geita mjini,ulishindwa nn kujenga uwanja huo geita hadi uupeleke kijijini kwako?Pesa zote hizo ziliidhinishwa na bunge lipi?-Lissu hapa hapa piga goli la kisigino.

Mtetezi wa wanyonge anayezuia soko huru kwa wakuli,ni mnyonga wanyonge. Wakulima wengi wa mazao ya biashara kama vile pamba,korosho,kahawa nk,hawana uhuru wa kuuza mazao yao.Wanapangiwa bei na serikali na bado wanakopwa.Mh lissu komboa nchi kwa kuwapa haki wakulima

Kitokacho kinywani mwa Magufuli sicho atendacho. Magufuli amekuwa mwingi wa kujinasibu kwamba maendeleo hayana chama.Huyu huyu amekuwa wa kwanza kuwatisha wapiga kura kwamba wasipochagua wabunge wa fisiem kamwe hawezi kuwapelekea miradi ya maendeleo kama maji,barabara,umeme nk,pesa zinazotekeleza miradi hii ni kodi za wananchi si za magufuli wala babake!-lissu mtimulie vumbi utinge ikulu

Serikali na Rais waliofanya mazuri,ya nini kuminya uhuru wa habari?Tv zote,kipindi hiki zinamnadi magufuli tu,demokrasia iko wapi?Sera za wagombea wengine tutazipataje?Bunge live wakafungia,wanaogopa nn?-lissu kamatilia baba,ikulu ni yako

Magufuli na CCM yake wanajimaliza wenyewe,wananchi siyo wajinga,hamchaguliki tena,na kama siyo ubabe mnaopewa jeuri na polisi,hamkustahili kupata hata jimbo moja!Imetosha!Mkapumzike-mitano kwanza,tunasafiri na Tundu Antipas Lissu-Rais atakayerejesha uhuru wetu kupitia katiba mpya
 
... it may take sometime, but eventually, CCM is set to vanish! Nothing man-made lasts forever as they want people to believe that they will rule endlessly! Far away, beyond distant hills at the end of the tunnel, some light is seen! Yes, the upcoming generation will get rid of this monster!
 
Mkuu umesahau kugusia mikopo ya wanavyuo riba ni kubwa mno 6% of the remaining debt kila mwaka inaumiza sana mikopo ya vyuo imekuwa biashara

Vijana toka 2015 hawana ajira magufuli anasema wajiajiri na misingi ya kujiajiri haipo wala hawajatengeneza mazingira ya vijana kujiajiri
 
... it may take sometime, but eventually, CCM is set to vanish! Nothing man-made lasts forever as they want people to believe that they will rule endlessly! Far away, beyond distant hills at the end of the tunnel, some light is seen! Yes, the upcoming generation will get rid of this monster!
Daah mkuu, hii post yako nimei screenshot kwa matumizi ya siku zijazo
 
Muda mrefu tu wamekuwa wakiponywa ponywa na Tume ya Uchaguzi yao. Watu walikwishaikataa muda mrefu. Maalim Seif amekuwa akishinda tangu 1995.
... it may take sometime, but eventually, CCM is set to vanish! Nothing man-made lasts forever as they want people to believe that they will rule endlessly! Far away, beyond distant hills at the end of the tunnel, some light is seen! Yes, the upcoming generation will get rid of this monster!
 
... it may take sometime, but eventually, CCM is set to vanish! Nothing man-made lasts forever as they want people to believe that they will rule endlessly! Far away, beyond distant hills at the end of the tunnel, some light is seen! Yes, the upcoming generation will get rid of this monster!
Obviously because now days people have got awareness
 
KITOKACHO KINYWANI MWA MAGUFULI...
Sikilizeni wenyewe kinachotoka kinywani mwa Magufuli...

Hakika huyu si wa kuongezewa miaka mitano, ni wa kutimuliwa mwisho wa mwezi huu! Utawaombaje kura wananchi huku ukiwatukana? Na unapata wapi ujasiri wa kuwatukana wakati huna uhakika na unachokisema? Halafu hata huwaombi radhi, unaendelea tu kama vile wao si binadamu wenye akili? Huu ni ujasiri au ni ufedhuli tu kwa ulevi wa madaraka?
 
Mi nauza pagale ujenzi umenishinda kila siku vifaa vya ujenzi vinapanda juu
 
Muda mrefu tu wamekuwa wakiponywa ponywa na Tume ya Uchaguzi yao. Watu walikwishaikataa muda mrefu. Maalim Seif amekuwa akishinda tangu 1995.

Muacheni Naalimu Seif na uwekezaji wake, kakuomba umsemee kwani? Anasiri anayojua yeye na Hayati Nyerere basi kati ya Watanzania 60M.
 
Katika miaka mitano ya utawala huu, askari hawajapata sare mpya za kazi. Waliambiwa wajinunulie wenyewe.

Kwa sheria za kazi za Jumuia ya madola, kila baada ya miaka miwili walipaswa kupewa jozi mbili za uniforms na viatu vya kazi.
 
Katika miaka mitano ya utawala huu, askari hawajapata sare mpya za kazi. Waliambiwa wajinunulie wenyewe. Kwa sheria za kazi za Jumuia ya madola, kila baada ya miaka miwili walipaswa kupewa jozi mbili za uniforms na viatu vya kazi.
Wakiendelea kuendekeza,Tania waliyonayo watahitajika kulipia hata vitendea kazi vingine ili waendee kazini,kila moja alipie zana atakayo kuwa anatumia awapo kazini.
 
Hata HARMONIZE alimsaidia HARMO RAPA kupanda kwenye chart!

Baada ya hapo Harmorapa yuko wapi?? anavaa Minyororo shingoni(Not chain).

CHADEMA jijengeni kichama zaidi, msipende kutrend kwa vioja vya hapa na pale.
 
Umeandika kwa hisia kali sana, Mungu atalufanikisha hili siku moja
 
Uchaguzi huu CCM inakwenda kushinda kwa kishindo kwakua upinzani nidhaifu kuliko wakati wowote tangu kuanzishwa kwa vyama vingi.
 
CCM wenyewe wanajuta kumsukumiza mgonjwa wa bipolar disorder, mshamba na Limbukeni wa kutupa mhutu hajui anakotoka Wala anakoenda , hajui hata anachokifanya .
IMG_20201011_160558.jpg
 
Back
Top Bottom