Pre GE2025 CCM wasikiliza kero za Wananchi Babati. Ally Hapi atoa elfu 50 kwa mstaafu wa jeshi tangu mwaka 1994 ambaye anadai mafao mpaka leo

Pre GE2025 CCM wasikiliza kero za Wananchi Babati. Ally Hapi atoa elfu 50 kwa mstaafu wa jeshi tangu mwaka 1994 ambaye anadai mafao mpaka leo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Ally Hapi, amesema kuwa kero nyingi zinazowakabili wananchi zinatokana na baadhi ya watendaji waliopo kwenye nafasi mbalimbali kutotenga muda wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Akizungumza na wananchi wa Babati Mjini wakati akisikiliza kero zao, Hapi amewataka watendaji wa serikali kuacha kukaa ofisini na badala yake kushuka kwa wananchi ili kutatua changamoto zao zinazowakabili moja kwa moja huku akisisitiza kuwa kushindwa kufanya hivyo kunasababisha wananchi kukosa mahali pa kupeleka matatizo yao, hali inayowaacha wakilalamika bila msaada wowote.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Aidha, Hapi amesisitiza kuwa msingi wa CCM ni watu na haki, hivyo ni wajibu wa viongozi kuwajali na kuwathamini wananchi.

Amesema kuwa tabia ya kutosikiliza wananchi inachangia kuwafanya wakose mtetezi jambo ambalo linaweza kudhoofisha imani ya wananchi kwa serikali na Chama katika eneo husika.

Hapi amewataka viongozi na watendaji wote kuzingatia wajibu wao ili kuhakikisha changamoto za wananchi zinatatuliwa kwa haraka na kwa ufanisi.


 
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Ally Hapi, amesema kuwa kero nyingi zinazowakabili wananchi zinatokana na baadhi ya watendaji waliopo kwenye nafasi mbalimbali kutotenga muda wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Akizungumza na wananchi wa Babati Mjini wakati akisikiliza kero zao, Hapi amewataka watendaji wa serikali kuacha kukaa ofisini na badala yake kushuka kwa wananchi ili kutatua changamoto zao zinazowakabili moja kwa moja huku akisisitiza kuwa kushindwa kufanya hivyo kunasababisha wananchi kukosa mahali pa kupeleka matatizo yao, hali inayowaacha wakilalamika bila msaada wowote.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Aidha, Hapi amesisitiza kuwa msingi wa CCM ni watu na haki, hivyo ni wajibu wa viongozi kuwajali na kuwathamini wananchi.

Amesema kuwa tabia ya kutosikiliza wananchi inachangia kuwafanya wakose mtetezi jambo ambalo linaweza kudhoofisha imani ya wananchi kwa serikali na Chama katika eneo husika.

Hapi amewataka viongozi na watendaji wote kuzingatia wajibu wao ili kuhakikisha changamoto za wananchi zinatatuliwa kwa haraka na kwa ufanisi.

50000 itamsaidia nini sasa? Seriously? Hiko nacho ni kitu cha kupost?
 
sasa afu50 ndio itafanya nini? yaani kumi kumi 5? ndio za kumpooza?
 
Back
Top Bottom