yvegenc prymacov
JF-Expert Member
- Jan 22, 2023
- 1,530
- 1,961
Unajua kusoma na kuandika,lkn kina mambo mengi sana huyajui yaliyokuwa yakiendelea kipindi cha utawala wa awamu ya tano.Ni Magufuli ndio alijitengenezea hayo mazingira, alimpuuza makamu wake. Magufuli alikuwa hajali mambo ya katiba. Kuna uhuni walitaka kuufanya nafikiri kuna kitu walistuka, ndio maana Samia akamwondoa Mabeyo kabla ya muda wake. Hata hivyo Mabeyo angetulia tu aachane na hayo mambo hayo. Si vizuri CDF kuongeaongea, mbona wenzake kina Mwamunyange wako kimya? Msukuma ni msukuma tu
Kwani yeye atakaa hapo milele? Ile nikupokezana tu unamkomoa tu wewe ipo siku hata wajukuu wanaitubia hiyo dhambiKwa Kweli walimdharau mno mama, Nimefurahi alivyowatia adabu. Mpaka sasa wanaishi na machungu sana.
Kufa ni Mpango wa Mungu lakini sio kila kifo anapanga Mungu, Kwa kifo cha Magu(RIP Brother) ilikuwa sio rahisi kutangazwa chanzo walichosema.Wewe unazungumzia Matokeo, hujui root causes. CDF amefanya kazi yake ya kutufahamisha nia ovu ya Sukuma gang dhidi ya Mama Samia. Wakajisahau kuwa kama Mungu ameruhusu kifo kitokee yeye ndio anayeruhusu nani awe Rais
NonsenseMagufuli alikua hafuati katiba katika kuongoza nchi kwahiyo hilo wala tusolishangae ndio maana watu kama bashite walikua na sauti kumzidi hata waziri mkuu au makamu wa rais.
Umenena vema mkuu, naungana na wewe.Nadhani kwa kiasi kikubwa mtazamo wako upo sahihi. Umesahau tu kujumuisha nafasi ya Bunge na Mahakama.
Ninachoona hapa ni mgongano wa mitazamo inayoegemea nadharia vs mazingira halisi.
Tujiulize, nani aliwakataza hao tunaoamini kuwa walistahili kushika hatamu wasishike hatamu! kwa nini nao walibaki kuwa wananchi!
Mazingira halisi ni kuwa Mkuu wa Serikali na Mkuu wa nchi anapokuwa katika hatari kubwa au nchi inapokuwa katika hatari kuingia au kuingizwa katika failed state kuna watu wanashika usukanai kwa ridhaa ya Mkuu mwenyewe au bila ridhaa yake regardless ya mwongozo wa kikatiba. Na mara nyingine hiyo ndio inakuwa mwisho wa katiba na desturi zilizokuwepo.
Ukimsikiliza kwa makini na ukatafakari kwa utulivu utaona kuwa the three giant ndio walishika usukani katika kipindi mhusika alipopoteza uwezo wa kuongoza hadi siku mbili baada ya kuondoka. wengine walikuwa wasikilizaji na wafuata maagizo. Lakini kubwa zaidi kulikuwa na sintofahamu kadhaa ndio maana mambo hayakwenda pengine vile wengi wangetarajia. Hizo sintofahamu hajaziweka wazi na pengine hazitokuja kuwa wazi kamwe. watabaki watu wachache wanaojua ni kilitokea, chanzo kilikuwa nini na waanzilishi wamechukuliwa hatua gani?
Pengine hao ambao wewe unahisi walipaswa kushika usukanai wangepewa fursa, pengine mambo yasingekuwa hivi yalivyo.
Hao ndugu watatu waliotuvusha wanastahili pongezi za hali ya juu sana, walizishinda nafsi na kuweka maslahi ya Tz mbele. Wangekuwa na tamaa au wangetetereka sijui tz ingekuwa ya namna gani hadi sasa.
Nahisi hao Giants huwa ni muhimu sana wakati wa uchaguzi mkuu hususan inapofika saa moja jioni baada mchakato wa kupiga kura kukamilika hadi saa ya kutangaza matokeo. Katika kipindi hicho hao watatu wasipokuwa na wewe imekula kwako. Ndugu yetu Lungu na Yule aliyepo Nyasa wanajua role ya hao watatu katika nyakati hizo.
Hakika.Ifahamike pia kuwa, katika uhalisia, makamu wa Rais kwa Tanzania ni cheo kisichokuwa na uzito wowote. Ni mtu wa kutumwa. Asipotumwa, anashughulika na masuala tu ya Mwungano na mazingira
AlooIfahamike pia kuwa, katika uhalisia, makamu wa Rais kwa Tanzania ni cheo kisichokuwa na uzito wowote. Ni mtu wa kutumwa. Asipotumwa, anashughulika na masuala tu ya Mwungano na mazingira.
Inaonekana kuwa mpango mzima wa kumtenga Makamu wa Rais uliwekwa na Magufuli.1. Aliyestahili kumpatia taarifa Makamo wa Rais juu ya kifo cha Rais Magufuli ni daktari wa Rais.
2. CDF Mabeyo alikuwa mkuu wa majeshi ndiyo, yeye pamoja na viongozi wengine wa vyombo vya usalama walitakiwa pia kupatiwa taarifa na Makamo wa Rais (Baada ya yeye kuwa mtu wa kwanza kabisa kufahamishwa) ili kuhakikisha tu usalama wa nchi upo vizuri.
