Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
Takwimu mbalimbali machoni pa uongozi wa juu wa CCM zimedhihirisha uchaguzi huu watadondoka vibaya katika Uraisi na Ubunge lakini watapeta katika udiwani.
Mwaka 1995, CCM walipoona viti vyote saba vya ubunge jijini Dar vinabebwa na NCCR-MAGEUZI serikali ya CCM iliitumia NEC kuchelewesha vitendea kazi vya uchaguzi na hivyo kuahirisha uchaguzi ili kuipa CCM nafasi ya kujipanga upya na huku wakielewa hasira za wapigakura dhidi yake zitakuwa zimepoa. Vilevile wengi wa wapigakura hawatarudi kupiga kura na matokeo yake mahudhurio kwenye chaguzi zilizoahirishwa yalikuwa ni kiduchu sana na CCM ilipeta kwenye majimbo sita ukiliondoa la Ubungo ambalo Dr. masumbuko Lamwai alilishinda. Hata yeye baadaye Mahakama Kuu ilitengua ushindi wake na CCM wakalibeba kiulaini!!!
Kutokana na historia hiyo ya kifisadi ambayo serikali ya CCM iliwahi kuitumia mwaka 1995 kwa ubunge wa majimbo ya Dar-Es-salaam upo wasiwasi mkubwa kuwa huenda mbinu hizo zikajirudia mwaka huu ili kupooza hasira za wapigakura na wakati huohuo CCM kujipanga upya kujibu mashambulizi...
Tunahitaji NEC watuhakikishie ya zamani hayatajirudia tena safari hii......Maana ni vigumu kwa mtu yeyote mwenye akili timamu kuelewa ilikuwaje mwaka 1995 Dar iwe haina vitendea kazi vya uchaguzi lakini kwingineko nchi nzima wasipate tatizo hilo. Ikumbukwe Makao Makuu ya NEC yapo Dar-Es-Salaam!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mwaka 1995, CCM walipoona viti vyote saba vya ubunge jijini Dar vinabebwa na NCCR-MAGEUZI serikali ya CCM iliitumia NEC kuchelewesha vitendea kazi vya uchaguzi na hivyo kuahirisha uchaguzi ili kuipa CCM nafasi ya kujipanga upya na huku wakielewa hasira za wapigakura dhidi yake zitakuwa zimepoa. Vilevile wengi wa wapigakura hawatarudi kupiga kura na matokeo yake mahudhurio kwenye chaguzi zilizoahirishwa yalikuwa ni kiduchu sana na CCM ilipeta kwenye majimbo sita ukiliondoa la Ubungo ambalo Dr. masumbuko Lamwai alilishinda. Hata yeye baadaye Mahakama Kuu ilitengua ushindi wake na CCM wakalibeba kiulaini!!!
Kutokana na historia hiyo ya kifisadi ambayo serikali ya CCM iliwahi kuitumia mwaka 1995 kwa ubunge wa majimbo ya Dar-Es-salaam upo wasiwasi mkubwa kuwa huenda mbinu hizo zikajirudia mwaka huu ili kupooza hasira za wapigakura na wakati huohuo CCM kujipanga upya kujibu mashambulizi...
Tunahitaji NEC watuhakikishie ya zamani hayatajirudia tena safari hii......Maana ni vigumu kwa mtu yeyote mwenye akili timamu kuelewa ilikuwaje mwaka 1995 Dar iwe haina vitendea kazi vya uchaguzi lakini kwingineko nchi nzima wasipate tatizo hilo. Ikumbukwe Makao Makuu ya NEC yapo Dar-Es-Salaam!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!