MwanaDiwani
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 5,536
- 2,266
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza mchakato wake wa uundaji mabaraza ya Katiba huku kikisisitiza msimamo wake ni kuwepo serikali mbili.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Nape Nnauye, amesema, chama hicho kimeshaunda mabaraza hayo kuanzia ngazi ya matawi hadi mkoa.
Alisema kuanzia Agosti 20 hadi 25 , vikao vya taifa vya chama hicho, vitapitia mapendekezo ya mabaraza hayo kabla ya kuyawasilisha kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Kwa mujibu wa Nape, kuanzia Agosti 20 hadi 23 kutakuwa na vikao vya Sekretarieti na kuanzia 24 hadi 25 kutakuwa na vikao vya juu vya taifa kwa ajili ya kupitia mapendekezo kabla ya kuwasilisha kwenye tume.
Akizungumzia msimamo wa chama wa kupinga kipengele cha Rasimu ya Katiba kinachopendekeza kuwepo kwa Serikali tatu, alisema msimamo huo hautakinzana wala kusababisha mvutano au ugomvi na makundi yenye msimamo tofauti.
Alisema tangu chama hicho kilipoweka hadharani hoja yake ya kupinga kipengele hicho na kupendekeza kuwepo na Serikali mbili, kumekuwepo na dhana potofu zinazosambazwa kwamba chama hicho, kina mvutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, jambo ambalo alisisitiza kuwa si kweli.
CCM inaamini kuwa haiwezekani kutengeneza Katiba itakayofurahisha watu wote wakati mmoja, hivyo ni vyema kuheshimiana na kuvumiliana katika mjadala wa kuboresha rasimu hii , hatuna ugomvi na tume wala mtu yeyote jambo la msingi tushindane kwa hoja, alisisitiza Nnauye.
Alisema haimaanishi kwamba chama hicho kinapuuza na kugombana wale wenye hoja tofauti kuhusu kipengele hicho.
Nasema hivi kwa kuwa kumekuwa na hoja kwenye baadhi ya vyombo vya habari ambazo zinawaaminisha wananchi kwamba, kitendo cha CCM kupinga kipengele hiki kimesababisha kuwepo na mvutano baina yake na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema.
Alisema chama hicho hakimshinikizi mtu akubaliane na mawazo yake na kwamba CCM kama taasisi inayo uhuru wa kuchangia rasimu, lakini yenyewe ni sehemu ndogo tu ya watanzania na iko tayari kuheshimu mawazo yao.
Chanzo: Habarileo.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Nape Nnauye, amesema, chama hicho kimeshaunda mabaraza hayo kuanzia ngazi ya matawi hadi mkoa.
Alisema kuanzia Agosti 20 hadi 25 , vikao vya taifa vya chama hicho, vitapitia mapendekezo ya mabaraza hayo kabla ya kuyawasilisha kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Kwa mujibu wa Nape, kuanzia Agosti 20 hadi 23 kutakuwa na vikao vya Sekretarieti na kuanzia 24 hadi 25 kutakuwa na vikao vya juu vya taifa kwa ajili ya kupitia mapendekezo kabla ya kuwasilisha kwenye tume.
Akizungumzia msimamo wa chama wa kupinga kipengele cha Rasimu ya Katiba kinachopendekeza kuwepo kwa Serikali tatu, alisema msimamo huo hautakinzana wala kusababisha mvutano au ugomvi na makundi yenye msimamo tofauti.
Alisema tangu chama hicho kilipoweka hadharani hoja yake ya kupinga kipengele hicho na kupendekeza kuwepo na Serikali mbili, kumekuwepo na dhana potofu zinazosambazwa kwamba chama hicho, kina mvutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, jambo ambalo alisisitiza kuwa si kweli.
CCM inaamini kuwa haiwezekani kutengeneza Katiba itakayofurahisha watu wote wakati mmoja, hivyo ni vyema kuheshimiana na kuvumiliana katika mjadala wa kuboresha rasimu hii , hatuna ugomvi na tume wala mtu yeyote jambo la msingi tushindane kwa hoja, alisisitiza Nnauye.
Alisema haimaanishi kwamba chama hicho kinapuuza na kugombana wale wenye hoja tofauti kuhusu kipengele hicho.
Nasema hivi kwa kuwa kumekuwa na hoja kwenye baadhi ya vyombo vya habari ambazo zinawaaminisha wananchi kwamba, kitendo cha CCM kupinga kipengele hiki kimesababisha kuwepo na mvutano baina yake na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema.
Alisema chama hicho hakimshinikizi mtu akubaliane na mawazo yake na kwamba CCM kama taasisi inayo uhuru wa kuchangia rasimu, lakini yenyewe ni sehemu ndogo tu ya watanzania na iko tayari kuheshimu mawazo yao.
Chanzo: Habarileo.