CEO wa Yanga alifungiwa maisha kujihusisha na soka Zambia

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001

Baada ya Yanga kumtambulisha Andre Mtine kama Mtendaji Mkuu wao mpya nimepitia vyanzo mbalimbali vimeonesha kuwa ana rekodi za kesi na tuhuma mbalimbali.

1- KESI YA UTAKATISHAJI FEDHA (2007) NDOLA, ZAMBIA ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฒ

- Andre Mtine alikamatwa na Mamlaka nchini Zambia kutokana na sakata la utakatishaji fedha wa kiasi na wizi wa kiasi cha Kwacha Million 100 sambamba na Maofisa wawili waandamizi ndani ya benki ya Posta ya Zambia.

Wahusika walikuwa Mtine, 43, a Football Association of Zambia (FAZ) Finance manager, Gilbert Kapambwe, 42 na Financial accountant Ignatius Kapembwa.

[Chanzo: The Times of Zambia ]

2- KUKAMATWA NA MAMLAKA ZA UHAMIAJI ZAMBIA ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฒ 2013

Mtine alikamatwa na Mamlaka za Uhamiaji nchini Zambia mnamo tarehe 18- 10- 2013 majira ya saa 6:30 mchana kutokana na kuvunja sheria za Uhamiaji kwa wachezaji watatu Stopilla Sunzu, Nathan Sinkala na Reinford Kalaba ambapo baadae waliitwa kutoa maelezo na wakaachiwa.

[Chanzo: Lusaka Voice]

3- KUKAMATWA NA MAMLAKA KUHUSU WACHEZAJI WA TIMU YA TAIFA YA ZAMBIA ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฒ (2014)

- Mtine inasemekana alishawishi wachezaji Nathan Sinkala na Stopilla wasusie mechi ya timu ya taifa ya Zambia dhidi ya Japan, huku pia FAZ wakisema wazi yeye ndie chanzo cha mgogoro kati yao na klabu ya TP Mazembe.

Alifungiwa maisha kujihusisha na soka nchini Zambia.

[ Chanzo: Lusaka Voice]

My Take
Ina maana Utopolo hamkumgugo huyu mtakatisha fedha? Au mmemchukua kimkakati kama mtalaam mwenye uzoefu wa kupiga?
 
Hata Ismail Aden Rage, Evance Aveva, Geofrey Nyange 'Kaburu', Zakaria Hancepope, Michael Wambura, na wengineo wengi! Wameshawahi kufungwa, kufungiwa kujihusisha na mpira, kukaa mahabisu kwa miaka kadhaa, nk kwa sababu ya wizi wa fedha za chama cha mpira wa miguu Tanzania, na pia wizi kwenye klabu yako ya Simba.

Hivyo hakuna jipya hapo. Mtu kama Ismail Aden Rage aliwahi kuwa mpaka Mwenyekiti wenu wa klabu mara baada tu ya kutoka jela. Sasa shida iko wapi kwa huyo Mzambia?
 
Hii mada imejadiliwa sana leo. Sijui ulilala? Kwa taarifa yako ni kwamba mahakama ilimsafisha na akaondolewa ban. Hata sasa ni mjumbe wa kamati mojawapo ktk Chama cha Soka Zambia
 
Ujinga mtupu watz wajo kibao wanna elimu kubwa alfu unaenda kuajir mkongo mjinga anakimbia risasi za uko Kuja Happ kutuonesha nn

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Morison + CEO,+ Manara = genge la waharifu. Wachezaji wataibiwa hadi zile nguo zao zenye vinyesi

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Hakuna watu wasiokuwa na furaha kwasasa kama Panya Road na mashabiki wa MAKOLO!,Na ukizingatia mashabiki wa MAKOLO ndo hao hao Panya Road,yaani mateso wanayopitia ni Jemedari binti kazumari tu ndiye anayejua![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dah ... Mi hayo Makesi kesi Yake Sijui Uhujumu Uchumi, Sijui Kutakatisha Pesa Na Rushwa Siwezi kuyasemea Maana Bado Sijaperuzi Mafaili...!

Isipokuwa Kilichonishitua ni Mbona Mzee Sana..! Yaani CV zote zilizotua Mezani Wameona ya Huyu Babu Mtine,
ndo Watuletee Wastaafu Kujichotea Pensheni Burebure...!
 

Sijawahi ona shabiki kichwa box kama wewe,unawaaibisha wenzako.Ni aibu JF kuwa na member kichwani hamna kitu kama wewe
 
Sijaona popote madai hayo kama yana uwiano na utekelezaji wake wa majukumu hapo Yanga.

Namtakia kila la heri.
 
Mzambia amepigwa life ban kujishughulisha na mpira wa miguu.
 
Mzambia amepigwa life ban kujishughulisha na mpira wa miguu.
Weka huo ushahidi wa kupigwa life ban mkurugenzi. Kama huna, basi jinyamazie tu kimya, ili CEO wetu atimize majukumu yake ya U CEO kwa utulivu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