3. Makamo wa Rais ndiye alitakiwa kuwa mtu wa kwanza kila hatua kujua afya ya Rais inaendeleaje.
4. CDF anachukua majukumu ya kuwa msaidizi mkuu wa Rais na mtoa taarifa kwa Makamo kuwa Rais amefariki (Kosa kubwa) mbaya zaidi Makamo wa Rais anakuwa mtu wa nne kuambiwa baada ya Waziri mkuu, CS na Taasisi ya kiswahili (Baada ya kujadili mpaka cheo cha Amiri jeshi mkuu)
Kosa ni la nani? Hayati Magufuli kujiundia kikundi chake cha siri kwa mambo yao huku wakimuondoa Makamo? Wasaidizi wake wakati Rais ni mgonjwa? Makamo wa Rais yupo Tanga anaongea kawaida tu huku Rais yupo kitandani akipigania uhai na wala hajulishwi hadi umauti tena masaa manne mbele baada ya mijadala ambayo kimsingi watu hawaijui katiba. Inafikirisha.
Sishangai kuona daktari binafsi wa hayati Rais Magufuli Prof. Mabula Mchembe kupotea ulingoni baada ya Samia kuwa Rais? Hivi yuko wapi huyu mtu?
Kwani hiyo ni hospitali ya nini? Kama hufahamu, ni heri ukakaa kimya. Serikali imeboresha sana hospital za jeshi.Kwa hiyo hii hospital ni bora zaid ya hospital za Jeshi ambako ndiko kunapaswa kuwepo huduma za kitabibu za juu zaidi kulingana na mahitaji..wanajeshi wanakwenda vitani na ni kundi kubwa wanahitaji huduma bora za kitatibu..nje ya kutibu viongozi wanapougua hii hospital ya mzena wanamtibu nani? Kwa nini zisiboreshwe zile hospital za jeshi?
Mzee wa Kino pole sana π€£π€£Huyu mchembe mke wake alipokuwa dc gairo alitutingisha sana,alikuwa jeuri sana
Ova
Pia inaweza kua ni mbinu ya kiusalama. Maana kama watu hawakutaki, unajua wana kuwazia nn?Nimeona Mabeyo akisema Magufuli {RIP} alivyoona hali yake ni mbaya na hawezi kupona tena, alimwambia Mabeyo amrudishe nyumbani.
Lakini Mabeyo akamwambia hawezi kuamuru hivyo, Magufuli akaonekana kumshangaa hata wewe CDF unashindwa kuamuru nirudishwe nyumbani?, Mabeyo akamwambia jukumu la kuamuru hivyo haliko chini yangu, hilo ni jukumu la madaktari.
Hata hili la Samia kuwa Tanga kwa shughuli za kiserikali, nalo linaweza kuwa tofauti na wengi tunavyodhani kwamba alifichwa.
Inawezekana ulikuwa mpango wao kutuficha sisi tusijue nini kinaendelea kumuhusu Magufuli, ndio maana hata PM nae akaja na hadithi Magufuli yuko mzima anachapa kazi, hii imekuwa tabia yao kutuficha hata ugonjwa wa viongozi wengine.
Unless Samia mwenyewe aje kuthibitisha vinginevyo, kwangu inawezekana kabisa licha ya Samia kuwa Tanga bado alikuwa anafahamu kila kitu kinachoendelea kuhusu afya ya Marehemu Magufuli, ni siri zao huko serikalini.
Kuna watu wanahisi Raisi na Makamu wake ni kama mke na mme, wako bega kwa begaKatiba kuhusu Rais na Makamu wake inafanana na katiba ya marekani kuwa Rais akifa Makamu anakuwa Rais. Sasa wewe unaonekana hujaangalia movie na series za kimarekani kuhusu vita iliyopo kwa Makamu kuutaka Urais!
RC Chalamila akiwa katika lindi la huzuni alisema kwa Katiba hii basi Rais aombe asipate Makamu Mchawi maana atamuondoa fasta akae yeye.
Kwa ilivyo Rais ni Taasis inayojiendesha kivyake na Makamu nae ni Taasis inayojiendesha kivyake kwa nchi yetu Rais ndio executive na Makamu wake anashughulika na Mazingira na Muungano basi. Mambo ya executive anapewa na Rais yale yaliyo katika level yake na ya vikao vya baraza la mawaziri so to say presidential general issues lakini exclusive zinabaki kwa Rais mwenyewe na vyombo vya dola vya nchi
Ameongea kipi kibaya? Unataka Mwamunyange aongeze kitu ambacho wakati kunatokea hakuwepo?Ni Magufuli ndio alijitengenezea hayo mazingira, alimpuuza makamu wake. Magufuli alikuwa hajali mambo ya katiba. Kuna uhuni walitaka kuufanya nafikiri kuna kitu walistuka, ndio maana Samia akamwondoa Mabeyo kabla ya muda wake. Hata hivyo Mabeyo angetulia tu aachane na hayo mambo hayo. Si vizuri CDF kuongeaongea, mbona wenzake kina Mwamunyange wako kimya? Msukuma ni msukuma tu
Balaa halafu watu wakajikuta ni wataalamu wa itifaki na masuala ya usalama wa taifa!humu kuna porojo za vijiweni balaaa
Una mengi ya kujifunza kuhusu CDF, IGP na Mkuu wa usalama wa Taifa.Chain of command
PRESIDENT >>V. P>>P. M huyo CDF ni mbali Sana anaripoti kwa waziri wa Ulinzi, Inakuwaje top secret ifahamike na CDF halafu VP na PM wasijue?
Pengine mwendazake alihisi kuna wasaliti hivyo akaamua kuvunja chain of command??
Msamehe mkuu πππ.CDF anaripoti kwa Waziri wa ulinzi??
Jamani tupumzisheni kidogo.