Hamna kitu ,hawa wajamaa wanaelewana vizuri sana tu,ila mikakati yao ya kuelewana ni kuonyesha picha kama hawaelewani machoni mwa Watanzania waliolala.
Hali hiyo inasababisha kujenga tamaa miongoni mwa watu na kuonekana hiki kitavunjika na kile kitapatikana.
Kwa zaidi ninavyowaelewa wanapanga mipango ya kuwababaisha wananchi na pia kupanga mipango ya kuihadaa dunia ,ila wanasahau kuwa dunia ya leo kuna wanaowaelewa na mbinu wanazotumia za kutoleana mijicho ni za kinafiki.
Unaweza kuwa ndani ya majambazi na kushirikiana nao kila kitu wakati wewe si jambazi na ikitokea kukamatwa wewe unaachiliwa kivyakovyako ,jamaa wa usalama wananielewa nazungumza kitu gani.
Kuliona wanalocheza nalo CCM ,angalia ushirikiano wao katika ufisadi na kauli zao, utawasikia wanalishughulikia na wengine watafikishwa mahakamani ,wakati siku zinaongezeka na hakuna la maana linaloonekana.
Mikwaruzano unayoiona iweke katika kundi la propaganda ,hapo utaielewa vizuri sana ni usanii ambao inabidi tushikane mashati na kutoana nishai ,lakini letu moja tunaelewa tunachokifanya ,ila wale wasiotuelewa wanaona kuna tatizo kubwa sana.