CECAFA Championship Record: Any Conclusion

CECAFA Championship Record: Any Conclusion

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Baada ya uhuru tulikuwa na mashindano yanitwa Gossage Cup. Mashindano haya yalikuwa yanadhaminiwa na kampuni ya madawa ya Gossage; mashinado haya hayakuwa na uhusiano na yale mashati ya Gossage, Shikibo, na Kurabo yaliyokuwa maarfusu sana wakati huo. Gossage Cup ilikuwa inahusiha nchi za Kenya, Uganda, Tanganyika na Zanzibar tu. Kipindi hicho kulikuwa na wachzaji maarufu sana kama Joe Kadenge na Livingstone Madegwa wa Kenya, Joseph Massajage kipa wa Uganda, na Mohamed Msomali na Maulid Dilunga wa Tanzania.


Mashindano haya yaliendelea hadi mwaka 1973 ambapo nchi za Somalia, Zambia na Ethiopia zilijiunga na mashindano hayo yakabilishwa jina na kuwa Ubingwa Afreika ya Mashariki na ya kati chini ya uongozi wa CECAFA ambao makao yake makuu yalikuwa Somalia kabla hayajahamishiwa Nairobi. Baadaye nchi nyingine kama Sudan, Malawi, Zambia na Zimbabwe zikajiunga na mashindano hayo. Mwaka 1994 baada ya uhuru wa Afrika ya Kusini, nchi za Zimbabwe, Zambia, na Malawi zilijitoa katika mashindano haya wakaanzisha ya kwao huko kusini, hivyo nchi za Rwanda, Burundi, Jibuti na Eritrea zikakaribishwa katika mashindano hayo. Wakati huo Rwanda ilikuwa katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

Historia ya washindi wa mashindano haya kuanzia mwaka 1974 ni kama ifuatavyo.

1974 Simba - Tanzania
1975 Yanga - Tanzania
1976 Luo Union- Kenya
1977 Luo Union - Kenya
1978 KCC - Uganda
1979 AFC Leopards- Kenya
1980 AFC Leopards - Kenya
1981 Gor Mahia - Kenya
1982 AFC Leopards - Kenya
1983 AFC Leopards - Kenya
1984 AFC Leopards - Kenya
1985 Gor Mahia - Kenya
1986 El Merreikh - Sudan
1987 SC Villa - Uganda
1988 Breweries - Kenya
1989 Tusker - Kenya
1990 Not held
1991 Simba SC - Tanzania
1992 Simba SC - Tanzania
1993 Yanga - Tanzania
1994 El Merreikh - Sudan
1995 Simba SC - Tanzania
1996 Simba SC - Tanzania
1997 AFC Leopards - Kenya
1998 Rayon Sport - Rwanda
1999 Yanga FC - Tanzania
2000 Tusker FC - Kenya
2001 Tusker FC - Kenya
2002 Simba SC - Tanzania
2003 SC Villa - Uganda
2004 APR FC - Rwanda
2005 SC Villa - Uganda
2006 Police - Uganda
2007 APR FC - Rwanda
2008Tusker FC - Kenya
2009 - Atraco FC - Rwanda
2010 APR FC - Rwanda
Utaona kuwa timu za Kenya na Tanzania zilikuwa mabingwa wa mashindano haya mara nyingi sana hadi mwaka 2002 ambapo kibao kiligeuka kikawa zaidi kwa Rwanda na Uganda. Kuanzia mwaka 2002, Tanzania imetwaa ubingwa huo mara moja, Kenya mara moja, Uganda mara tatu, na Rwanda mara nne.

Hii inanirudisha kuwa uongozi wa Kagame, japo ni wa mkono wa upanga, umerudisha nidhamu sana huko Rwanda. Je matatizo yetu michezoni pia yanasababishwa na viongozi wa nchi kwa jumla ambao wamsheindwa kujenga nidhamu za kazi ?
 
Back
Top Bottom