LGE2024 CCM Yatoa Wito wa Viongozi Waadilifu Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

LGE2024 CCM Yatoa Wito wa Viongozi Waadilifu Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Kada Mzalendo

Senior Member
Joined
Oct 9, 2024
Posts
142
Reaction score
97
KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametoa wito mzito kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi na wananchi kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, akisisitiza umuhimu wa kuchagua viongozi waadilifu na wenye moyo wa kuwatumikia wananchi.

Ametaka wagombea wanaoteuliwa wawe watu wanaopenda amani na utumishi, huku akiwakemea wale wenye chuki na visasi.

“Nyinyi wanaCCM mnatakiwa kutuchagulia wagombea wazuri, wanaojua kuwa uongozi ni utumishi. Mtu asiyependa watu na aliyejaa chuki hafai kuwa kiongozi wa wananchi,” alisema Dk. Nchimbi.

Aidha, amewataka wananchi waendelee kuiamini CCM kama chombo kinacholenga kuwaletea maendeleo endelevu. "Endeleeni kukiamini Chama cha Mapinduzi ili tuzidi kushika dola na kuongoza kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania," alihimiza Dk. Nchimbi.

 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametoa wito mzito kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi na wananchi kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, akisisitiza umuhimu wa kuchagua viongozi waadilifu na wenye moyo wa kuwatumikia wananchi.

Ametaka wagombea wanaoteuliwa wawe watu wanaopenda amani na utumishi, huku akiwakemea wale wenye chuki na visasi.

“Nyinyi wanaCCM mnatakiwa kutuchagulia wagombea wazuri, wanaojua kuwa uongozi ni utumishi. Mtu asiyependa watu na aliyejaa chuki hafai kuwa kiongozi wa wananchi,” alisema Dk. Nchimbi.

Aidha, amewataka wananchi waendelee kuiamini CCM kama chombo kinacholenga kuwaletea maendeleo endelevu. "Endeleeni kukiamini Chama cha Mapinduzi ili tuzidi kushika dola na kuongoza kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania," alihimiza Dk. Nchimbi.

View attachment 3132812
ni ujumbe mzito na wa maana sana kutolewa na kiongozi mwandamizi wa chama kinachoaninika na kukubalika kwa waTanzania, na kwa maana nyingine ni agizo kwa waTanzania kuzingatia wito huo na kuufanyia kazi kwa vitendo kwa wakati muafaka.

thank you CCM SG for a powerful massage of the day 🐒
 
Back
Top Bottom