CCM weka hadharani sababu hasa za Serikali mbili

CCM weka hadharani sababu hasa za Serikali mbili

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Miaka 50 ya muungano imepita huku watanzania wakihoji kwanini kuna serikali ya Zanzibar lakini hakuna serikali ya Tanganyika, majibu yaliyokuwa yakitolewa kujibu swali hili yanapingana na majibu yanayotolewa na upande wa Zanzibar yanayodai kuwa Zanzibar ni nchi kamili iliyokuwa huru na yenye mipaka yake kamili na katiba, bendera na wimbo wa taifa wake.

Majibu yaliyokuwa wakipewa watanganyika yalidai kwamba Tanganyika ni nchi kubwa kuliko Zanzibar hivyo muungano ungeimeza Zanzibar. Majibu ya namna hii yaliwakanganya watanzania hasa watanganyika kwa miaka 50 sasa maana hayawaingii akilini. Hivi ni nani anayewaoenea huruma wa Zanzibar kuwa watamezwa na Tanganyika kwenye muungano wakati mipaka ya Zanzibar kama nchi inajulikana tangu awali kama ilivyo kwa mipaka ya vijiji, kata, wilaya na mikoa nchini inavyofahamika pia? Sijawahi kusikia mkoa wa Dar es Salaam umeumeza mkoa wa Arusha, Lindi, Mwanza wala Morogoro kwa jambo lolote.

Madaraka ya mkuu wa mkoa wa Mbeya yanajulikana na yale ya mkuu wa mkoa wa Kigoma yanafahamika pia. Sababu ya Zanzibar kumezwa na Tanganyika haina mashiko hata kidogo. Watanzania wanahitaji kufahamu kwanini muungano uwe wa serikali mbili na sio moja wala tatu. Hatutaki kuumiza vichwa vyetu kwa miaka 50 mingine tena kwa swali kama hili. Tunaomba sababu halisi ya serikali mbili CCM waiweke hadharani ili watu wote tuzijue, maana taifa hili ni letu sote sio la CCM.

Inavyoonekana wazanzibari hawataki serikali moja ambayo ndiyo ingeleta uimara wa muungano. Ili kuleta ulinganifu wa kinachotokea Zanzibar ni kubadilisha utawala wa mikoa ya Tanzania bara ijiendeshe yenyewe kwa asilimia fulani chini ya mkuu wao wa mkoa wa kuchaguluwa na wanamkoa wenyewe kama vile mkuu wa Zanzibar yenye watu mil. 1 anavyochaguliwa na Wazanzibari wenyewe.

Kisha tutahiyari jina la kumuita huyo mkuu wa mkoa aliyechaguliwa na wananchi wenyewe kama aitwe mkuu wa mkoa, rais wa mkoa au gavana, mtemi, n.k wa mkoa husika. Kisha kila mkoa uwe na sheria, kodi na taratibu zake kama ilivyo kwa Zanzibar. Mwisho wa siku tunakuwa na Rais mmoja tu wa jamhuri ya Tanzania mwenye heshima ndani ya nchi na kimataifa.

Bunge la katibu msije mkapoteza fursa hii adimu mkaja na katiba itakayolalamikiwa tena kwa miaka 50. tangulizenu utaifa mbele. Serikali mbili ni kwamanufaa ya nani?
 
1. kudumisha muungano
2. kuepuka mzigo mzito wa gharama kwa mtanzania maskini kuendesha serikali tatu, ya nne ikiwa ni serikali za mitaa (halmashauri na mikoa)
3. hakuna sababu ya msingi kwenda kwenye serikali 3 kama kweli tunataka kuimarisha muungano,
 
Majibu marahisi kwa masawali magumu
1. kudumisha muungano
2. kuepuka mzigo mzito wa gharama kwa mtanzania maskini kuendesha serikali tatu, ya nne ikiwa ni serikali za mitaa (halmashauri na mikoa)
3. hakuna sababu ya msingi kwenda kwenye serikali 3 kama kweli tunataka kuimarisha muungano,
 
tanzania ni nchi maskini hakuna sababu ya kujiongezea gharama ya kuanzisha madaraka mapya. hao maafisa wa serikali ya tatu tutawalipa kwa kodi zetu wenyewe. hatuna uwezo huo tafadhali
 
Wewe ndio unahitaji kubalehe,ni lini mtakubali kwamba huu muungano haupo?Zanzibar ni nchi ila tanganyika ni tanzania,zanzibar iliungana na nani?when you guys realize that you are living a life of an ostrich,then you will have reached your puberity
acha mawazo mfu dogo, balehe
 
