Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita kimepata pigo baada ya diwani wake wa Kata ya Nyaruyeye Halmashauri ya Geita, Malimi Saguda kufariki dunia.
Malimi ameshika nafasi ya udiwani kwa vipindi viwili mfululizo na amefikwa na mauti akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Bugando kwa ugonjwa wa nimonia tangu Novemba 23, 2024.
Ni miezi minne imepita tangu diwani mwingine wa baraza hilo, Peter Kulwa aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari apoteze maisha.
Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani wa Halmashuri ya Geita, Charles Kazungu amesema kifo hicho kilitokea jana Desemba 5, 2024 wakati akipatiwa matibabu jijini Mwanza.
Malimi ameshika nafasi ya udiwani kwa vipindi viwili mfululizo na amefikwa na mauti akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Bugando kwa ugonjwa wa nimonia tangu Novemba 23, 2024.
Ni miezi minne imepita tangu diwani mwingine wa baraza hilo, Peter Kulwa aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari apoteze maisha.
Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani wa Halmashuri ya Geita, Charles Kazungu amesema kifo hicho kilitokea jana Desemba 5, 2024 wakati akipatiwa matibabu jijini Mwanza.