Miaka 50 ya muungano imepita huku watanzania wakihoji kwanini kuna serikali ya Zanzibar lakini hakuna serikali ya Tanganyika, majibu yaliyokuwa yakitolewa kujibu swali hili yanapingana na majibu yanayotolewa na upande wa Zanzibar yanayodai kuwa Zanzibar ni nchi kamili iliyokuwa huru na yenye mipaka yake kamili na katiba, bendera na wimbo wa taifa wake. Majibu yaliyokuwa wakipewa watanganyika yalidai kwamba Tanganyika ni nchi kubwa kuliko Zanzibar hivyo muungano ungeimeza Zanzibar. Majibu ya namna hii yaliwakanganya watanzania hasa watanganyika kwa miaka 50 sasa maana hayawaingii akilini. Hivi ni nani anayewaoenea huruma wa Zanzibar kuwa watamezwa na Tanganyika kwenye muungano wakati mipaka ya Zanzibar kama nchi inajulikana tangu awali kama ilivyo kwa mipaka ya vijiji, kata, wilaya na mikoa nchini inavyofahamika pia? Sijawahi kusikia mkoa wa Dar es Salaam umeumeza mkoa wa Arusha, Lindi, Mwanza wala Morogoro kwa jambo lolote. Madaraka ya mkuu wa mkoa wa Mbeya yanajulikana na yale ya mkuu wa mkoa wa Kigoma yanafahamika pia. Sababu ya Zanzibar kumezwa na Tanganyika haina mashiko hata kidogo. Watanzania wanahitaji kufahamu kwanini muungano uwe wa serikali mbili na sio moja wala tatu. Hatutaki kuumiza vichwa vyetu kwa miaka 50 mingine tena kwa swali kama hili. Tunaomba sababu halisi ya serikali mbili CCM waiweke hadharani ili watu wote tuzijue, maana taifa hili ni letu sote sio la CCM. Inavyoonekana wazanzibari hawataki serikali moja ambayo ndiyo ingeleta uimara wa muungano. Ili kuleta ulinganifu wa kinachotokea Zanzibar ni kubadilisha utawala wa mikoa ya Tanzania bara ijiendeshe yenyewe kwa asilimia fulani chini ya mkuu wao wa mkoa wa kuchaguluwa na wanamkoa wenyewe kama vile mkuu wa Zanzibar yenye watu mil. 1 anavyochaguliwa na Wazanzibari wenyewe. Kisha tutahiyari jina la kumuita huyo mkuu wa mkoa aliyechaguliwa na wananchi wenyewe kama aitwe mkuu wa mkoa, rais wa mkoa au gavana, mtemi, n.k wa mkoa husika. Kisha kila mkoa uwe na sheria, kodi na taratibu zake kama ilivyo kwa Zanzibar. Mwisho wa siku tunakuwa na Rais mmoja tu wa jamhuri ya Tanzania mwenye heshima ndani ya nchi na kimataifa. Bunge la katibu msije mkapoteza fursa hii adimu mkaja na katiba itakayolalamikiwa tena kwa miaka 50. tangulizenu utaifa mbele. Serikali mbili ni kwamanufaa ya nani?
ufumbuzi hapa ni sekali!; tatu.3 au.Moja.1 hatutaki bla bla ya serkali mbili.2! hapa hakuna kitu muungano sababu zenj bado ni bado ya wazenji tu! Na Tanganyika imegeuzwa kitega uchumi cha wazenj!
 
Mie huwa nawashangaa watanganyika,hivi kwann muungano uwe kwa zanzibr tu kama vile hakuna nchi nyengine duniani,tunasema tena na tena na tena na tena tuachiwe tupumuee.. Zanzbr kwanza.
 
tanzania ni nchi maskini hakuna sababu ya kujiongezea gharama ya kuanzisha madaraka mapya. hao maafisa wa serikali ya tatu tutawalipa kwa kodi zetu wenyewe. hatuna uwezo huo tafadhali
Kwani kwa sasa hayo mambo yanayopendekezwa kuwa ndiyo yawe ya muungano yanagharimiwa na nani? Tunaye rais wa jamhuri ya muungano - anagharimiwa na nani? Tunaye waziri mkuu ambaye ni wa-Tanganyika tu kwa sasa anagharimiwa na nani? Kinachotakiwa ni kuwa na bunge dogo la muungano na bunge la wastani la Tanganyika (hivyohivyo kwa serikali) ndiyo maana tunataka katiba itaje idadi ya wizara. Hii itasaidia kutumia gharama chini kuliko za sasa kundesha serikali tatu. Kwa maoni yangu tayari tunazo serikali tatu, ila ile ya tatu (ya Tanganyika) imejificha kwenye serikali ya muungano - tunataka nayo iwe wazi. Hata mambo yetu yapo kiserikali tatutatu; kwa mfano katika vyama vya siasa -unaye mwenyekiti, halafu makamu mwenyekiti bara(Tanganyika) na makamu mwenyekiti zanzibar; na kwa wengine hata makatibu wakuu wako hivyo hivyo! Its time to walk the talk
 
Back
Top Bottom